Makapuku Forum

Makapuku Forum

KUNA wanaume nawasifu kwa kuzingatia usafi wa mavazi yao na hata muonekano wao licha ya kuwa wengine wameamua kuliweka kando kidogo suala hili.
Unapokuwa mtanashati unakuwa na kila sababu ya kujiamini.
Usafi wa mwili umekuwa ukisisitizwa sana kutokana na ukweli kuwa usafi ni afya na muhimu kwa kila moja kuwa na tabia ya kuwa msafi wakati wote.
Usafi ni pamoja na kuoga na kutakata vizuri, kutorudia kuvaa nguo ambayo imevaliwa na inanuka jasho na hata kunyoosha nguo vizuri kabla ya kuvaliwa.
Singlet pamoja na kuvaliwa ndani ya shati pia zimekuwa zikivaliwa zaidi na wanamichezo ikiwemo mieleka na wale wa mbio ndefu.
 
Wengi wanavaa singlet ndani ya nguo nyingie iwe kwa wanaume au kwa wanawake
"Unaponunua singlet unazingatia zaidi ubora na kitambaa kilichotumika kutengeneza nguo hizo kama ni pamba au aina nyingine ya kitambaa, lakini wanaume wengi wanapendelea pamba zaidi" anasema mkazi mmoja wa Jijini Dar es salaam.
Uvaaji wa singlet unatakiwa kuzingatia zaidi usafi kutokana na ukweli kuwa nguo hiyo imekuwa ikivaliwa sana na wakati mwingine huathiriwa zaidi na jasho linalotoka mwilini.
 
Pia ni vizuri kuhakikisha usafi wa kwapa ili kuweza kuhakikisha kuwa,singlet yako inakuwa katika hali ya usafi muda wote na ili isiwe tabu kwako kuinua mkono kwani wengi wanaficha kwapa zao kutokana na uchafu kitu ambacho si kizuri.
Uvaaji huo unazingatia sana rangi kutokana na matakwa ya mvaaji ila wengi wanapendelea rangi nyeupe.
Nguo yoyote ya rangi nyeupe ni nzuri na inapendeza ikivaliwa kwani rangi nyeupe pia huonyesha kipimo cha usafi wako.
Kwa kina dada wanaopenda kuvaa singlet nao wanatakiwa kuhakikisha kuwa kwapa zao zinakuwa safi ili kuweza kuwa huru zaidi.
 
WANAWAKE wamekuwa na uchaguzi wa aina gani ya nguo ambayo inatakiwa kuvaliwa katika mtoko wa usiku.
Kuna wale ambao hupendelea kuvaa nguo za kung'aa na wale ambao hupendelea nguo za kawaida lakini zenye mitindo bora zaidi.
Uchaguzi wa nguo inayotakiwa kuvaliwa unatakiwa kuzingatia mambo mengi ikiwemo kuvaa kulingana na tukio husika, kama ni pati ya kawaida au ni kwa ajili ya sherehe fulani.
 
Uvaaji wako unatakiwa kuzingatia rangi ya nguo na rangi ya mwili wako.
Kama wewe ni mweusi hutakiwi kuvaa nguo nyeusi kwani haitakupendeza, unashauriwa kuvaa nguo za rangi nyeupe,nyekundu, gold, bluu au njano.
Na kama wewe ni mweupe nguo ya rangi nyeusi au rangi nyingine itakupendeza kulingana na rangi ya ngozi yako.
Nguo ndefu ni nzuri zaidi kama zitavaliwa kwa kiatu kirefu na kubeba mkoba mdogo.
 
Cha kuzingatia ni kuhakikisha kuwa nguo hiyo haikuletei tabu wakati wa kutembea kwani nguo ikiwa ndefu sana husababisha mvaaji kuishikilia na kuonekana wakati mingine kama kituko.
Vaa nguo kulingana na umbo na hata urefu wako, nguo za wazi na ndefu hupendeza sana kama zitavaliwa na mkufu au ushanga shingoni.
Jambo la muhimu ni kuhakikisha kuwa, unakuwa na nguo maalum ya kutokea na unatunza vizuri nguo zako kwani hilo litakusaidia kuongeza umaridadi wako na kujiamini zaidi.
 
MZIO wa ngozi au aleji ni tatizo linaloweza kukupata kutokana na mwili wako kukataa kitu fulani, hutokana na sababu ikiwemo hewa na hata chakula tunachokula.
Kimsingi ni matatizo ya mlipuko wa mfumo wa kuhami mwili kwa kutumia au kuwa katika eneo ambalo linatibua mfumo wa mwili kwa kitu ambacho pengine wengine wala hawana tatizo nacho.
 
Kuna vitu ambavyo huibua mzio kama vumbi katika nyumba, mavi ya panya, manyoya ya wanyama na hewa yenye aina ya spiriti.
Mzio unaweza kukufanya uwe na ukrutu, mafua, pumu na hata kuvimba kwa mwili.
Wapo watu ambao hupata tatizo la ngozi, kuwashwa na hata kujaa.
Kuna mambo mengi sana ya kujifunza, lakini inaonekana kuwa tatizo hili husababishwa na mazingira na wakati mwingine ni tatizo la kurithi.
 
Katika dunia ambayo inatamba sana na teknolojia, tatizo la mzio lipo kubwa na hasa kemikali zinazotumika katika vyakula na hata urembo vinapotibua kemikali zinazotengeneza aleji katika mwili.
Kuna dalili tofauti za kuelezea aleji (mzio), lakini ni kitu ambacho ama hakika kinaweza kutibua uzuri na urembo wako na hata wakati mwingine kufanya mtu usiwe na raha kwa kutokea ukurutu au kuvimba kwa mwili.
 
Kuna aleji mbaya kama za kuumwa na mdudu ambapo wengine hubadilika na kuvimba mwili au eneo na hata presha ya damu kupungua kabisa.
Pia kuna tatizo la kuwa na aleji na dawa na chakula.
Ninachotaka kukuambia kwa leo ni haja ya kuwa mwangalifu katika vitu vingi na mara nyingi inafaa mtu kuwa mtulivu na kuachana na kile kitu ambacho kinakuletea tabu.
 
Kama huna uhakika nini kinakuletea mushkeri, ni vyema kutafuta viashiria vyake kwa kumuona mtaalam wa aleji.
Sehemu kubwa ya aleji haitibiki, san asana wataalam watakupatia dawa Fulani za kukusaidia kupunguza makali, lakini kwa vyovyote vile hali hii unaweza kuimudu mwenyewe kwa kuhakikisha unaondokana na ulaji au utumiaji wa vipodozi vya ovyo ovyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom