Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20180824-002631.jpeg
 
Mwezi Novemba mwaka 2009, Jamaa Aliyefahamika Kwa Jina La John Jones Alikua Pamoja Na Wenzake Wakitalii Katika Pango Moja Huko Uttah Ambalo Huwa Linatembelewa Na Watalii Mara Kwa Mara.

Wakati Wakiwa Wanafanya Utalii Wao, Kaka Yake Ambae Nae Alikua Katika Msafara Huo Anasema Mdogo Wake Aliamua Kwenda Njia Nyingine Ili Aendelee Kutalii Zaidi.

Kilichotokea Ni Jamaa Alijikuta Akibanwa Katika Moja Ya Njia Alipokua Akijaribu Kupita Juu Chini, Yani Kichwa Chini Miguu Juu.

Licha Ya Juhudi Nzito Zilizofanywa Kutaka Kumuokoa Lakini Ilishindikana Kwa Sababu Ya Namna Njia Ilivyokua Kiasi Kwamba Kama Ungemvuta Basi Mngetoka Na Kiungo Kimoja Moja.

Walichofanya Ni Kumpa Chakula Na Pia Kumchoma Baadhi Ya Dawa Ili Kumtuliza Kidogo Kidogo, Na Baada Ya Masaa 28 Tangu Kugundulika Kubanwa Eneo Hilo John Alifariki Dunia.

Familia Yake Pamoja Na Wamiliki Wa Eneo Hilo Walikubaliana Kufanya Maziko Eneo Hilo Hilo Na Pia Kuziba Ili Kukinga Watu Wengine Kuja Kupata Madhara.

John Aliacha Mke, Pamoja Na Mtoto Wake Mdogo Ambapo Pia Mke Wake Alikua Ni Mjamzito.

Kuna Filamu Pia Inayohumuhusu Inaitwa "The
Screenshot_20180820-180127.jpeg
Screenshot_20180820-180139.jpeg
Screenshot_20180820-180158.jpeg
 
Umewahi Tazama Filamu za "The Amytville Horrors" Zipo Nyingi, ya Mwisho Bila Shaka Imetoka Mwaka 2017.
-
Filamu Hiyo Ni Stori Ya Ukweli, Sema Zingine Zimeongezewa Chumvi Kimtindo Lakini Filamu Ya mwaka 1979 Ndiyo Inaakisi Uhalisia.
-
Stori Ya Ukweli...Mwaka 1974, Ronald "Butch" Defeo Jr Katika Makazi Yake Huko Amytville Aliwaua
watu Sita Kutoka Katika Familia Yake.
-
Katika Maelezo Yake, Alikiri Kufanya Hivyo Lakini Anasema Kuwa Katika Nyumba Hiyo Ambayo Alikua Akiishi, Kuna Sauti Zilikua Zikimwamwambia Awaue Wenzake Kila Mara.
-
Mwaka Mmoja Badae, Familia Ya Bwana Lutz, ilihamia Katika Nyumba hiyo.
-
Lakini ndani Ya Siku 28 Tu Walikimbia Nyumba Hiyo, wakisema Kuwa Walikua Wakikumbana Na Mambo Ya Ajabu Na visanga Vizito.
-
Kufuatia Hali Hiyo, Polisi Waliamua Kuchunguza Vizuri Zaidi Kuhusu Nyumba Hiyo, Ambapo Walitegesha Camera maalumu Kwa Umbali kidogo Na Nyumba Hiyo...Camera Hizo Ni Zile Zenye Uwezo Wa Kupiga Picha Za Infrared..Yani Picha Zenye Kupenya Na Kuchukua Hata katika Sehemu Ya giza Na Katika Vitu Visivyoonekana Kirahisi.
-
Mojawapo Ya picha Waliyopata Ndo Hiyo Hapo Kama Unavyoona.
-
Inaamika kuwa Huyo Dogo Ndiye John Matthew, Ambae Alikua Mdogo Mdogo Bado Wakati Anauwawa Mwaka 74 Na Bwana Ronald

Screenshot_20180824-174809.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom