Makapuku Forum

Makapuku Forum

1911>Alizaliwa Ronald Reagan rais wa Marekani(1981-89)

Kutoka familia ya kimaskini hadi urais.

Government's view of the economy could be summed up in a few short phrases: If it moves, tax it. If it keeps moving, regulate it. And if it stops moving, subsidize it.

abc_archive_SPBB8803A_wg.jpg
 
Tafasiri Unavyoweza: Nguvu Unayo, Itumie

Ankal wangu ana usemi wake ambao napenda niutumie leo kwenye kipengele hiki cha kutafasiri unavyoweza. Usemi wenyewe ndo huo kwenye kichwa cha habari (title). Kila mwenye uwezo, ana nguvu. Hapa nieleweke kabisa nguvu nazoziongelea hapa ni zaidi ya nguvu za mwili. Nimesema haya ili kuiweka sawa tafasiri ya nguvu uliyonayo ninayoingelea hapa, sio utafasiri kwa kuweka nguvu za kike au za kiume, kichwa cha nyoka hakibebi mzigo.

Naongelea nguvu uliyonayo ambayo unayo inayoweza kushawishi, kubadili masuala yanayokuzunguka na kubadili tabia (social power). Nguvu hii ninayoiongelea hapa huzaliwi nayo, unaipata kupitia kuwa na utambuzi sahihi (well informed), na ukiikosa nguvu hii basi ni bila shaka utajikuta unapelekwapelekwa bila kujua unakopelekwa ndiko au siko unakotaka kwenda. Mtu mwenye taarifa ana nguvu, kubali au kataa, hawezi kunyanyaswa kijinga, anajua haki zake na wajibu wake kwa jamii. akienda kupiga kura anaiambia kura yake ifanye nini anachokitaka na wala haongozwi na mapenzi yakishabiki.

Tafasiri unavyoweza, social power unaihitaji sana kama unavyohitaji nguvu nyingine za mwili. Ukikosa nguvu ya ushawishi basi tambua kuwa kitakachoumia ni nguvu zako za mwili. Tafuta maarifa uweze kuzifanya nguvu za mwili ziwe na maana kwenye jamii. Tafasiri unavyoweza
 
Kutokana na kipaji changu cha kutabiri, nayaona yafuatayo kwako:
1. Umeshika simu yako ya mkononi.
2. Unasoma hii habari.
3. Wewe ni binadamu hai kabisa.
4. Huna jeuri ya kusema neno PIPI bila kufungua mdomo.
5. Ha ha ha nakuona umejaribu kusema neno PIPI.
7. Unajicheka mwenyewe.
8. Nimeona meno yako.
9. Unatabasamu!
10. Umeruka namba 6.
11. Ha ha ha ha unacheki kama kuna namba 6.
12. Umetabasamu!
....Nilipe gharama ya utabiri
 
Muziki: Siuelewi, Naupenda

..mjomba wangu bhana, yeye huwa hana cha mswalie mtume, akitaka kufanya jambo humkatazi. Ni ngumu kumkataza kwa sababu kwanza huwa anaanza kwa kutafiti ili ajiridhishe kabisa kabla hajalifanya hili jambo. Ni msomi na anajuaga anafanya nini. Nikusalimie Kapuku mwenzangu na kukwambia kuwa wewe ni mtu mwema sana na unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu bora kabisa, asante.

Ni masaa machache yamekaribia kufikia jumatano, fyi. si kila unachopenda unakielewa, vingine huwa tunapenda kwa sababu tu unapenda. Kupenda bila sababu, hakuna ubaya kupenda bila sababu, shida inakuja pale unapoamua kupenda bila sababu na kile unachopenda hakikupendi. Mimi napenda kiinglishi lakini chenyewe hakinipendi, nikiongea wiki tu kitambi chote kinapungua, si nzuri kwa afya yangu ya muonekano.

Muziki sasa, siuelewi kabisa huu wimbo lakini naupenda. Hulazimishwi kuupenda maana kupenda ni uamuzi wa moyo.

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom