Makapuku Forum

Makapuku Forum

IMG-20180116-WA0017.jpg
 
Tafasiri Unavyoweza: Mkataba

Tunaingia kwenye makubaliano tofauti na ya kila namna mara nyingi na kila wakati. Iwe ni makubaliano yanayohusiana na makazi, mahusiano, ajira, kilimo, biashara, matumizi ya mtandao, mawasiliano na taja makubaliano yoyote ambayo umewahi kuingia au unapanga kuingia. Makubaliano haya ama unaingia na mtu mmoja au kundi (entity) kiufupi yanaitwa mkataba. Serikali yetu huingia mkataba na serikali nyingine, watu binafsi, makampuni na usisahau wananchi tunaiweka serikali madarakani kwa mkataba.

Tafasiri unavyoweza, mkataba waweza kuwa wa mdomo au maandishi. Mkataba ni makubaliano ya pande mbili au zaidi (reciprocal or mutual agreement) kukubaliana au kutokubaliana kufanya jambo mahsusi. Mkataba mzuri ni wa maandishi, huu huleta uwajibikaji na rejea ya yale mliyokubaliana, mnaweza kukaa na kufanya mabadiliko juu ya mlichokubaliana au kukataliana.

kwa kuwa mkataba ni makubaliano au kutokubaliana juu ya kitu, ukikiuka mkataba basi tegemea kulipishwa au kulipa fidia, uharibifu, usumbufu, kufilisiwa, na adhabu nyingine zinazoendana na mkataba.

Tafasiri unavyoweza, makubalianao sahihi huja kwa sababu una taarifa sahihi, hautishwi, hujachochewa, hujahemka na una akili timamu. Usiingie mkataba kama huna hayo niliyosema vinginevyo unaweza kujikuta matatizoni. Kura yako kwa chama unachokipa madaraka ni kukubaliana na sera zake, kisipotimiza mlichokubaliana basi kuna sababu gani ya kukirudisha madarakani wakati mwingine! Tafasiri unavyoweza

contract_pressure_sign_text_10626.gif
 
Muziki: Mabadiliko

.....mabadiliko ni muhimu sababu hutokea na sababu. Mabadiliko mengine yanakubadilisha na ukijidai kupingana nayo yanakubadilisha. Ndivyo ilivyo, kubali ukatae. Ninakusalimia kapuku mwenzangu ninayekuheshimu na kukuthamini sana maana wewe ni mtu makini na Forum hii ni nzuri kwa sababu wewe u sehemu yake.

Wikend yangu ilikuwa nzuri, kupumzika na kuendelea kusoma kitabu ambacho nimekipata hivi karibuni kama zawadi. Mhh, zawadi ya kipekee kabisa japo ungeniambia nichague zawadi wala nisingepepesa macho kusema nachagua kupewa zawadi ya 'hela'. Unajua zawadi mweiz Januari inapaswa kuwa hela na si vitu vingine kama kitabu au maua. BTW, kwetu sisi zawadi za maua na vitabu hatujafikia karne hiyo, hayo ni mambo ya kizungu.
Kwanini nimekuja na ishu ya mabadiliko nikiitazama Januari, yes, huu nimwezi dume, mwezi wa kodi, ada, na bills za kumwaga, ni mwezi unaoset miezi mingine itakuwaje kwani ni mwanzo wa mwaka. mabadiliko januari ni muhimu na ni vizuri kubadilika hali ya chini kwenda juu, ubaya kwa uzuri na usilipe ubaya kwa ubaya, utaongeza chuki na ukitaka kuiondoa lipa ubaya kwa upendo.

Muziki sasa, ninakufurahia sana Kapuku wewe na sioni haya kulisema hili maana unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu znuri kabisa ya kuwepo. Burudika na muziki leo zamani

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom