Nimezipokea shikamoo zenu Shunie na ABJ kwa marhaba yenye mashamushamu na kama mnekuwa karibu kila mtu ningemwambia anywe kinywaji anachopenda kwa gharama zake
...unaweza kusema chochote unachotaka, nchi huru hii na ndiyo maana mimi kwa kutumia uhuru wangu usio na mipaka wala mbwa Hobby ninakusalimia wewe Kapuku ambaye unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu znuri kuwepo. Inawezekana narudiarudia sana haya maneno, vumilia tu na una uhuru wa kuchukia kama yanakuudhi na ikiwa ni tofauti basi furahia maana wewe ni mtu bora sana hapa.
Leo ni Jumatano, kama ulikuwa hujui ninakujulisha sasa na kukutakia wakati mzuri ulionao wakati unaburudika na huu muziki ninaoupenda zaidi.
Hivi humu Makapuku hamna Ma Dr wale wa Binadamu? Nataka TU kujua kama Mawazo yanachangia kupata vidonda vya tumbo! Vipi kuhusu ndoto? Ndoto zetu hazitusababishii ulcers? Mimi Ktk hobby zangu, ndoto ni No. 1