Obe
Platinum Member
- Dec 31, 2007
- 10,282
- 35,652
Tafasiri Unavyoweza: Mhanga Kupenda
Ninaandika nikikuandikia wewe mdogo wangu, ninaandika kwa sababu unanihusu. Sababu nyingine ya kuandika ni kwa sababu nimepitia na ninapenda kuandika. Hakuna ubaya kufanya jambo kwa ajili ya mtu, ila usijitoe zaidi pale anapokuchukulia poa kwa kile unachomfanyia. Ujinga wakati wa kwenda. Usiwe mhanga mara mbili, ikitokea mara ya pili basi wewe si mhanga, umependa. Tafasiri unavyoweza.
Mhanga ninayoiongelea hapa sio ile ya 'a victim' kama mhanga wa vita, mafuriko, ugaidi, uonevu wa kisiasa n.k. naongelea mhanga wa mtu mwingine kukuchukulia poa (taking advantage of you). Akiamini kabisa kuwa kwake wewe hugeuki hupinduki. Kwake wewe ni fursa ya upande mmoja, hakuna cha mia mia, unamfaidisha wewe unaumia. Huu ndo uhanga ninaouongelea hapa, kwa kizungu cha UK wanauita 'dupe' (tamka dYoop). Maana wewe unadanganyika kiurahisi kisa unapenda sana. Hutaanza wewe kupenda na hutakuwa wa mwisho. tafasiri unavyoweza.
Naandika kama shairi, halina vina, lakini mizani utaipata ukinisoma kama wimbo mpya na baadaye utasahau. Maisha ndivyo yalivyo, uhuru uko kwenye kusahau. Jipende mwenyewe kwanza, nafasi ya kwanza ni ya kwako, huu si ubinafsi ni ukweli maana ulipompa nafasi ya kwanza alikuchezea, alicheza na moyo wako. Somo umelipata, jitendee haki, wa pili awe wa kwanza kukufuata wewe na kukuambia shida yake kwako, kama ni kupenda leo awe wa kwanza kusema anakupenda.
usijipe nafasi ya kupoteza, wewe ni wa thamani, mama yako kama hakukukumbusha basi hukumsikia akiongea maana hukumuangalia usoni ulikuwa unaangalia chini. Fungia moyo wako kabatini na funguo kaa nazo, ukitaka kumfungulia mtu naye aje akuoneshe kuwa moyo wake kaufungia kabatini, mbadilishane funguo. wewe ni wa thamani na si samani ya kuhamishwa hapa na kule. Tafasiri unavyoweza. Ningependa unisome zaidi mdogo wangu, nakuita mdogo wangu si kwa sababu ninakuzidi umri, hapana, ni kwa sababu ninaandika kwa mkono mmoja.
Ninaandika nikikuandikia wewe mdogo wangu, ninaandika kwa sababu unanihusu. Sababu nyingine ya kuandika ni kwa sababu nimepitia na ninapenda kuandika. Hakuna ubaya kufanya jambo kwa ajili ya mtu, ila usijitoe zaidi pale anapokuchukulia poa kwa kile unachomfanyia. Ujinga wakati wa kwenda. Usiwe mhanga mara mbili, ikitokea mara ya pili basi wewe si mhanga, umependa. Tafasiri unavyoweza.
Mhanga ninayoiongelea hapa sio ile ya 'a victim' kama mhanga wa vita, mafuriko, ugaidi, uonevu wa kisiasa n.k. naongelea mhanga wa mtu mwingine kukuchukulia poa (taking advantage of you). Akiamini kabisa kuwa kwake wewe hugeuki hupinduki. Kwake wewe ni fursa ya upande mmoja, hakuna cha mia mia, unamfaidisha wewe unaumia. Huu ndo uhanga ninaouongelea hapa, kwa kizungu cha UK wanauita 'dupe' (tamka dYoop). Maana wewe unadanganyika kiurahisi kisa unapenda sana. Hutaanza wewe kupenda na hutakuwa wa mwisho. tafasiri unavyoweza.
Naandika kama shairi, halina vina, lakini mizani utaipata ukinisoma kama wimbo mpya na baadaye utasahau. Maisha ndivyo yalivyo, uhuru uko kwenye kusahau. Jipende mwenyewe kwanza, nafasi ya kwanza ni ya kwako, huu si ubinafsi ni ukweli maana ulipompa nafasi ya kwanza alikuchezea, alicheza na moyo wako. Somo umelipata, jitendee haki, wa pili awe wa kwanza kukufuata wewe na kukuambia shida yake kwako, kama ni kupenda leo awe wa kwanza kusema anakupenda.
usijipe nafasi ya kupoteza, wewe ni wa thamani, mama yako kama hakukukumbusha basi hukumsikia akiongea maana hukumuangalia usoni ulikuwa unaangalia chini. Fungia moyo wako kabatini na funguo kaa nazo, ukitaka kumfungulia mtu naye aje akuoneshe kuwa moyo wake kaufungia kabatini, mbadilishane funguo. wewe ni wa thamani na si samani ya kuhamishwa hapa na kule. Tafasiri unavyoweza. Ningependa unisome zaidi mdogo wangu, nakuita mdogo wangu si kwa sababu ninakuzidi umri, hapana, ni kwa sababu ninaandika kwa mkono mmoja.