Uji huo ni mjumuisho wa nafaka mbalimbali na mara nyingine mpaka mboga mboga.
Kwa kawaida huchanganywa Mahindi, Mchele, Ulezi, soya, mtama, karanga na dagaa au Mahindi, ulezi, soya, mchele, karanga, ngano, ufuta.
Mchanganyiko hutegemea ni nani ambaye ametengeneza.
Kwa sasa unga huu umekuwa biashara muhimu kwa baadhi ya watu. Kwani huchanganya na kusaga kisha kuwauzia watu ukiwa katika vifungashio mbalimbali.
Baadhi ya kina mama huchanganya nafaka na kutengeneza wenyewe unga huu wa lishe kwaajili ya watoto wao na si biashara.