Makapuku Forum

Makapuku Forum

USIKIMBILIE KUWA MZAZI YAJUE HAYA KUMI MUHIMU KWANZA.

1.Maisha yako yatabadilika moja kwa moja! Utajifunza matumizi mazuri ya fedha, ulaji, kuendesha gari kwa hekima, Mahusiano na mpenzi wako yatabadilika (kwa uzuri au ubaya) mtajiona wa tofauti sana. Muda wako wa ziada utapenda ulale kwani kukosa usingizi halitakuwa jambo la ajabu.

2.Utatakiwa upende anachopenda Mtoto.
Sahau kuhusu timu yako uipendayo kwa muda, kipindi chako ukipendacho, utajua machache sana yanayoendelea duniani, na sasa utapenda anachopenda mtoto. Utakuwa mtoto kwa muda, hii ni kawaida sana.
 
3.Nyumbani Kwako kutakuwa kijalala Kidogo
Watoto wanapenda michezo mingi sana! Usitegemee kukuta sebule yako ni safi muda wote kama ulivyozoea, usifikirie kwamba atavijali vitu vyako kama unavyojali wewe.








4. Simu/ Computer yako itakuwa ya mwanao.
Licha ya juhudi zote jua ya kwamba watoto watagusa simu, au computer yako tu! Watapenda kuwa na wewe, kufanya kazi kama wewe, na kutumia vitu vyako. Hakikisha vitu vilivyo kwenye simu, au computer yako vinamfaa, na hakuna ubaya akiona.
 
5.Utaanza Kujiona na kuona Makosa uliyoyafanya ukiwa mdogo, utaijua thamani yako na ya wazazi wako ambao pengine hawatakuwepio.




6.Hutaweza tena Kutumia fedha kwa ajili yako mwenyewe kwani utaona kila fedha unayotumia, ungeweza kutumia na familia nzima. Na utajisikia raha zaidi kumnunulia mwanao kitu zaidi ya kujinunulia wewe mwenyewe.
 
7.Suala la Muda litabadilika, na utalaumiwa zaidi na watu wako wa karibu kwamba hujui kutunza muda. Usitegemee kujiandaa kwa haraka unapotoka kama zamani.


8.Miezi Michache ya mwanzo baada ya kupata mtoto, kitakuwa kipindi kigumu zaidi kuwahi kukutana nacho, ratiba zako za kulala, kuoga, kupika, kusali nk zitabadilika kabisa. Utapitia vipindi vigumu, utakosa fedha ila hakuna namna tena.
 
9.Rafiki wako wa karibu atakuwa Daktari au Muuguzi wa mwanao. Utazijua hospitali nyingi zaidi kuliko bar, na kumbi zako za zamani za kustarehe.


10. Jiandae kwa dharula za aina zote, hakikisha una fedha ya dharula au wakati mwingine itakubidi uhamishie ofisi nyumbani ili uweze kuendelea na shughuli zako za kila siku.
 
WAJUA NINI HUTOKEA BAADA YA KUACHA KUVUTA SIGARA? TAZAMA HATUA HIZI KUMI

Unafikiria kuacha sigara? ….Yees! wazo zuri. Kwanini? Kwa sababu utaanza kuona faida za kuacha kuvuta sigara ndani ya dakika ishirini tu baada ya kuacha! Wajua inachukua muda gani mpaka kiasi cha nicotine kutoka mwilini mwako? Soma haya…

1.Dakika ishirini (20) tu, baada ya kuacha kuvuta sigara mapigo yako ya moyo huanza kurudi katika hali ya kawaida

2. Masaa mawili baada ya kuacha kuvuta sigara, mzunguko wako wa damu hurudi katika hali ya kawaida. Kiwango cha nicotine hushuka mpaka asilimia 6.2



3. Wajua wavuta sigara wana hasira za haraka? Baada tu ya masaa 24 yaani siku moja baada ya kuacha sigara, mvutaji hujisikia mwenye amani na akikaa hivyo kwa wiki moja zaidi hujisikia katika hali bora zaidi.
 
4. baada ya siku mbili tu toka uache kuvuta sigara, neva zilizoanza kufa huanza kurudi katika hali yake na kiwango cha kunusa na uwezo wa ulimi kutambua ladha huongezeka!

5. Siku tatu baadae mwili wako hautajisikia kuwa na nicotine tena kwa asilimia 100% japo bado itakuwepo kwa kiasi Fulani. Na utaanza kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa kama TB au mshtuko wa moyo.

6. Wiki moja tu baada ya kuacha sigara utakuwa na uwezo wa kufanya shughuli yoyote ya kutumia nguvu ambayo mwanzo ulikuwa ukichoka kwa haraka baada tu ya kufanya hivyo.

7. Mwezi mmoja mpaka mitatu baada ya kuacha, mapafu yako huanza kuwa safi na kurudi katika hali yake ya kawaida
 
8. Mwaka mmoja baada ya kuacha sigara, hatari yako kupata magonjwa kama TB na mshtuko wa moja hushuka mpaka asilimia 50% kulinganisha na mvutaji!

9. Miaka mitano baada ya kuacha sigara Utakuwa umepunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kupata kiharusi. Na kupunguza kama si kuondoa kabisa uwezekano wa kupata TB (inategemeana umevuta kwa mda gani)


10. Miaka Kumi na zaidi baada ya kuacha sigara, tapunguza uwezekano wa kupata kansa ya mapafu, na madhara hayataonekana mwilini mwako kwa asilimia karibu mia moja (100%) na Utakuwa na furaha zaidi maishani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom