Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 348,117
- 1,249,282
Mbinu Itakayokusaidia kutambua na kubadili mawazo mabaya yanayokuja kwako mara kwa mara .
Tamaa mbaya, mawazo mabaya, mitazamo mibaya inayotokea kwenye maisha yako yanaweza kutoweka kwa urahisi kuliko unavyofikiria . Unapokuwa unafikiria vibaya kila mara unaongeza risk ya uharibifu wa akili yako, unasababisha matatizo ya afya yako, Mahusiano yako, kipato chako hakiwezi kukaa vizuri.
Lakini habari ya mijini ni hii , kila mtu anaweza kujifunza jinsi ya kuondokana na Negative thinking. Mimi nimejifunza kitu kikubwa hapa, Kwamba mtu anapoamua kujifunza kubadilisha mawazo mabaya aliyonayo juu ya kitu chochote , sio tu atajisikia vizuri bali tabia inabadilika pia
Kutengeneza tabia nzuri ni ngumu , lakini kuishi tabia nzuri ni rahisi. Na kutengeneza tabia mbaya ni rahisi lakini kuishi tabia mbaya ni ngumu kupita kiasi. Wazazi wengi wanalea watoto kimayai , wanasahau kuwa kiburi cha mtoto kinaanzia akiwa na umri wa miaka 3. Hapo usimnyime mtoto fimbo kila anapokosea. Ni vizuri kuanza kujenga misuli ya akili inayofikiri mazuri mapema.
Jinsi Gani Unaweza Kubadilisha Mawazo Mabaya.
Mawazo haya husimamia hapa; Kujilaumu, kutazama Habari mbaya, Huzuni ya kuotea, mawazo mabaya juu ya wengine, kazi , biashara, mahusiano. Usipokuwa makini unaweza kufikiri ni mawazo mazuri lakini sio. Tambua ni jinsi gani mawazo mabaya yanavyokuja kwako.
1.Kujilaumu. Mahali ambapo unatakiwa kuchukua jukumu lako na kujiona kuwa huwezi kutimiza lengo kutokana na tatizo la kiakili ndani yako ni kutokujua kutumia muda wako vizuri. Kila kitu utakuwa unaona kama unaharibu. Jaribu kutazama muda ulionao na ule ambao umetumia unapokuwa unajilaumu utagundua kuwa kuna tatizo ndani yako mwenyewe.
2.Kutazama Habari Mbaya; Kama kuna mambo tisa mazuri yametokea kwa siku, Utaona jinsi inavyokuwa rahisi kufuatilia lile moja baya badala ya kufuatilia mengi mazuri. Lakini tambua kuwa kuzamia kwenye mawazo hayo mabaya yatakukwamisha kwenye giza kubwa na ukiwa na utupu mkubwa. Ni muhimu kurudi kwenye mazuri kila mara unapoona dalili hio mbaya. Rudi kwenye Nuru.
3.Huzuni Ya Kuotea. Hata kama hujui ni kitu gani kitatokea kesho, Ni vizuri kjijengea tabia ya kuwaza mema kila mara. Muombe Mungu kila siku akujaze Tunda la roho ndani mwako. Neno la Mungu Linasema kuwa Katika Mathayo 7:7 Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtaona, Bisheni nanyi mtafunguliwa. Kama unaona upungufu wa kitu ndani yako muombe Mungu. Yakobo 1:5. mtu wa kwenu akipungukiwa na …. Na aombe Dua kwa Mungu awapaye wote kwa ukarimu.
Huenda unakuwa na wasiwasi wa kutokupandishwa cheo, kutokupata wateja, kuharibika kwa mahusiano, kutokupona ugonjwa ulionao, Huzuni ya kuotea isikuharibie utabiri wako mzuri kwa ajili ya kesho yako.
4.Kujishusha Hadhi; Kujisemea maneno mabaya mwenyewe, mfano umeenda kwenye usaili na kujiona kama umefanya vibaya kabla ya matokeo au kujishawishi mwenyewe kuwa huwezi kupata kazi . Kwa jinsi unavyozidi kuwaza mabaya ndivyo unavyojishusha chini zaidi. Na jinsi unavyojisikia vibaya unashindwa kuwaza mazuri.
Kitu Gani Cha Kufanya Mara Unapoona Hali Hio Inakupata.
Mara tu unapotambua hali hio inakutokea . Haraka sana Angalia muda wako unatumiaje, Isije ikawa akili yako imekuwa karakana la Adui . Akili ikiwa bize huwezi kuwaza mabaya. Jiulize mwenyewe kama Unawafanyia watu kile ambacho unapenda wewe ufanyiwe? Ukiwa unajiwazia mabaya mwenyewe, utafungulia mlango wa watu kukuwazia mabaya pia. Jiulize kama ungeweza kusema nini kwa rafiki ambaye ana tatizo kama hilo?
Fanya mchakato mpya wa kusave pesa za kutosha kwa ajili ya baadae.
Thubutu leo kujisemea maneno mazuri , na ukumbuke kuwa kujenga tabia nzuri sio siku moja, kwa hio usikate tamaa, dhamiria kubadilika. Inawezekana.
Tambua kuwa kuwekeza inahitaji juhudi kubwa. Kubadilika kimwili inategemea sana mabadiliko ya kiroho . Ubongo wako unakusubiri wewe kufanya maamuzi ya kitu gani unataka katika maisha yako.
Tamaa mbaya, mawazo mabaya, mitazamo mibaya inayotokea kwenye maisha yako yanaweza kutoweka kwa urahisi kuliko unavyofikiria . Unapokuwa unafikiria vibaya kila mara unaongeza risk ya uharibifu wa akili yako, unasababisha matatizo ya afya yako, Mahusiano yako, kipato chako hakiwezi kukaa vizuri.
Lakini habari ya mijini ni hii , kila mtu anaweza kujifunza jinsi ya kuondokana na Negative thinking. Mimi nimejifunza kitu kikubwa hapa, Kwamba mtu anapoamua kujifunza kubadilisha mawazo mabaya aliyonayo juu ya kitu chochote , sio tu atajisikia vizuri bali tabia inabadilika pia
Kutengeneza tabia nzuri ni ngumu , lakini kuishi tabia nzuri ni rahisi. Na kutengeneza tabia mbaya ni rahisi lakini kuishi tabia mbaya ni ngumu kupita kiasi. Wazazi wengi wanalea watoto kimayai , wanasahau kuwa kiburi cha mtoto kinaanzia akiwa na umri wa miaka 3. Hapo usimnyime mtoto fimbo kila anapokosea. Ni vizuri kuanza kujenga misuli ya akili inayofikiri mazuri mapema.
Jinsi Gani Unaweza Kubadilisha Mawazo Mabaya.
Mawazo haya husimamia hapa; Kujilaumu, kutazama Habari mbaya, Huzuni ya kuotea, mawazo mabaya juu ya wengine, kazi , biashara, mahusiano. Usipokuwa makini unaweza kufikiri ni mawazo mazuri lakini sio. Tambua ni jinsi gani mawazo mabaya yanavyokuja kwako.
1.Kujilaumu. Mahali ambapo unatakiwa kuchukua jukumu lako na kujiona kuwa huwezi kutimiza lengo kutokana na tatizo la kiakili ndani yako ni kutokujua kutumia muda wako vizuri. Kila kitu utakuwa unaona kama unaharibu. Jaribu kutazama muda ulionao na ule ambao umetumia unapokuwa unajilaumu utagundua kuwa kuna tatizo ndani yako mwenyewe.
2.Kutazama Habari Mbaya; Kama kuna mambo tisa mazuri yametokea kwa siku, Utaona jinsi inavyokuwa rahisi kufuatilia lile moja baya badala ya kufuatilia mengi mazuri. Lakini tambua kuwa kuzamia kwenye mawazo hayo mabaya yatakukwamisha kwenye giza kubwa na ukiwa na utupu mkubwa. Ni muhimu kurudi kwenye mazuri kila mara unapoona dalili hio mbaya. Rudi kwenye Nuru.
3.Huzuni Ya Kuotea. Hata kama hujui ni kitu gani kitatokea kesho, Ni vizuri kjijengea tabia ya kuwaza mema kila mara. Muombe Mungu kila siku akujaze Tunda la roho ndani mwako. Neno la Mungu Linasema kuwa Katika Mathayo 7:7 Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtaona, Bisheni nanyi mtafunguliwa. Kama unaona upungufu wa kitu ndani yako muombe Mungu. Yakobo 1:5. mtu wa kwenu akipungukiwa na …. Na aombe Dua kwa Mungu awapaye wote kwa ukarimu.
Huenda unakuwa na wasiwasi wa kutokupandishwa cheo, kutokupata wateja, kuharibika kwa mahusiano, kutokupona ugonjwa ulionao, Huzuni ya kuotea isikuharibie utabiri wako mzuri kwa ajili ya kesho yako.
4.Kujishusha Hadhi; Kujisemea maneno mabaya mwenyewe, mfano umeenda kwenye usaili na kujiona kama umefanya vibaya kabla ya matokeo au kujishawishi mwenyewe kuwa huwezi kupata kazi . Kwa jinsi unavyozidi kuwaza mabaya ndivyo unavyojishusha chini zaidi. Na jinsi unavyojisikia vibaya unashindwa kuwaza mazuri.
Kitu Gani Cha Kufanya Mara Unapoona Hali Hio Inakupata.
Mara tu unapotambua hali hio inakutokea . Haraka sana Angalia muda wako unatumiaje, Isije ikawa akili yako imekuwa karakana la Adui . Akili ikiwa bize huwezi kuwaza mabaya. Jiulize mwenyewe kama Unawafanyia watu kile ambacho unapenda wewe ufanyiwe? Ukiwa unajiwazia mabaya mwenyewe, utafungulia mlango wa watu kukuwazia mabaya pia. Jiulize kama ungeweza kusema nini kwa rafiki ambaye ana tatizo kama hilo?
Fanya mchakato mpya wa kusave pesa za kutosha kwa ajili ya baadae.
Thubutu leo kujisemea maneno mazuri , na ukumbuke kuwa kujenga tabia nzuri sio siku moja, kwa hio usikate tamaa, dhamiria kubadilika. Inawezekana.
Tambua kuwa kuwekeza inahitaji juhudi kubwa. Kubadilika kimwili inategemea sana mabadiliko ya kiroho . Ubongo wako unakusubiri wewe kufanya maamuzi ya kitu gani unataka katika maisha yako.
abee dada
TUOMBE:Baba yetu na Mungu wetu Tunakushukuru sana kwa yote unayotutendea,Asante kutuamsha salama leo tarehe 17 Jumatatu Septemba 2018 Tunaomba endelea kutusamehe, kutupigania ..ponya wagonjwa ,ponya mioyo iliyopondeka ..angalia wajane,wagane ,yatima na waliopoteza tumaini tusaidie tuweze kusema ndiyo kwa upendo wako mkuu na kukutumainia .
