Mwaka 1811, Tecumseh, kiongozi wa jadi marekani na vijana wake walikabiliwa na jeshi la marekani likiongozwa na William Henry Harrison. Vita vilipigwa katika Mto Tippecanoe na kumalimalizika kwa kushindwa kwa Tecumseh na kusababisha kifo cha kaka yake, Tenskwatawa. Vita hiyo ilitokana na kutetea eneo lao dhidi ya upanuzi mkubwa wa ardhi wa Marekani hadi magharibi. Tecumseh alikufa miaka miwili baadaye katika Vita vya Thames alipokua akiwasaidia Waingereza kupambana na Wamarekani.
Hapa ndo patamu sasa
Kulingana na simulizi, Tecumseh alitoa laana ambayo imewasumbua wamarekani kwa takribani miaka 200. Laana ilikuwa kwamba kila rais wa Marekani atakaechaguliwa katika mwaka unaogawanyika na ishirini na kuishia na sifuri atakufa kabla ya kumaliza kipindi chake.
Laana hii ilidhihirika mwaka 1841 wakati William Henry Harrison alipokufa kwa homa ya tumbo (typhoid) miezi michache baada ya kushinda uchaguzi mwaka 1840. Tangu wakati huo, laana hiyo hiyo ilipewa jina la "Laana ya Tippecanoe" au "Laana ya Tecumseh,".
Marais wengine waliokumbwa na laana hii ni

Abraham Lincoln, alichaguliwa mwaka 1860 na kuuawa mwaka 1865.
James A. Garfield alichaguliwa 1880, mwaka 1881 akapigwa risasi na kufa baadaye mwaka huo huo.
William McKinley alichaguliwa tena mwaka 1900. Alipigwa risasi mwaka 1901 na kufa wiki moja baadaye.
Warren G. Harding, aliyechaguliwa mwaka 1920. Alikufa kwa mshtuko wa moyo mwaka 1923. Uvumi unasema alilishwa sumu na mkewe.
Franklin D. Roosevelt, aliyechaguliwa tena mwaka 1940 kwa kipindi cha tatu, alipata kiharusi na kufa baada ya miezi 3 kuingia muhula wake wa nne mwaka 1945.
John F. Kennedy alichaguliwa mwaka 1960. Aliuawa mwaka 1963.
Ronald Reagan alichaguliwa mwaka 1980 lakini aliepuka kifo baada shambulio la risasi ya John Hinkley iliyomkosa kwenye moyo mwaka 1981.
George W. Bush alichaguliwa mwaka 2000, nae 2005 alikumbana na jaribio la kushambuliwa.
Ni Ronald Reagan na George Bush pekee ndio walionusulika kifo kutoka katika laana hii.
Mjadala kwa Sasa ni "Je, rais mteule wa Marekani 2020 bwana Joe Biden atafanikiwa kuepuka laana hii?"