Nadhani wengi wetu humu tushawahi kusikia au kushuhudia vile vimbwanga vya vyoo vya shuleni, wanafunzi kuona vitu vya ajabu, kusikia sauti za ajabu na harufu za pirau chooni. Sasa bwana sio bongo tu hadi nchi za wenzetu huko mambo haya yapo.
Huko Japan kuna Hanako-san, Hanako-san ni mzimu wa msichana ambaye anasumbua katika vyoo vya shule. Maelezo kuhusu sura na mwili wake hutofautiana, lakini anaelezewa huonekana amekata nywele na kuvaa sketi nyekundu.
Maelezo kuhusu asili ya Hanako-san pia yanatofautiana kulingana na vyanzo tofauti tofauti. Kuna wanaosema kuwa Hanako-san alikuwa mtoto aliyeuawa na mzazi mnyanyasaji katika choo cha shule; Wengine husema, alikuwa msichana aliyejiua katika choo cha shule na wengine wanadai alikuwa mtoto aliyedondokewa na ukuta wa choo wakati wa Vita vya pili vya dunia.
Inasemekana Hanako-san mara nyingi anaonekana katika vyoo vya wasichana. Ukitaka kumuona unabisha hodi mara tatu katika mlango wa choo au kuita jina Hanako-san ndipo anaitika.
Kulingana na hadithi hiyo, mtu anaebisha hodi au kumuita Hanako-san anaweza kuona damu, mkono au Hanako-san mwenyewe. Hanako-san anaweza kumvuta mtu huyo kwenye choo na kusababisha kifo kwa mtu huyo au Mtu huyo anaweza pia kuachwa bila
kudhuliwa lakini anaweza kuwa anamuona Hanako-San akiangalia kwenye kioo.