Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Sijui Chochote

Kichwa cha habari hapo kisikufanye ukadhani ni kweli sijui chochote, nilichomaanisha hapo ni mimi kukosa kumbukumbu kama nimekusalimia wewe unayelifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Ujue nini, bila wewe MF ni kama majukwaa mengine tu lakini kwa kuwa wewe upo basi jukwaa hili ni sehemu nzuri sana kuwepo na tupenane asante kwa hili.

Nimefurahi kumuona anko wangu ambaye dalili zote zinaonesha kaachika kule alikowenda maana si kwa upole huu anaouonesha yaani amekuwa mtaratibu utasema mfanyakazi wa chumba cha barafu. Leo kwanza kanisalimia kitu ambacho hata wewe umeshangaa.

Muziki sasa, hebu tuburudike na muziki, asante sana wote mliotuburudisha na sogozi za kuvutia na uongo dhambi mwenzenu nimefunga na sikujua kama Tumosa ana chura wa maana asiyetosha kwenye bodaboda ila bajaj yenye air condition

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom