Kwa mwendo konokono hutembea taratibu sana, na kutokana na mwili wake kuwa mlaini ili asiumie anapotembea hutanguliza ute ute chini, pindi anapouvuta mwili wake asipate kuumia, na ute ute huo hufanya kutengeneza alama ya njia aliyopita, konokono huwa na uzito wa gram zipatazo 5 na kuendelea, na urefu wao huwa inchi zipatazo 7 na kuendelea, ukiondoa hayo muujiza wa konokono ni kwamba ana maisha marefu huishi zaidi ya miaka 10.
Kimsingi konokono wapo wa aina tatu wapo wa nchi kavu, maji baridi na maji ya chumvi, maisha yao huathiriwa sana na viumbe wafuatao kwakuwa huwatumia kama chakula, viumbe hao ni pamoja na ndege,panya, Kobe,binadamu, mijusi nk.
Konokono mwendo wake ni taratibu sana mpaka sasa hakuna ushahidi wa kutosha kuonesha kwamba kuna konokono aliyewahi kuvuka salama barabara, mwendo wao ni wa kusua sua sana, utafiti unaonesha ya kwamba ili aweze kumaliza umbali wa kilometer moja anahitaji wiki moja na siku mbili.
SIFA ZA KONOKONO.
1. wana uwezo mzuri wa kutizama usiku kuliko mchana.
2. Ni ngumu sana kujua jike ni yupi na dume yupi hiyo yote ni kwa sababu jinsia zote kila konokono anazo.
3. Konokono anapotaga baada ya kutotoa, magamba ya mayai hula na ambayo hayatatotolewa huliwa na watoto wake.
4. Konokono hawasikii kabisa, hivyo hujiongoza kwa kunusa .
5. Ukimmwagia chumvi konokono anayeyuka kabisa na kupotea, hivyo kama wamevamia kwako mwaga maji ya chumvi tuu.
6.konokono huweza kutembea gamba lake akiweka juu au likiwa chini na akatembea pasina ya tatizo lolote.
7. Kiumbe huyu pengine ndiye mwenye meno mengi kuliko wengine, watafiti hudai ana meno yanayozidi elfu moja.
8. Konokono ni kiumbe asiyekula nyama kabisa, hivyo akikupanda mwilini kwa bahati mbaya mtoe kistaarabu hawezi kukuuma.
9. Konokono hupendelea mazingira machafu na yenye giza yenye unyevu nyevu.
10. Konokono huweza kuufupisha mwili wake ajifichapo katika gamba lake, na baada kilichosabisha ajihami kutoweka hutoa tena mwili wake.