Makapuku Forum

Makapuku Forum

MAAJABU KUMI (10) AMBAYO HUJUI KAMA MWILI WAKO HAUWEZI KUYAFANYA
10. Huwezi Kuandika Namba Sita Ukiwa Unazungusha Mguu Wako Wa Kulia Mwelekeo Wa Saa (Clockwise).Kaa Kwenye Kiti, Nyanyua Mguu Wako Wa Kulia Juu, Kisha Anza Kuuzungusha Kwa Duara Kwa Kufuata Muelekeo Wa Saa (Yaani Kutoka Kushoto Kwenda Kulia) Endelea Kufanya Hivyo Huku Unaandika Nambasita (6). Umegundua Nini? Mguu Wako Umegeuka Na Kuanza Kuzunguka Muelekeo Wa Kushoto!!

9. Huwezi Kurusha Mate Ukiwa Umeachama Mdomo!


8. Huwezi Kunyanyua Kidole Chako Cha Pete Katika Hali Ifuatayo;


Kunja kidole chako cha katikati juu ya meza ukiviacha vidole vyako vinne vikiwa vimenyooka kama inavyoonekana kwenya picha kushoto. Jaribu kunyanyua dole gumba, kisha nyanyua kidole kinachofuata, na kidole kidogo cha mwisho... rahisi sio?? SASA nyanyua kidole cha pete... kimegoma!
 
7. Huwezi Kuchezesha Pua Yako Kulia Na Kushoto

(Sijasema ujaribu kufanya zoezi hili)



6. Huwezi Kuokota Kitu Chini Ukiwa Umeegamia Ukuta Na Visigino Vyako Vimegusa Ukuta Huo
fanya zoezi lifuatalo; Simama ukiwa umenyooka huku sehemu ya nyuma ya miguu yako (visigino) vikiwa vimegusa ukuta. jaribu kuokota kitu mbele ya miguu yako!


5. Huwezi Kutikisa Sikio Lako
ukijaribu utajikuta kichwa chako kinainama muelekeo wa sikio ulilojaribu kutikisa!


4. Huwezi Kupiga Chafya Bila Kufunga Macho!


3. Huwezi Kujitekenya
 
SABABU KUMI KWANINI UNATAKIWA KUANZA KULA TENDE

1.Huongeza nguvu kutokana na kuwa na sukari ya asili, unaweza kuchanganya na maziwa na kupata mchanganyiko bora!

2.Huzuia meno kuoza, na ni tiba nzuri kwa wagonjwa wa anemia kutokana na kuwa na madini mengi ya chuma.

3.Hupunguza uwezekano wa kupata Kiharusi (stroke) kwani hazina cholesterol kabisa! Pia zina vitamini na madini kwa wingi.


4. Huongeza uwezo wa Kujamiiana kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha nguvu

5.Hupunguza madhara ya pombe mwilini na kurudisha afya ya mtu.
 
6.Zina kiasi kikubwa cha kamba kamba ambazo hufanya mtu apate choo kirahisi na laini

7. Licha ya kuwa tamu, tende haziongezi kiwango cha sukari mwilini, hivyo zinaweza kutumika kama mbadala wa sukari

8. Huimarisha Mifupa na kuondoa maumivu ya mara kwa mara ya mifupa kutokana na kuwa na madini ya chuma, na potassium kwa wingi.

9. Tende ina msaada mkubwa kwa mama mjamzito, humuongeza nguvu, na hazina madhara kiafya kwa mtoto. Pia husaidia kupata uzazi salama


10.Ulaji wa tende kwa wingi husaidia kuongeza mwili kwa wale waliokonda kupita kiasi. Hivyo hushauriwi kula tende kupita kiasi kama huhitaji kuongeza mwili.
 
MADHARA 10 YA KUTUMIA SHISHA! (VIJANA WENGI HAWAJAYAJUI)

1.Kansa
Licha ya kupita ndani ya maji, moshi wa shisha huwa na kiwango kikubwa cha carbon monoxide na nicotine ambazo humfanya mtumiaji awe kwenye hatari kubwa ya Kupata Tatizo la kansa ya koo, ama mapafu.

2.Matatizo ya Moyo
Moshi na tumbaku husababisha mishipa ya damu ya artery Kuziba, Matokeo yakemoyo hushindwa kufanya kazi kwa ufanisi wake.
3.Huharibu Fizi (periodontal disease)
Hii hutokana na kuongezeka kwa kiasi cha sumu ya nicotine kwenye damu na fizi matokeo yake ni kuharibika kwa fizi na kupata matatizo ya meno.

4. Fangasi na Kifua kikuu (TB)
Kutokana na kutosafishwa vizuri kwa bomba za kuvutia shisha (hasa kutokana na wengi kujali kipato kuliko afya za watu) Mtumiaji hujiweka kwenye hatari kubwa ya Kupata magonjwa ya kuambukizwa kama fangasi, au hata vidonda vya tumbo kwa kuvuta kimelea cha helicobacteria

5.Kuzaa Njiti (mtoto mwenye uzito mdogo)
Hii ni kwa wanawake wanaotumia shisha wakiwa wajawazito. Pia mtoto huyo ni rahisi kuwa na magonjwa yanayohusiana na upumuaji
 
6. “Nicotine Addiction”
Hii ni hali ya kuwa mtumwa wa Sumu ya Nicotine. Mtumiaji wa shisha huvuta kiwango sawa cha nicotine kama mvutaji wa sigara hii husababisha sumu hii hatari kuingia kwenye damu yake, matokeo yake hataweza kuishi bila kutumia shisha au sigara.

7.Kupoteza Uwezo za Kujamiiana.
Utafiti unaonesha kuwa, wanawake wanaotumia shisha hupoteza hamu ya kujamiiana kwa kiasi kikubwa. Hali ni mbaya zaidi kwa wanaume kwani huchangia kwa kiasi kikubwa upungufu wa nguvu za kiume.

8.Kuchakaa kwa ngozi.
Kama ilivyo kwa watumiaji wa sigara, matumizi ya shisha huchangia kwa kiasi kikubwa katika uharibifu wa ngozi. Mtumiaji wa muda mrefu wa shisha huzeeka haraka zaidi ya asiyetumia.

9.Asthma na Allergy Zingine
Uvutaji wa shisha huharibu utando laini uliopo kwenye njia za pua na koo, uharibifu huu unaweza kusababisha matatizo ya allergy, na asthma.


10.Kwa kuwa Haina Ladha kama ya sigara, watu wengi (hasa vijana) huona shisha ni mbadala mzuri wa sigara, bangi, na madawa mengine ya kulevya wakihisi haina madhara kumbe wanajiangamiza wenyewe!
 
IMG_20181003_132120.jpg
dncbvm1wsaeqmuc-jpg.877188.jpg
38300996_2022461497766353_3594765276018638848_n-jpg.838379.jpg
IMG_20181001_192423.jpg
IMG_20181003_131237.jpg
IMG_20181003_132146.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom