Makapuku Forum

Makapuku Forum


Muziki: Kufungia Mwaka


Nikutakie wikend njema ya mwisho wa mwaka 2017. Sina hakika kama nitakuwa nimejiwahisha sana nikikutakia mwisho mwema wa 2017. Kapuku wewe, na unajijua kuwa muda wote tangu tumekutana humu mwanzo wa 2017, umekuwa ni ntu makini, mwelewa, mcheshi, mkali, mpuuzi, unayejali, mwenye utayari wa kusaidia na kuongea kilichoko moyoni mwako. Hata mimi nimekuwa hivyo hivyo maana nami kama wewe ni binadamu asiyekamilika.

Natamani kukuambia kitu ambacho unajua kabisa nimekuwa sichoki kukwambia kila mara. Wewe, yes wewe unayesoma aya hii, bila uwepo wako hapa Jukwaa hili lingebaki kuwa la kawaida sana, lakini kwa sababu wewe uko hapa na umeweka input za maana kulisongesha jukwaa hili, MF imekuwa ni jukwaa bora sana. Shukrani sana.

Binafsi nimejifunza mengi hapa, maarifa ya kutosha nimeyapata hapa. Tofauti zetu zimekuwa ni nguvu yetu, nakosa maneno mazuri ya kukwambia wewe mtu makini kabisa na umekuwa na nafasi ya kipekee katika maisha yangu.

Muziki sasa, leo ni maneno matupu, nitajitahidi kuchagua muziki nilioamini ulibamba vizuri hapa, ni kwa maoni yangu na Jumapili nitakukaribisha kuchagua wimbo wako uliokushika katika kipengele hiki, kwa hizi siku chache zilizobaki kumaliza mwaka. Wikend njema
Asante Obe ubarikiwe
 
ISAYA 62

6."Juu ya kuta zako ee Yerusalemu nimeweka walinzi,usiku na mchana kamwe hawatakaa kimya"

Enyi mnaomkumbusha Mwenyezi -Mungu ahadi yake, msikae kimya;

USIKU MWEMA DAMU YA YESU IWAFUNIKE..

MSIKAE KIMYA MKUMBUSHE BWANA AHADI YAKE.
 
tenor.gif
Hapafunguki..na pia muziki sijauona ...God Bless U
 
Asante Obe ubarikiwe
Asante BH, unanipa tabasamu kila wakati kwa namna ambayo bila kuchoka unatuweka sote katika sala zako.
Hata tu/napokukera bado hujawahi kubadili utaratibu wa kuniombea mimi na member wote bila kujali.

Hata unaponikera kwa kutosoma tule tumaandishi twangu tudogooo bado sichoki kukwambia, wewe ni wa kipekee yaani maneno mawili tu, awesome you. Usiku mwema
 
Asante BH, unanipa tabasamu kila wakati kwa namna ambayo bila kuchoka unatuweka sote katika sala zako.
Hata tu/napokukera bado hujawahi kubadili utaratibu wa kuniombea mimi na member wote bila kujali.

Hata unaponikera kwa kutosoma tule tumaandishi twangu tudogooo bado sichoki kukwambia, wewe ni wa kipekee yaani maneno mawili tu, awesome you. Usiku mwema
Asante sana kwa kujali..wewe ni wa pekee sana Obe namshukuru Mungu kwa ajili yaako akubariki na akulinde Baba siku zote za maisha yako
 
Asante BH, unanipa tabasamu kila wakati kwa namna ambayo bila kuchoka unatuweka sote katika sala zako.
Hata tu/napokukera bado hujawahi kubadili utaratibu wa kuniombea mimi na member wote bila kujali.

Hata unaponikera kwa kutosoma tule tumaandishi twangu tudogooo bado sichoki kukwambia, wewe ni wa kipekee yaani maneno mawili tu, awesome you. Usiku mwema
Mtaasisi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom