Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wanamitindo wenye ulemavu wa ngozi wameshiriki katika shindano la kuiwakilisha Kenya katika mashindano makubwa ya Afrika mashariki ya kumtafuta Mr & Miss Albino.

Mashindano haya yamenuiliwa ubadili mtazamo wa jamii dhidi ya walemavu hawa.
Screenshot_20181030-184801.jpeg
 
Wanajeshi wakiwa wamemkamata Mbunge Alfred Yekatom maafuru Rambo kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR),

aliyefyatua risasi hewani akiwa ndani ya ukumbi wa bunge baada ya kuibuka kwa mvutano. Wabunge walikuwa wakivutana wakati wakijiandaa kupiga kura kuchagua spika wa Bunge.
Screenshot_20181030-185001.jpeg
 
Gari la kubeba watalii linalotumia nishati ya umeme wa jua (e-car) limezinduliwa rasmi katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Gari hilo linalomilikiwa na Mount Kilimanjaro Safari Club (MKSC) halipigi kelele hivyo kutosumbua wanyama, pia ni rafiki kwa mazingira kwani halitoa moshi.
Screenshot_20181030-185146.jpeg
 
Kampuni ya IPP imetangaza kuanza ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza simu (smartphone) zitakazokaa na chaji kwa wiki moja na pia zitafaa kuchajiwa kwa umeme wa jua.

Uwekezaji huo unakadiriwa kugharimu TZS 11bn, na uzalishaji utaanza ndani ya miezi 3 ijayo, ambapo utatoa ajira 2,000.

Screenshot_20181030-185246.jpeg
 
Meya wa Manispaa ya Iringa (CHADEMA), Alex Kimbe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi kujitafakari kwa kuomba radhi, ili kurejesha imani yake kwa watumishi wa mkoa huo. Amesema, kama Waziri (Selemani Jafo) ameomba radhi kwa niaba yake, na yeye ni lazima aombe radhi.
Screenshot_20181030-185458.jpeg
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza Novemba 15, 2018 kuwa ndio mwisho wa kupokea maombi ya uanachama wa CCM na kupewa dhamana ya uwakilishi kwa Wabunge na Madiwani kutoka vyama vingine.
Screenshot_20181030-185643.jpeg
 
Kampuni ya IPP imetangaza kuanza ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza simu (smartphone) zitakazokaa na chaji kwa wiki moja na pia zitafaa kuchajiwa kwa umeme wa jua.

Uwekezaji huo unakadiriwa kugharimu TZS 11bn, na uzalishaji utaanza ndani ya miezi 3 ijayo, ambapo utatoa ajira 2,000.

View attachment 916350
Opportunities ndio hizi vijna tuzichangamkieni.
 
Samahani Ndugu, Baba, Waume na Shemeji kwa sababu hili linawahusu nyote!!

Utafiti umebaini kuwa kinamama wanastahili kusubiri kwa MWAKA MMOJA baada ya kujifungua kabla ya kupata ujauzito mwingine ili kupunguza hatari ya kumpoteza mama na mtoto
.
Muda mfupi kati ya mimba moja hadi nyingine humuweka mama katika hatari ya kuzaa mtoto ambaye hajatimiza wakati wa kuzaliwa,mtoto mdogo au kifo chake.

Eheee kwa hivyo vuteni pumzi jamani USIMHARAKISHIE MAUTI MPENZI WAKO View attachment 916344
Wewe peke ndio ulikuwa haujui,,wenzio mbona tunafahamu
 
Back
Top Bottom