Makapuku Forum

Makapuku Forum

ACHA KUJIANGAMIZA! KAMA UNAFANYA HAYA UNAJIUA KIMAISHA.

1. Kujiweka wa mwisho na Kujinyima muda wa kufurahi /kustarehe
Maisha yako yamejengwa kwa vipande vidogo vidogo ambavyo kila kimoja kina nafasi yake, na kikikosekana, basi vingine havitakaa kwenye nafasi zake na kuharibu maisha yote.

Wengi tumekuwa tunawapa nafasi wengine kwanza na kuamua kujiweka sisi wa mwisho. Matokeo yake, unajinyima muda wa kupumzika, kula, kustarehe nk! Matokeo yake huwi na furaha na maisha yako!

2.Kukubali kuendeshwa na matukio mabaya yaliyopita
Kuhisi kwa kuwa kuna kitu Fulani kibaya kilikutokea kwenye maisha yako basi
maishahayatawezekana tena. Pengine ulifiwa, kufukuzwa kazi, shule, kuibiwa au kufilisika.

3.Kukubali kuzungukwa na watu wasiokufaa
Ni rahisi, Siku zote watu waliokubali kushindwa, huwa na sababu za kukupa kwa nini wameshindwa kimaisha, na ukikaa karibu nao watakupa sababu hizi na kukufanya uamini kwamba huu ndio ukweli, na hutakuwa tayari kupiga hatua zaidi.

4.Kukimbia matatizo na kuogopa kushindwa
Je wajua? Ukikimbia matatizo yako, siku zote yatakimbia pamoja nawe. Usikimbie tatizo, likabili na kuamka haraka kila tunapoanguka. Na epuka Kuhisi kuna mtu mwingine anahusika na furaha yako.

5. Kuharibu Maisha ya Mwingine ili Ufanikiwe
Ukiharibu maisha ya mwingine, unaharibu ya kwako! Unaweza kuita Karma, Gundu, au majina mengine, lakini jua ya kwamba hii hutokea kweli. Pia ni ngumu kukaa na hayo mafanikio Maana hutakuwa na plani ya pili ya mafanikio zaidi ya kudhurumu, kuiba, kuua nk!

6. Kuamini Wewe ni Mifupa na nyama tu!
Hili ni kosa kubwa sana maishani, wengi huamini binadamu n mifupa na nyama tu, hivyo hakuna hata ya kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa tu “eti” Mwisho wa siku tutakufa na kuzikwa! Je, Unawaachia nini wanao na kizazi chako? Je kwa nini hasa Mungu alitupa utashi tofauti na Mbuzi na wanyama wengine?

Kumbuka, Tungeamua kuamini kuwa sisi ni Nyama na mifupa tu, kusingekuwa na Magari, Simu, Majengo ya kisasa, na Hata hii dini tuliyonayo tusingeipata.
“do your part, make world a better place”

7.Kulaumu Vitu vinavyotokea na kutokuwa tayari kutafuta suluhisho Pengine kwa kutotaka kufanya maamuzi magumu au kutojua Majukumu yako ni yapi (badilika)

8. Kuamini kila kinachosemwa na “Wataalamu”
Siku hizi kila sekta kuna watu wanaojiita wataalamu (mimi mmoja wapo!) Lakini nasikitika kukuambia kuwa, wengi wa wataalamu hawa, hawako sahihi kwani siku hizi watu wanapata kipato kutokana na kuyaelewa matatizo ya watu na si kujua suluhisho.
Usimuamini mtu eti tu kwa kuwa analielezea kwa uzuri na analielewa tatizo lako bali muamini anayeweza kutoa suluhisho linalokuwa msaada kwa tatizo lako

9. Kuhisi huwezi kwa kuwa kuna mtu anakuambia hivyo
Kuna watu maishani wapo sii tu kwa kukukwamisha wewe, bali pia kumkwamisha kila anayewazunguka. Ukiona hakubaliki kwa jinsi ulivyo, basi jua huko mahali sahihi. Usikubali kuishi kama mtu mwingine kwa kuwa tu unataka kukubalika maishani.

10. Kuona huhitaji chochote cha kusoma
Maisha yanachekesha! Kitu kinaweza kuwepo leo, na kesho kisikuwepo. Kama kuna kitu unataka kufanya, fanya sasahivi. Kama ni wazo la muda mrefu, basi anza leo kutekeleza kidogo kidogo. Kila muda una changamoto zake. Hata tajiri mkubwa duniani Bill gates anachangamoto zake kulingana na nafasi aliyonayo.
Asanteeee
 
Kumbe aliwahi kuwa bingwa wa ndondi
UNAMJUA VIZURI IDI AMINI WA UGANDA? SOMA MAMBO HAYA 10 UBAKI MDOMO WAZI!

1.Aliwahi kuwa bingwa wa ndondi wa uzito wa juu nchini Uganda mwaka 1960-1961

2.alijichagua kuwa Raisi wa Uganda kwa mapinduzi ya kijeshi, na waganda wengi walimchukulia kuwa ni shujaa kwa kumuondoa raisi walieona “anasuasua” Milton Obote mwaka 1971.

3.Aliua watu zaidi ya laki tatu (300,000) kwa kipindi cha miaka 8 aliyokuwepo madarakani kabla ya Kung’olewa na Majeshi ya kitanzania mwaka 1979 baada ya kutaka kuteka sehemu ya Tanzania.

4.Aliwatimua raia wote wenye asili ya Kihindi nchini kwake na kutaifisha mali zao zote.

5.alijipa vyeo kibao na kujiita Field Marshall Al Hadj Doctor Idi Amin Dada!

6.Inasemekana alimtumia malkia wa uingereza Elizibeth II barua za kimapenzi akimuomba amuoe ili aweze kujiita mfalme kwani alikuwa ameshajipa vyeo vyote kasoro “King” Yaani mfalme.

7.Ana watoto zaidi ya 40 huku akiwa ameoa wake 6. Mmoja wa wake zake alikutwa ameuawa kinyama baada ya kupata ujauzito na mtu mwingine.

8.Vyombo kadhaa vya Habari vimekuwa vikimuhusisha na ulaji wa nyama za watu hasa maadui zake aliowaua.

9.Licha ya Ukatili dhidi ya binadamu, Idi amin hajawahi kufikishwa mahakaman mpaka anakufa mwaka 2003 na kuzikwa nchini Saudi Arabia alikokuwa akiishi uhamishoni.


10. Hajawahi kuandika popote historia ya maisha yake wala kuruhusu mtu yeyote Yule kuandika kuhusu maisha yake!
 
KWA MWENYE AKILI TIMAMU LAZIMA UJIULIZE MASWALI HAYA KUMI KABLA SIKU HAIJAISHA

1.Je, leo nina nafuu yoyote kuliko jana? Kama ipo ni ipi?

2. Ni Kitu gani kipya nimejifunza leo?kama hakuna basi soma hata kitabu ukurasa mmoja.

3. Kuna maamuzi yapi mapya au chaguzi zipi nimefanya kuboresha maisha yangu?

4.Kuna chochote nimefanya kwa ajili ya mtu mwingine au dunia kwa ujumla. Kumbuka sio kila zuri unalofanya lazima likufaidishe wewe au ndugu yako moja kwa moja, bali mazuri yaw engine ndiyo yatakayokunufaisha wewe na jamii yako.

5. Je, nimemuudhi nani leo? Au pengine
nimekwaruzana na nani? Na je nini hatma yake?

6. Je, nini umekifanya kwa ajili ya kesho?

7.Umetimiza kiasi gani mipango uliyojiwekea hapo kabla?

8. Nitafanya nini Kesho ili Kurekebisha nilipokosea leo?

9. Je , nimeonesha upendo kiasi gani kwa familia yangu kwa ujumla? mzazi, mke, mume, watoto au hata mpenzi wako.

10. Ni lipi limekuudhi zaidi na ni lipi limekufurahisha pia?
 
ACHA KUJIANGAMIZA! KAMA UNAFANYA HAYA UNAJIUA KIMAISHA.

1. Kujiweka wa mwisho na Kujinyima muda wa kufurahi /kustarehe
Maisha yako yamejengwa kwa vipande vidogo vidogo ambavyo kila kimoja kina nafasi yake, na kikikosekana, basi vingine havitakaa kwenye nafasi zake na kuharibu maisha yote.

Wengi tumekuwa tunawapa nafasi wengine kwanza na kuamua kujiweka sisi wa mwisho. Matokeo yake, unajinyima muda wa kupumzika, kula, kustarehe nk! Matokeo yake huwi na furaha na maisha yako!

2.Kukubali kuendeshwa na matukio mabaya yaliyopita
Kuhisi kwa kuwa kuna kitu Fulani kibaya kilikutokea kwenye maisha yako basi
maishahayatawezekana tena. Pengine ulifiwa, kufukuzwa kazi, shule, kuibiwa au kufilisika.

3.Kukubali kuzungukwa na watu wasiokufaa
Ni rahisi, Siku zote watu waliokubali kushindwa, huwa na sababu za kukupa kwa nini wameshindwa kimaisha, na ukikaa karibu nao watakupa sababu hizi na kukufanya uamini kwamba huu ndio ukweli, na hutakuwa tayari kupiga hatua zaidi.

4.Kukimbia matatizo na kuogopa kushindwa
Je wajua? Ukikimbia matatizo yako, siku zote yatakimbia pamoja nawe. Usikimbie tatizo, likabili na kuamka haraka kila tunapoanguka. Na epuka Kuhisi kuna mtu mwingine anahusika na furaha yako.

5. Kuharibu Maisha ya Mwingine ili Ufanikiwe
Ukiharibu maisha ya mwingine, unaharibu ya kwako! Unaweza kuita Karma, Gundu, au majina mengine, lakini jua ya kwamba hii hutokea kweli. Pia ni ngumu kukaa na hayo mafanikio Maana hutakuwa na plani ya pili ya mafanikio zaidi ya kudhurumu, kuiba, kuua nk!

6. Kuamini Wewe ni Mifupa na nyama tu!
Hili ni kosa kubwa sana maishani, wengi huamini binadamu n mifupa na nyama tu, hivyo hakuna hata ya kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa tu “eti” Mwisho wa siku tutakufa na kuzikwa! Je, Unawaachia nini wanao na kizazi chako? Je kwa nini hasa Mungu alitupa utashi tofauti na Mbuzi na wanyama wengine?

Kumbuka, Tungeamua kuamini kuwa sisi ni Nyama na mifupa tu, kusingekuwa na Magari, Simu, Majengo ya kisasa, na Hata hii dini tuliyonayo tusingeipata.
“do your part, make world a better place”

7.Kulaumu Vitu vinavyotokea na kutokuwa tayari kutafuta suluhisho Pengine kwa kutotaka kufanya maamuzi magumu au kutojua Majukumu yako ni yapi (badilika)

8. Kuamini kila kinachosemwa na “Wataalamu”
Siku hizi kila sekta kuna watu wanaojiita wataalamu (mimi mmoja wapo!) Lakini nasikitika kukuambia kuwa, wengi wa wataalamu hawa, hawako sahihi kwani siku hizi watu wanapata kipato kutokana na kuyaelewa matatizo ya watu na si kujua suluhisho.
Usimuamini mtu eti tu kwa kuwa analielezea kwa uzuri na analielewa tatizo lako bali muamini anayeweza kutoa suluhisho linalokuwa msaada kwa tatizo lako

9. Kuhisi huwezi kwa kuwa kuna mtu anakuambia hivyo
Kuna watu maishani wapo sii tu kwa kukukwamisha wewe, bali pia kumkwamisha kila anayewazunguka. Ukiona hakubaliki kwa jinsi ulivyo, basi jua huko mahali sahihi. Usikubali kuishi kama mtu mwingine kwa kuwa tu unataka kukubalika maishani.

10. Kuona huhitaji chochote cha kusoma
Maisha yanachekesha! Kitu kinaweza kuwepo leo, na kesho kisikuwepo. Kama kuna kitu unataka kufanya, fanya sasahivi. Kama ni wazo la muda mrefu, basi anza leo kutekeleza kidogo kidogo. Kila muda una changamoto zake. Hata tajiri mkubwa duniani Bill gates anachangamoto zake kulingana na nafasi aliyonayo.
asante Numbi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom