Makapuku Forum

Makapuku Forum

Jaman ifike mahali tuheshimiane, nimevumilia sana ila nimeshindwa. Kwa maoni yangu na sitaki kumponda mtu yeyote, baada ya kutafakari sana na kupima uzito kwa pande zote, ninachodhani na ninadhani na nyie pia mtakubaliana na mimi, maana ni jambo lipo wazi kabisa, ikibidi nitakumbusha na mifano kadhaa kwa mustakabali wetu kama kikundi, mi naomba tu niseme na nina sababu za kuamua kulisema hili hapa. Kwa sababu zilizo wazi na nahisi na nisinukuliwe vibaya nasema hivi,(ingawa kiukweli sijali itakavyotafsiriwa na wengine) na pia nataka wote muwe mashahidi, kwakweli hata sikumbuki nilikuwa nataka kusemaje.
 
WAPENDANAO WAKI POST PICHA

WAZUNGU: Me and My Bae

WABONGO: Ulinikuta nikiwa nimeshaumizwa moyo pamoja na kifua, ukanijali na kunipunguza maumivu, Kama ingekua kukupenda wewe ni dhambi, acha niende motoni. Nakupenda Sana mpenzi wangu, Siwezi Kuishi bila Wewe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom