Makapuku Forum

Makapuku Forum

Msaidizi wa Rais "Mpambe" wa Rais (ADC-Aide De Camp) Kanali Bernad Paulo Masala Mulunga, wewe ulizoea kusimama nyuma ya Rais kuhakikisha yu salama. Tulizoea kukuona kila alipo Hayati Rais Dkt John Magufuli.

Leo hii unatoa heshima za mwisho, wewe umesimama kwa ukakamavu, yeye amelala, amelala kwenye jeneza, amelala na hatoamka tena. Watanzania tunakushukuru kwa utumishi wako

20210322_170145.jpg
 
Mama yetu Samia Suluhu, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amiri Jeshi Mkuu maneno yako yametutia moyo, yametufariji, yametupa matumaini.

Tunaomba maneno yale yakutie nguvu nawe pia. Mungu ibariki Tanzania, Mungu akubariki Rais wetu.
View attachment 1731793
20210322_170523.jpg
 
“Naomba kuungana na kauli ya Rais wetu Mama Samia, Watanzania tuendelee kushirikiana, kuzidisha upendo, umoja na mshikamano miongoni mwetu huku kila mmoja kwa imani yake tukiendelea kumuombea Mpendwa wetu kwa Mwenyezi Mungu”- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye shughuli za kumuaga Hayati Magufuli

“Watanzania, naomba tuendelee kutenda mema, nasi Viongozi tutaendelea kuendeleza yote aliyotenda na kubuni yenye muelekeo wa mambo aliyoyafikiria Rais Magufuli kuwa yataifikisha Tanzania mahali pazuri”- MAJALIWA

“Nawashukuru sana Madaktari na Watu wa Msalaba Mwekundu waliojenga vibanda vya huduma ya kwanza na kutibu waliofikwa na matatizo ya kiafya huko Dar es Salaam na maeneo mengine wakati wa kumuaga Mpendwa wetu”- MAJALIWA

“Nawashukuru Vyombo vya Habari kwa kazi ya kuwaelekeza Watanzania kila hatua ya matukio ambapo Watanzania wote sasa wamepata uelewa wa ratiba ya kumuaga Hayati Rais Magufuli”- MAJALIWA
RIPHayatiMagufuli
20210322_170950.jpg
 
Rais Mstaafu Mzee Jakaya Kikwete na Rais Mstaafu Mzee Ally Hassan Mwinyi wakiwa kwenye shughuli za kuuaga mwili wa Hayati Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma leo.

RIPHayatiMagufuli
20210322_195546.jpg
 
“Hayati Magufuli alikuwa Muungwana aliyeona fahari kumsifia Mtu akiwa bado hai, hakuwa Mtu wa kujikweza ndio maana kwenye shughuli zote mliowaona Wastaafu, niwaombe Wastaafu Mimi ni Kijana wenu, hakuna kitakachoharibika, tutaendeleza alipoishia, tutafika alipopatamani”-Rais Mama Samia Suluhu kwenye shughuli za kumuaga Hayati Magufuli Dodoma leo

“Kupitia Hayati Magufuli Tanzania tulimpata Makamu wa Kwanza wa Rais Mwanamke na sasa ni Rais wa Kwanza Mwanamke Tanzania, nashukuru kupitia yeye alinipa nafasi na tukaonesha Wanawake tunaweza”- Rais Mama Samia

“Hayati Magufuli ameondoka lakini alishamaliza kazi ambayo alikuja kuifanya Duniani, kazi hiyo ilikuwa ni kutuonesha njia, kutuonesha kazi inavyofanywa, namna ya kutekeleza na kuchukua maamuzi magumu kwa Taifa, hatuna budi kufuata njia aliyotuachia”-Rais Mama Samia

RIPHayatiMagufuli
20210322_195707.jpg
 
“Naomba kuungana na kauli ya Rais wetu Mama Samia, Watanzania tuendelee kushirikiana, kuzidisha upendo, umoja na mshikamano miongoni mwetu huku kila mmoja kwa imani yake tukiendelea kumuombea Mpendwa wetu kwa Mwenyezi Mungu”- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye shughuli za kumuaga Hayati Magufuli

“Watanzania, naomba tuendelee kutenda mema, nasi Viongozi tutaendelea kuendeleza yote aliyotenda na kubuni yenye muelekeo wa mambo aliyoyafikiria Rais Magufuli kuwa yataifikisha Tanzania mahali pazuri”- MAJALIWA

“Nawashukuru sana Madaktari na Watu wa Msalaba Mwekundu waliojenga vibanda vya huduma ya kwanza na kutibu waliofikwa na matatizo ya kiafya huko Dar es Salaam na maeneo mengine wakati wa kumuaga Mpendwa wetu”- MAJALIWA

“Nawashukuru Vyombo vya Habari kwa kazi ya kuwaelekeza Watanzania kila hatua ya matukio ambapo Watanzania wote sasa wamepata uelewa wa ratiba ya kumuaga Hayati Rais Magufuli”- MAJALIWA
RIPHayatiMagufuliView attachment 1731795
...huyu jamaa hata siamini anachosema, alituhakikishia kabisa kuwa tusiwe na wasiwasi kumbe ni jiongo kuu la mawaziri
 
Asante Shunie kwa kutuhabarisha hapa jukwaani. Pamoja sana
Anco Lee simu zangu sio kwamba sipokei ila zimeibiwa, wakati tunaaga kumbe wengine wanafanya yao, nimeibiwa simu na saa yenye bluetooth
 
Kutoka Mwanza ni maandalizi yakiendelea kufanyika Uwanja wa CCM Kirumba sehemu ambayo itatumika kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli March 24,2021.

Wananchi wa Mwanza na mikoa jirani watapa nafasi hiyo kabla ya mwili wa Hayati Rais Magufuli kuelekea Chato mkoani Geita ambako utapumzishwa March 26,2021 nyumbani kwake Chato.
RIPHayatiMagufuli
20210323_161420.jpg
20210323_161420.jpg
20210323_161351.jpg
20210323_161449.jpg
20210323_161510.jpg
20210323_161510.jpg
 
Umoja wa Mataifa umesema Bendera ya Umoja wa Mataifa itapepea nusu mlingoti Makao Makuu ya Umoja huo New York Ijumaa March 26 kumuenzi Hayati Dr. John Pombe Magufuli, Ofisi ya Itifaki imesema Ofisi zote za UN duniani zimehimizwa kufanya hivyo pia.
20210323_161543.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom