Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210109_081643.jpg
 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais - TAMISEMI David Silinde amemkabidhi Mwalimu Mkuu wa Ikhanoda Secondary, Wilayani Singida, Omary Selestine kwa Polisi na TAKUKURU baada ya kugundua matumizi mabaya ya fedha za umma katika ujenzi wa bwalo la chakula la wanafunzi wa shule hiyo.

Hayo yamejiri baada ya Silinde kufanya ziara katika shule hiyo kukagua mradi wa lipa kutokana na matokeo ambao shule hiyo walipewa kwa ajili ya ujenzi wa bwalo lakini mpaka sasa fedha zaidi ya milion 50 zimetumika huku ujenzi ukiwa katika hatua ya msingi.

"Huwezi nunua bati za milioni 70 unataka kujenga nini?, au unanunua tofali kwa Tsh. Elfu 5 ni tofali aina gani?, mchukueni huyu mwalimu na kamati nzima ya ujenzi wakaeleze wametumiaje fedha za ujenzi wa mradi huu”-Silinde

Silinde pia amemsimamisha kazi Mwalimu Mkuu huyo na kuvunja kamati ya ujenzi ya shule hiyo na kumvua madaraka Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo baada ya kushindwa kusimamia ujenzi wa bwalo la chakula katika shule hiyo.
20210109_084220.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amesema kiwanda cha saruji cha Dangote kitaanza rasmi uzalishaji Jumatatu January 11, 2021, ametoa kauli hiyo baada ya kutembelea kiwanda hicho kuona maendeleo yake na kupata taarifa kutoka kwa CEO wa kiwanda Abullahi Baba.

Kiwanda hicho kilisimamisha uzalishaji kwa Wiki kadhaa kutokana na hitilafu za kiufundi.

“Nimefarijika kutembelea kiwanda cha cement hapa Dangote na kujionea hatua waliyofikia katika matengenezo ya mtambo ulioleta hitilafu na kupelekea kusitishwa kwa uzalishaji wa saruji "
20210109_084436.jpg
 
“Naipongeza Kampuni ya Kichina kwa kushinda zabuni ya ujenzi wa reli ya kisasa Kilometres 341 kutoka Mwanza hadi Isaka( mradi una gharama ya Tril 3.0677), nina matumaini watafanya kazi kubwa”-JPM mbele ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi leo Chato

“Nimemuomba Waziri Wang Yi, akafikishe salamu zangu kwa Rais Xi Jinping kwamba watusamehe madeni yakiwemo ya USD Mil. 15.7 ya deni tulilobeba wakati wa ujenzi wa reli ya TAZARA, deni la USD Mil.137 la nyumba za askari pamoja na deni la kiwanda cha Urafiki la USD Mil.15, nimeomba watufutie kwasababu China ni Rafiki zetu, pia wao ni Matajiri”-JPM

“Nimewaeleza hali halisi kwamba China ni Nchi Tajiri Duniani, na sisi Tanzania tuna mazao mengi, ndio maana kwenye zawadi zangu nimetoa korosho, chai na kahawa, nataka wakaanze kula korosho za Tanzania badala ya Nchi nyingine, huu ndio wakati wa kulishika soko la China”-JPM

“Nampongeza sana Waziri Wang Yi kwasababu hajavaa barakoa maana anajua Tanzania hakuna Corona na kwa kumuhakikishia nakwenda kumshika mkono tukale chakula
20210109_084644.jpg
 
Maelfu ya Wakulima Nchini India wameandamana wakiwa na Matrekta na kuifunga Barabara kuu karibu na New Delhi ili kuishinikiza Serikali kuachana na muswada mpya wa Sheria ya usimamizi wa mashamba ambao Wanadai unawaumiza Wakulima.

Muswada huo pamoja na mambo mengine unamzuia mkulima kuuza mazao yake moja kwa moja kutoka shambani kwa Mfanyabiashara/Mteja bila usimamizi wa Serikali, kitu ambacho Wakulima wanaamini kitafanya faida ya kuuza mazao kuwa ndogo zaidi, Serikali na Wakulima watakutana leo kujadili hilo.

“Haiwezekani nilime mwenyewe ndizi, nyanya, vitunguu nk na nikatazwe kumuuzia mteja shambani kwangu kisa Serikali inataka inipangie bei au ipate ushuru mkubwa, mbona hawajanisaidia kulima?”-Mkulima
(Swipe kuona picha nyingine)
20210109_090223.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom