Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nimecheka mpaka kwenye daladala wananishangaa
Jana usiku kuna Jirani yangu..kanitumia text "mambo vipi?"…halafu tunakaa nae mtaa mmoja nikaona nikimjibu ni uharibifu wa hela nikaenda kumgongea mlango saa 7 usiku. Alipofungua nikamjibu "shwari"halafu nikarudi nyumbani kulala zangu.. Sipendagi kuchezea salio..
 
Kweli kabisa
Maisha yetu ni kama mti wa matunda. Kuna wakati unapukutisha majani, kuna wakati unakuwa na maua, wakati mwingine unakuwa na matunda mengi yenye kuvutia, wakati mwingine matunda yanaisha kabisa. Usijichukie uwapo kati ya kipindi kimojawapo. Usihukumu maisha yako kwasababu ya kosa moja! Au kwasababu ya magumu ya wakati mmoja, vumilia kipindi cha matunda kinakuja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom