Imani hii inaitwa Reincarnation (Kuzaliwa upya), ni imani ambayo ipo tangu miaka mingi sana, zaidi ya miaka 1000 iliyopita na bado inaaminika hadi sasa.
Reincarnation ni neno la kilatin lenye maana ya "entering the flesh again", yaani kitu kile kile lakini kinaingia sehemu mpya. Miongoni mwa watu wenye imani hii ni watu wa dini za Kihindu (Hinduism),Budha (Buddhism) na Jain (Jainism).
Wanaamini kuwa mtu anapokufa nafsi yake inabaki duniani na kutafuta mwili kwaajili ya kuzaliwa upya. Mtu anapozaliwa upya hakumbuki chochote kuhusu maisha yaliyopita na anaweza kuzaliwa upya akiwa katika muonekano ule ule wa kimaumbile (same physical appearance) au akazaliwa akiwa katika mwili mwingine.
Inaelezwa kuwa kama ukiota kuhusu maisha tofauti na unayoishi sasa, basi ni dhahiri nafsi yako ilitumiwa na mtu kabla kwa namna hiyo, au ukienda sehemu na ukahisi umeshawahi kufika au hata kuota kuna sehemu kama hiyo, ni uthibitisho kuwa mtu mwingine aliyewahi kutumia nafsi yako alifika eneo hilo.
Licha ya dini hizi kuwa na imani sawa kuhusu kuzaliwa upya, lakini zinatofautiana kuhusiana na ukomo wa idadi ya kuzaliwa upya. Kuna wanaoamini hakuna ukomo wa idadi ya kuzaliwa upya, wengine wanaamini mwisho mara 7 na wengine mara 13.
Wanaoamini ukomo wa mara 13 wanaamini mtu akishazaliwa upya mara 13 ndipo nafsi yake hupotea jumla duniani, yaani ukifa basi roho yako atazaliwa nayo mtu mwingine, naye akifa itahamia kwa mwingine hadi mkifika watu 13 nayo inapotea mazima.
Kulingana na imani hii kuna namna ya kujua wewe ni uzao wa ngapi wa nafsi yako.
Mfano mimi nimezaliwa tarehe 18.03.1996, unajumlisha namba zote katika tarehe yangu ya kuzaliwa 1+8+0+3+1+9+9+6 unapata jumla 37. Alafu unajumlisha tena namba hizi

3+7=10, Jibu unalopata ndiyo idadi ya uzao wa nafsi yako uliopo, Kwahiyo mimi ni mtu wa 10 katika uzao wa nafsi niliyonayo, nikifa atazaliwa nayo mtu mwingine wa 11 hadi ifike mwisho 13.
Wanaamini kuwa binadamu anaishi mara moja, lakini roho yake inaishi maisha 13 ndipo inapotea kabisa duniani, japo inakuwa haina kumbukumbu yoyote juu ya maisha mengine ya nyuma.
Pia inaaminika kwamba watu wanazaliwa upya ili kukamilisha yale waliyopanga kabla ya kufa.