Uvutaji wa bangi miongoni mwa vijana barubaru unaathiri kwa kiwango kikubwa mno kukua kwa ubongo wao na uwezo wa ubongo wao kumakinika shuleni.
Utafiti uliohusisha vijana 3800 kati ya miaka 13 - 19 nchini Canada, umebaini kuwa bangi inaathiri uwezo wa kusoma na hata kufanya maamuzi katika miaka ya baadaye
Licha ya jitihada zao zilizoonekana kuungwa mkono na rais wa Uganda, Yoweri Museveni, wabunge wa upinzani na wachache kutoka chama tawala wameshindwa katika kura ya kuondoa kodi ya huduma za kuhamisha pesa kwenye mitandao ya simu za mkononi maarufu kama mobile money.
Katika kura ya kuitikia, wabunge 164 walitaka kodi hiyo ibaki lakini 124 walitaka itupiliwe mbali.
Serikali inasisitiza kuwa kodi hiyo ya asilimia 0.5 ni muhimu kwa uchumi wa nchi.
"Tumeifahamisha serikali ya Tanzania kwamba marekebisho ya sheria ya takwimu 2015, iwapo yatatekelezwa, huenda yakaathiri sana kuandaliwa kwa takwimu rasmi na zisizo rasmi, ambazo huwa muhimu sana kwa ustawi wa taifa lolote lile," benki ya dunia .
Kutokana na hilo, benki ya dunia imesema inajadiliana na serikali kuhusu utoaji wa msaada zaidi katika kujenga mifumo ya takwimu endelevu unaofaa kwa wakati huu.
Mtangazaji maarufu wa kipindi cha redio cha Hot 91.9 FM Sasha Martinengo, raia mwenye asili ya kizungu,
amefutwa kazi baada ya kumuita kiongozi wa upinzani wa chama cha Economic Freedom Fighters, Julius Malema tumbili.
Jiji la Dar es Salaam ni miongoni mwa miji ambayo haina miinuko na upo karibu sana na bahari. Unatajwa na wanasayansi kuwa upo katika hatari ya kuzama katika miaka 50 ijayo .
Mji huu wa Dar es salaam unaweza kuathirika kutokana na ongezeko la joto kama mvua nyingi zitanyesha na miundombinu kuendeea kuwa mibaya.
Mombasa imetajwa kupotea baada ya miaka 20, Pemba katika kisiwa cha Panza , maji zaidi ya mita 100 yameingia nchi kavu na tayari Tanzania imeshapoteza visiwa viwili kimoja kipo maeneo ya Tanga Pangani na kingine Rufiji'fungu la nyani. Je tufanye nini kuokoa miji
Tendo la ndoa kwangu ni balaa tupu, ni Mateso!!' Isley Lynn,Mwanamke aliyejitokeza hadharani na kusema Mwili wake umekataa kata kata tendo la ndoa.
Madaktari wamemwambia kuwa anaugua VAGINISMUS :
Hali ya mwili kuwa na hofu ya baadhi au aina yoyote ya kitu kupenya kwenye uke.
Misuli ya uke huwa ngumu na wakati huo mwanamke hana udhibiti wa mwili wake.
Je unafahamu hali hii ?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.