
TUOMBE
Baba katika Jina la Yesu Kristo Asante kwa siku mpya ya Jumamosi tarehe 30 DESEMBA
2017 ambayo umetuchagua tena tuweze kuuona Utukufu wako
watu wengi walitamani nafasi hii hawajaweza kuiona siku ya leo uliwatwaa Baba tunaomba uwapokee wapumzike kwa Amani.
Karibu Roho Mtakatifu shusha Mapaji tuwe Imara siku ya leo
BABA Tunakuomba Utusamehe makosa yetu yote ambayo tumetenda kwa mawazo kwa maneno kwa matendo na kutotimiza wajibu wetu mbalimbali tulionao
Uturehemu twakusihi Baba yetu
Tunaomba utusaidie kuwasamehe wale wote waliotukosea Mfalme wa Amani walioomba msamaha na wale ambao hawajaomba msamaha tuwasamehe na kuyasahau yote waliyotutendea
Wabariki wote katika Ndoa zetu na nyua zetu familia zetu czzz Waume Wake Watoto Wasaidizi wa ndani Ndugu Jamaa Marafiki Wachumba wakutafute wewe Baba
Bariki Watumishi wote wa Mungu wote ulimwenguni uwaandae Baba wakalishe Waumini kinachokupendeza na ukaonekane kwa watu wote katika huduma
Bariki viongozi wa Serikali wakutafute kwa
Bidii Nchi iwe na Amani wakatende haki na kuwa na hofu yako Baba.
Baba Ponya Wagonjwa na ponya dawa wanazotumia na wanawauguza waweze kutoa huduma kwa Upendo wasipungukiwe.
Tunakushukuru kwa uponyaji unaoendelea Baba kwa wagonjwa wetu wote tunaomba afya zao zizidi imarika
Walinde wajawazito wote na wanaojifungua Baba umewapa kibali cha kushiriki kazi ya uumbaji kila walichobeba ni wazo lako Baba tunaomba wawe salama mikononi mwako wao na viumbe ulivyowakabidhi mfalme wa Amani
Asante kwa uwepo wako katika vipindi vyote vya uumbaji na ushiriki wao
Baba Bariki wasafiri na vyombo Majini Nchi Kavu na hata Angani ukawe Dereva mwema Damu ya Yesu itufunike tuendako na tunakotoka
Baba wafariji Wafiwa Wajane Wagane Yatima Wafungwa Mahabusu Wenye huzuni na wahitaji wote Walioachwa Waliotelekezwa wasio na chakula Waliodhurumiwa wakuangalie na kukutegemea wewe tu maana imeandikwa Heri aliyemfanya Bwana kuwa Tumaini lake
Baba tunaomba Ubariki Sadaka zetu na matoleo mbalimbali tutakayokutolea na kabla hatujakutolea Basi Baba Tupatane na Wenzetu Tuwasamehe Tuwapende na Kuwaheshimu.
Epusha Wivu Visasi Masengenyo Chuki Dharau Kiburi Kujisahau na Majivuno ili Sadaka zetu Zikakubalike mbele yako ziwe za Kukupendeza Mfalme wa Amani
Bariki kila kazi za mikono yetu ziwe Halali na za kukupendeza
Baba mwema tunausubiri mwaka mpya tunaomba neema yako tufike salama .
Baba Asante kwa Sababu Unatupenda na utajibu sawasawa na mapenzi yako Amen
Tunaomba yote haya kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth Amen
JUMAMOSI NJEMA WAPENDWA
DAMU YA YESU ITUFUNIKE
SHALOM
