
TUOMBE:
Bwana Yesu asante kwa ljumaa njema ya leo. 29 DESEMBA 2017
Baba hata kufika tarehe hii ya leo ni kwa neema,Mungu wetu tupe kumalizia mwaka huu salama huku tukikuangalia wewe mfalme wa Amani.
Asante kwa ulinzi wako kwetu Mungu Mkuu
Umetulinda
Bwana wa majeshi
Ni wengi walitamani kuiona hii siku lakini hawakuweza kufika.
Baba siku ya leo ni siku ambayo wengi Tunakuwa ktk maombi
Mungu ninakuomba katika Jina la Yesu Kristo Maombi yetu Bwana yakawe ni manukato mazuri mbele zako.
Kumbuka wenye shida mbali mbali
Taabu na mateso ya kila aina EeeMungu ukawakumbuke
Angalia ndoa/familia ambazo hazina amani wala furaha
Mungu warudishie upendo wao wa kwanza
Ambao hawajakujua wewe Mungu wa kweli katika jina la Yesu Kristo Bwana ukawaokoe.
Kumbuka wamama wanaohitaji Watoto
Bwana ukafungue matumbo yao.
Na wale wajawazito wawe salama pamoja na uhai uliowakabidhi wautunze na kuuleta duniani..wape kujifungua salama.
Waangalia Wanafunzi, wagonjwa ,Yatima na wajane
Wakumbuke BWANA Yesu
Nimeomba haya nikiamini,NA nashukuru maana utatenda sawa na mapenzi yako katika Jina la Yesu Kristo wa Nazareth
AMEN
IJUMAA NJEMA..MBARIKIWE

