"Kwa taarifa tulizonazo mpaka jana jioni zaidi ya Watu Bilioni 3.9 karibu Watu Bilioni 4 Duniani walikuwa wanafuatilia tukio la kumuaga Hayati Magufuli Kitaifa jana Dodoma na naamini leo pia itakuwa hivyo, tunawashukuru Waandishi wa Habari kwa kazi nzuri”- Waziri Mkuu Majaliwa, Zanzibar
Kutoka Chato hapa ni Uwanja wa Michezo wa Magufuli, zitakapofanyika shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli March 25 2021, nyumbani kwake Chato na mwili wake kupumzishwa March 26 2021.
Kutokea Visiwani Zanzibar katika Uwanja wa Amaan, Mjini Magharibi, hizi ni picha za Wananchi walivyomuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dr.John Pombe Magufuli.
Msafara uliobeba mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dr.John Pombe Magufuli ukielekea Ikulu ya Zanzibar ambapo mwili huo utalazwa Ikulu kisha March 24 utapelekwa Mwanza.
Hillary Clinton ambae ni Mke wa Rais wa zamani wa Marekani pia Mgombea Urais wa Marekani mwaka 2016 ni miongoni mwa waliotumia kurasa zao za Twitter kumtakia kila la kheri Rais mpya wa Tanzania na Mwanamke wa kwanza kuwa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan.
Hillary ameandika ———> “Best wishes to SuluhuSamia Tanzania’s new president and the first woman to hold the office, as she leads and serves her country”
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.