Makapuku Forum

Makapuku Forum

mambo mengi ya kufanya ili tuwe watu wa kuvutia kila wakati.Mpangilio wa mavazi hufanya mtu kuonekana maridadi.
Kama wewe ni mvaaji wa tai unapovaa unazingatia mambo yapi? Na je unafunga tai yako kwa namna inayokubalika?
Wengine huwa hawafahamu jinsi ya kufunga tai na hivyo kuleta mushkeri wakati wa kuvaa tai na kusababisha tai kukaa upande. Unapoamua kuvaa tai na shati ambalo halijanyooshwa ambalo linakuwa kwenye mikunjo au kuvaa tai na ndala unakuwa umeua maananzima na kulivunjia heshima vazi hili.
 
Tai ni vazi lawatu walio maridadi kama huwezi kuwa maridadi basi vazi hili halikufai kabisa.
Unapovaa taa unatakiwa kuzingatia aina ya umbo lako kama wewe ni mnene vaa tai inayoendana na mtu mnene na kama wewe ni mwembamba basi vaa tai inayoendana na mtu mwembamba.
Kuna wengine huvaa tai zinazofika magotini na kuwa kichekesho anapopita mtaani
 
Tai ni vazi ambalo huongeza heshima na hadhi ya mvaaji cha muhimu ni jinsi gani unavaa tai yako na ikiwezekana jaribu kumechisha tai na suruali kwa vile ili tai upendeze ni laima iendane na nguo unayovaa.
Ni vyema ukahakikisha kuwa unakuwa na tai zenye rangi tofauti ambazo zitaendana na nguo unazovaa.
mwisho
 
Kama huna uhakika nini kinakuletea mushkeri, ni vyema kutafuta viashiria vyake kwa kumuona mtaalam wa aleji.
Sehemu kubwa ya aleji haitibiki, san asana wataalam watakupatia dawa Fulani za kukusaidia kupunguza makali, lakini kwa vyovyote vile hali hii unaweza kuimudu mwenyewe kwa kuhakikisha unaondokana na ulaji au utumiaji wa vipodozi vya ovyo ovyo.

...nilikatazwa kunywa maziwa ili kuondokana na kuwashwa lakini haikusaidia kila wakati fulani wa msimu unapoanza basi ni kuwashwa hasa wakati nimemaliza kuoga. walikata ngozi (biopsy) kuangalia nini tatizo maana kama ni dawa za kunywa na kupaka nimetumia. Sasa, mitishamba inasaidia kidogo.

Asante kwa somo
 
Umuhimu wa kuvaa hereni

Hereni ni mapambo yanayovaliwa masikioni.
Kuna aina nyingi za hereni katika tamaduni mbalimbali. Heleni hutengenezwa kwa kutumia madini ya thamani kama dhahabu au diamond.
Pia hutengenezwa kwa kutumia silver na almasi.
Lakini pia kwa kutumia ubao, mfupa au kioo, vifuu vya nazi na Kutokana na tamaduni mbalimbali, hereni zimekuwa zikivaliwa zaidi na wanawake, wanaume au jinsia zote mbili.
Mara nyingi uvaaji wa heleni unatakiwa kuzingatia aina ya nguo uliyovaa, hapo unatakiwa kucheza na rangi.
Mpangilio wako wa nguo na hereni hata na viatu utakufanya uonekane maridadi muda wote.
 
Wanawake wa kimasai wamekuwa wakijipamba kwa mapambo
ya shanga hali ambayo inawafanya wazidi kudumisha
utamaduni wao.
Pia hereni zilizotengenezwa kwa shanga zimekuwa zikiwavutia watu wengi kuvaa kutokana na nakshi yake
 
Uvaaji wa bangili na maana zake

BANGILI ni kitu kilichotengenezwa kwa lengo la kuvaliwa mkononi kama saa.
Bangili hutengenezwa kwa kutumia ngozi, kitambaa kigumu, plastiki, chuma, na wakati mwingine huwa na nakshi za aina mbalimbali.
Fasheni za bangili hutegemea na matakwa ya mavaaji kwani kuna wale ambao wanapenda kuvaa bangili zilizotengenezwa kwa vito vya thamani kama dhahabu na almasi na wengine wakipendelea kuvaa bangili zilizotengenezwa kutokana na vitu vya asili.
 
Bangili licha ya kuwa ni urembo wa mkononi, wakati mwingine hutumika kama alama hasa kwa wagonjwa wanapokuwa hospitalini na hutumika kama alama ya mgonjwa.
Hapa nchini kumekuwa na wasanii wa uchongaji ambao
hutengeneza bangili kwa kutumia magome ya miti na wakati mwingine kwa kutumia vifuu vya nazi.
 
Inaaminika kuwa bangili ambazo hutokana na vifuu vya nazi zimekuwa zikipendeza kuvaliwa kutokana na muonekano wake kwa ujumla na pia huuzwa kwa gharama nafuu ambapo wengi wanamudu kununua kuliko bangili zilizotengenezwa kwa vito vya thamani.
Uvaaji wa bangili pia unatakiwa kuzingatia rangi ya mvaaji, kama mtu ni mweusi anashauriwa kuvaa bangili zenye mng'ao ili kuweza kuwa na muonekano mzuri.
Ni vizuri kama tutazingatia mpangilio wa rangi katika uvaaji wa bangili na itapendeza kama uvaaji huo utazingatia na rangi ya nguo au viatu.
 
Uondoji wa nywele katika maeneo flani
MWANAMKE na hata mwanaume anatakiwa kuwa msafi na si usafi wa kubahatisha.Sehemu ya nywele za siri zimeelezwa kuwa ni sehemu ambapo ngozi yake ni yenye kuhitaji uangalifu mkubwa wakati wa kuziondoa.
Hizi si nywele za kawaida na haziwezi kuondolewa kiholela.Sehemu zinazokaa nywele hizo ni kwapani na maeneo ya faragha.
 
Kutokana na unyeti wa ngozi katika maeneo hayo watu wa fasheni wamekuwa wakisisitiza kuwa waangalifu zaidi wakati wa kuyafanyia usafi.
Maeneo haya yanatakiwa yaachwe bila mikwaruzo wakati wa marekebisho ya kiusafi yanapofanyika.
Pamoja na kwamba uondoaji wa nywele hizo hauna shida sana wengi wa watu wanapata shida sana baada ya kuondoa nywele husika.
 
Hii inatokana ama na vifaa vinavyotumika katika uondoaji au ule ukweli wa kawaida kwamba maeneo hayo yanahitaji kuangaliwa kwa makini.
Wengi wetu hunyoa maeneo hayo kwa kutumia nyembe na hii pia huleta matatizo ya kiufundi katika ngozi husika.
Wengine hufanya kitu kinachoitwa Waxing lakini kina maumivu makubwa kwa kuwa nywele huchomolewa kutoka katika kiini chake.
 
Hata hivyo ukifanikiwa kuondoa unakaa muda mrefu kabla ya kupata shida nyingine.
Ukifanya mwenyewe kazi hii utachanganyikiwa,manake unaweza kuzua uwasho wa kutia aibu kutokana na ngozi yako kukataa kusalimu amri kwakazi yako mwenyewe. Nywele zinazokua ndani huwa tatizo kubwa, njia hii huleta matatizo makubwa.
Unaweza kutumia utaalamu wa kisasa wa kuondoa moja kwa moja nywele hizo, lakini unahitaji fedha na hii ndio shida yenyewe, si kila mtu ana fedha za kufanya mambo hayo.
 
Uondoaji huu wa kudumu wa kutumia laser huchukua muda mwingi na ama hakika ni miezi kadhaa na hii hakuna mtu anayeitaka.
Bado wapo baadhi ya wanawake ambao wanafanya juhudi za kunyoa na pia kung'oa nywele hizo katika muda mbalimbali.
Lakini pia ukienda kwa wataalamu wanaweza kukupatia vitu vya kuondoa nywele hizo kwa raha kubwa.
Zipo pia kemikali za kuondoa nywele ambapo huzihitaji shauri ni kwenda kwa saluni -zinazohusika.
 
Back
Top Bottom