Makapuku Forum

Makapuku Forum

Jinsi ya kurembesha macho

UNAWEZA kuweka macho yako katika hali ya kupendezanakuhakikisha yanakuwa na mvuto wa kipekee.
Kama unataka kufanya macho yako yaonekane meusi pakawanja kulingana na aina ya macho yako bila kujali kama kamauna macho makubwa au madogo.
Kama una macho madogo unatakiwa kuchora mstari pembenibaada ya kupaka wanja, hii husaidia watu wenye machomadogo kuonekana kuwa wana macho makubwa.
 
Anzia kupaka kwenye kona za macho wakati mwingineunatakiwa kushikiria jicho wakati wa kupaka wanja.
Watu wenye macho makubwa wanashauriwa kupaka wanjawenye mistari myembamba ambayo inanakshiwa na urembo ndani yake.
Unatakiwa kuhakikisha kuwa, wanja unaotumia hauna madharakwa macho yako kwani kuna aina nyingine ya wanja mtuanapotumia macho huwasha au hutoa machozi.
 
Pia usipende kutumia kila aina ya wanja kwa ajili ya usalamawa macho yako, unaweza kutumia bidhaa za kampuni moja tu nasi kubadilibadili kila wakati.
Wakati wa kupaka wanja fuata mstari na rudi hivyo kwa marambili nyingine hadi kuhakikisha kuwa wanja umekolea vizuri.
Pia unaweza kutumia pamba kwa ajili ya kupaka shedo juu yamacho kwa rangi ambayo umechagua.
 
Hakikisha kuwa, unapokuwa unatengeneza macho yakounatakiwa ukae kwenye kioo na uwe umetulia ili kuwezakutengeneza macho yako vizuri huku ukitumia kioo ambacho kitakuonyesha vizuri.
Ni vizuri kuchagua tangi za kupaka na ni heri pia kama rangiunazochagua zinaendana na nguo au kiatu utakachovaa.Ni vizuri kupaka rangi ya kung'aa wakati wa usiku na pia rangizilizotulia wakati wa machana.
Unaweza kupaka mascara kwa kutumia brash kwa ajili ya kurembesha kope zako ili ziweze kuinuka na kuleta mvuto katika macho yako.
 
Siri ya papai katika urembo wako


Tunda la kitropiki la papai lina vitamini C na E likiwa na siri
kubwa ya urembo na hutumika kutengeneza facial za aina mbalimbali.
Papai limekuwa likitumiwa kama njoia boya ya kutunza uso wako na
kumfanya mtu kuwa na ngozi ya asili.
Bidhaa ambazo zimekuwa zikitengenezwa kwa kutumia tunda la papai ni
pamoja na sabuni, lotion, tona, moisturiza, facial peels na nyingine
nyingi.
Ukitumia facial mask ya papai utakuwa na sura nzuri ya asili na kukupa
uonekanaji mzuri wa uso wako.
Facial mask hii huweza hutumika kwa watu wa umri na aina yoyote ya ngozi
 
Facial mask ya papai ina nguvu ya kung’arisha uso wako.

Pia inasaidia ngozi ambayo imeshaanza kupatwa na makunyanzi kutokana
na umri kuonekana ya kuvutia kwani pia imekuwa ikiondoa chunusi na
makunyanzi pia.
Ni rahisi kutengeneza facial mask ya papai na ukitumia itakusaidia
katika kukabiliana na ngozi iliyoanza kuchoka, kung’arisha ngozi
Kuna na njia nzuri za kuhakikisha kuwa, tunakuwa na nyuso nzuri zenye
kupendeza na kuvutia ikiwemo kutumia vitu vya asili pamoja na matunda
ya aina mbalimbali ambayo husaidia zaidi katika kuimarisha ngozi .
Mask ya mchanganyiko wa papai yai na yai ni nzuri katika kuhakikisha
kuwa unakuwa na ngozi nzuri na nyororo
 
Njia hii pia husaidia hata wale wenye nyuso za mafuta ambao wamekuwa
wakisumbuliwa na chunusi mara kwa mara kwa kufanya ngozi kuwa kavu.
Unaweza kutengeneza aina hii ya mask kwa kufanya yafuatayo:-

Chukua papai likate kasha toa mbegu na kasha lisage kwa kutumia blenda
ay kuondaponda kwenye kibakuli kwa kutumia kitukama mchi mdogo wa
kinu.
Kisha weka mchanganyiko huo kwenye chombo ulichokichagua kama kikombe au bakuli.
Vunja yai na koroga kuhakikisha kuwa mchanganyiko huo umechanganyika vizuri.
 
Safisha uso wako kwa kutumia cleanser au maji ya vuguvugu na uondoe
uchafu wote ulioganda usoni.
Kisha paka mask kuzunguka uso wako, na unapopaka hakikisha kuwa,
mchanganyiko huo haugusi macho yako.
Osha uso wako baada ya dakika 15 kwa kutumia maji ya vuguvugu. Jifute
kwa kutumia taulo safi
Unaweza kupaka losheni, tona au moisturiza.

Husaidia kutunza ngozi na kuondoa vipele na uchafu ulioganda usoni.
Hii ni njia rahisi ya kutengeneza uso isiyo na gharama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom