Makapuku Forum

Makapuku Forum

‹The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 53
ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA...

Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.
“Najua unampenda binti yangu Togo, lakini nakuomba sana mwanangu, ukifanya naye mapenzi tutampoteza, yeye si miongoni mwa jamii yetu na mwili wake hauna kinga yoyote, hebu zingatia sana ninachokwambia, nakuomba usimguse,” baba yake Rahma alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkubwa.
Tofauti na baba ambaye kila akiongea alikuwa akifokafoka, baba Rahma alikuwa akizungumza kwa utaratibu sana na nikajikuta nikimuelewa sana.
Jambo ambalo nilishindwa kulikataa ndani ya moyo wangu ni kwamba nilikuwa nikimpenda sana Rahma kwa hiyo akili za harakaharaka zilianza kunituma kufikiria namna ninavyoweza kukivuka kikwazo kilichokuwepo kati yetu kwani kiukweli sikuwa tayari kumpoteza.
“Kwa hiyo na yeye akiwa miongoni mwetu tutaruhusiwa kuoana?” niliuliza swali ambalo liliwafanya baba na baba Rahma watazamane kwa sekunde kadhaa.
“Lakini si unajua kwamba mwenzako anasoma na siku chache zilizopita mama yake alikuwa akifuatilia mambo ya chuo?”
“Hata akimaliza hakuna shida,” nilijibu huku nikiwa na wasiwasi na atakachokisema baba.
“Wewe mtoto mpumbavu sana, yaani umeshupalia kabisa, ina maana hujui kama nyie mmeshakuwa ndugu? Halafu hiyo michezo ya mapenzi umeianza lini wakati wewe bado mdogo?”
“Lakini baba mimi nampenda Rahma.”
“Unampenda? Unajua maana ya kupenda wewe? Toka lini wewe ukampenda mtu? Hebu toa wendawazimu wako hapa, yaani badala uelekeze nguvu kwenye ulimwengu mpya tuliokufunulia unaanza mambo yako ya mapenzi hapa, una akili wewe?” baba alinifokea.
“Hapana, huna haja ya kuwa mkali mzee mwenzangu,” baba yake Rahma alimkatisha baba kisha akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa.
“Unampenda kwa kiasi gani?”
“Nampenda sana baba.”
“Lakini nyie mmeshakuwa ndugu?”
“Mbona undugu wetu siyo wa damu?”
“Kama kweli unampenda, nakuomba uzingatie nilichokwambia, hayo mengine tuachieni sisi wazazi wenu,” baba yake Rahma alisema kwa upole. Ilihitaji ujasiri mkubwa kuzungumza mambo yale mbele ya baba lakini kwa kuwa baba Rahma alikuwa mwelewa, na mimi nilijikuta nikipata nguvu.
Majibu aliyonipa, yaliufanya moyo wangu ufurahi sana, nikajiapiza kwamba sitakutana naye tena kimwili kwa kuhofia kumpoteza lakini nikawa nafikiria mbinu nyingine mbadala na harakaharaka akili zangu zilinituma kutafuta muda wa kutosha wa kukaa na Rahma na kumweleza ukweli kuhusu mimi, baba na baba yake na mwisho nimshawishi na yeye ajiunge kwenye jamii yetu.
Tayari nilishaanza kuona dalili za ushindi, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu, hisia tamu zikawa zinapita kwenye mishipa yangu huku nikivuta picha ya miaka kadhaa baadaye, nikiishi na Rahma kama mume na mke halali.
“Kilichotuleta hapa siyo hiki tulichokuwa tunakizungumza,” baba yake Rahma alivunja ukimya, baba akawa anatingisha kichwa kukubaliana naye huku akiwa amenitolea macho ya ukali.
“Leo umefanya kitu cha ajabu sana na kama isingekuwa nguvu za ziada kutumika, ungeweza hata kuuawa kule Mlandizi, kama hiyo haitoshi umesababisha majanga mengine ambayo hayakuwepo kwenye ratiba, umesababisha yule dereva wa bodaboda amepoteza maisha,” alisema baba yake Rahma, kauli ambayo ilinishtua kuliko kawaida.
Kilichonishtua zaidi ni kusikia kwamba yule dereva wa bodaboda amekufa, moyo ulishtuka kuliko kawaida.
“Kibaya zaidi umesababisha watu hapa mtaani waanze kututilia mashaka, kwa nini umeenda kumroga huyo kijana dereva wa Bajaj hapo nje? Hujui kama ni hatari sana watu kujua kama unajishughulisha na haya mambo ya giza? Mtoto mpumbavu sana wewe,” baba aliongezea kwa ukali, nikajiinamia kwani kiukweli nilikuwa nimefanya makosa makubwa.
“Lakini nilikuwa nataka kujifunza,” nilijibu kwa sauti ya chini, baba yake Rahma akaniambia kwamba mambo hayo huwa hujifunzi kama unavyojifunza mambo mengine, bali kuna utaratibu wake.
Akaniambia kwamba nilichokifanya kilikuwa makosa makubwa kwa watu wa jamii yetu na kama zilivyo sheria, yeyote anayeenda kinyume lazima akumbane na rungu la Mkuu. Kauli hiyo ilizidi kunitisha moyoni mwangu, nikajaribu kuvuta taswira ya Mkuu, yule kiongozi wa watu wa jamii yetu, hofu ikazidi kunijaa.
“Ili kumfurahisha, inabidi usiku wa leo ufanye juu chini nyama zipatikane, tukifika tutaenda kukuombea msamaha na kwa kuwa utakuwa na mzigo, bila shaka atakupa adhabu ndogo, kinyume na hapo anaweza hata kuamuru uliwe nyama ukiwa hai,” alisema baba yake Rahma, nikajikuta nikitokwa na kijasho chembamba.
Baba Rahma aliniona hali niliyokuwa nayo, akaniambia nisijali watanisaidia lakini kitu cha kwanza, ilikuwa ni lazima nikatoe sadaka ya kitu ninachokipenda zaidi, nje ya familia yangu.
Sikumuelewa kauli yake hiyo, akanifafanulia kwamba wanaposema kitu, kwenye imani yao wanamaanisha mtu kwa hiyo ilikuwa ni lazima nimfikirie rafiki yangu ninayempenda zaidi ambaye ndiye angetolewa kafara usiku ili mimi nisamehewe na Mkuu kwa kitendo changu cha kwenda kwenye msiba wa mtu ambaye tumemla nyama na mimi ndiye niliyesababisha kifo chake.
“Mimi sina rafiki hapa mjini, kwanza sijazoeana na mtu yeyote,” nilijitetea, baba akaniambia kwamba anawajua marafiki zangu wengi tu Chunya.
“Sasa nitaendaje Chunya?”
“Hutakiwi kuhoji kwa sababu hakuna kisichowezekana, unachotakiwa ni kututajia mtu, vinginevyo wewe ndiyo utaaliwa leo,” baba alisema, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi huwa na kawaida ya kuwatoa kafara watu wao wa karibu na ndiyo maana watu wakishajua kwamba wewe ni mchawi wanajitenga na kukuogopa sana lakini nilikuwa naona kama ni hadithi za kufikirika tu, lakini sasa yalikuwa yamenifika.
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 54
ILIPOISHIA:
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
SASA ENDELEA...

“Lakini baba...”
“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.
Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.
“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.
Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.
Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.
Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.
Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.
Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.
Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.
Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.
“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.
“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.
“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.
Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.
Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.
“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.
Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.
“Umeshajiandaa?”
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.
“Haya nifuate.”
“Lakini bado sijala.”
“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.
Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.
Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!
Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.
Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.
Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.
Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.
Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.
“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.
“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 49
ILIPOISHIA:
Ndani ya dakika mbili tangu tukae mkao huo, kuna mambo ya ajabu yalianza kunitokea, mapigo ya moyo yakawa yanazidi kwenda mbio kuliko kawaida kutokana na kile nilichokuwa nakishuhudia.
SASA ENDELEA...

Nilianza kuona ile hali kama ambayo ilinitokea siku ile nilipovamiwa barabarani na kujeruhiwa vibaya na baadaye kuingia kwenye ulimwengu wa tofauti, nikawa najihisi kwamba japokuwa nilikuwa nimekaa pale chini na wenzangu, taswira nyingine ya mwili wangu ilikuwa ikianza kupaa juu na kuelea angani, nikawa sielewi nini kinachotaka kutokea.
Cha ajabu ni kwamba, yule aliyekuwa akianza kupaa ndiyo alikuwa mimi kwa sababu nilikuwa najitambua kabisa, nikainamisha kichwa na kutazama chini, nikajiona nikiwa nimekaa pale juu ya zulia, nikiwa nimeshikana mikono na yule mwenyeji wetu, Raya na Firyaal, jambo ambalo lilisababisha hofu kubwa ndani ya moyo wangu.
“Noo! Sitaki kufa tena, sitakiii,” nilisema kwa sauti ya juu, nikashtukia nikiporomoka kutoka pale juu nilipokuwa nikielea, nikaanguka chini kama furushi na kujibamiza sakafuni kwa kishindo.
Nilipofumbua macho, kila mtu alikuwa amepigwa na butwaa akiwa ni kama haamini kilichotokea, nikawa nahema kwa nguvu huku nikiwa nimelala sakafuni, sikukumbuka hata niliwaachia wenzangu mikono saa ngapi, wote wakabaki kunishangaa.
“Hutaki kufa tena? Unamaanisha nini?” aliniuliza yule mwenyeji wetu, nikainuka pale nilipokuwa nimeanguka na kukaa, nikawa nawatazama mmoja baada ya mwingine huku nikijihisi aibu kubwa usoni.
“Naongea na wewe kijana, vipi mbona sikuelewi?” yule mwenyeji wetu alizidi kunibana kwa maswali lakini sikuwa na cha kujibu, Raya na Firyaal wote wakawa wanaendelea kunitazama kwa macho ya mshangao, kila mmoja akionesha kuwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia nitajibu nini.
“Hata sielewi kilichotokea,” nilisema, wote wakashusha pumzi ndefu na kutazamana.
“Hebu naombeni mtupishe mara moja mimi na Jamal, alisema yule mwanamke ambaye kiumri alikuwa mtu mzima, Raya na Firyaal wakasimama na kutoka mle chumbani, wakaenda kukaa sebuleni, nikawa nawasikia wanazungumza lakini sikuelewa walikuwa wakizungumzia nini ingawa nilijua kwamba walikuwa wakiniongelea.
“Hebu niambie ukweli, umeona nini au kipi kilichokutokea?” aliniuliza mwanamke huyo wa makamo, mweupe na mnene kiasi, niligeuka huku na kule na nilipohakikisha tupo wawili tu, nilimuuliza swali juu ya swali.
“Umesema OBE ni nini?”
“Mbona nakuuliza swali unaacha kunijibu na wewe unaniuliza? Tupo nyuma ya muda na tunatakiwa kufanya haraka kumsaidia Shamila, niambie nini kimetokea?”
“Ninachotaka kukwambia kinahusiana na hiyo OBE na nahisi hii si mara ya kwanza kutokewa na hiki kilichonitokea,” nilimwambia, kwa mara nyingine akashusha pumzi ndefu na kunitazama. Nadhani alihisi kwamba sikuwa huru kuzungumza kwa sababu mara kwa mara nilikuwa nikigeuka na kutazama mlangoni.
Ikabidi ainuke na kwenda mpaka mlangoni, akaufunga na kurudi pale nilipokuwa nimekaa, safari hii akanisogelea karibu huku akinitazama kwa macho ya udadisi.
“Shamila si ni rafiki yako?”
“Ndiyo.”
“Unamuamini?”
“Ndiyo. Vipi kwani?”
“Kama unamuamini Shamila basi nakuomba uniamini na mimi, your secrets are safe with me (siri zako zitakuwa salama ukiwa na mimi) aliongea kwa kuchanganya na Kiingereza kuonesha kwamba alikuwa ameenda shule. Kabla sijamjibu, akaendelea:
“Nikikutazama kuna kitu nakiona lakini siwezi kukielezea mpaka mwenyewe uniambie. Halafu inaonekana kuna jambo halipo sawa kwenye mwili wako, una wapenzi wangapi?” aliniuliza swali ambalo lilinishtua sana, nikashindwa kumuelewa alikuwa ameona nini kwangu na swali lile lilikuwa na uhusiano gani na nilichomuuliza.
Nikashindwa cha kumjibu zaidi ya kubaki nikimkodolea macho usoni, akanishika mkono na kunifanya nizinduke. Sijui kwa nini hali ya mawazo kutengana na mwili wangu ilikuwa ikinitokeatokea sana safari hii. Yaani ilikuwa unaweza kuniona nakutazama ukahisi akili zangu zipo pale lakini kumbe nikawa nawaza kitu kingine tofauti kabisa.
“Shamila ni mwanangu, mimi ni mama yake mdogo kwa hiyo nakuomba tena usiwe na wasiwasi unapokuwa na mimi, hebu nijibu maswali yote niliyokuuliza, sawa baba,” aliongea kwa lugha ya upole na kubembeleza, nikashusha pumzi ndefu na kidogo nikaanza kuhisi amani ndani ya moyo wangu.
“Nina mpenzi mmoja tu, kwa nini umeniuliza?”
“Unajua kwa mtu mwenye utaalamu wa elimu ya nguvu zisizoonekana kama mimi, nikikutazama tu naweza nikajua wewe ni mtu wa namna gani. Nikikuangalia naona kama kwa siku za hivi karibuni umekutana kimwili na zaidi ya mwanamke mmoja na inaonesha pia upo kwenye mipango ya kufanya hivyo kwa wanawake wengine zaidi, kama nimekosea naomba unisamehe,” alisema yule mwanamke, kauli iliyozidi kunishangaza mno.
Alichokisema kilikuwa kweli, nilikuwa nimekutana kimwili na Raya na Shamila kwa kuwachanganya ingawa wenyewe hawakuwa wakijua chochote na kama hiyo haitoshi, nilikuwa kwenye mipango ya kufanya hivyo kwa Firyaal pia ambaye yeye ndiye aliyeonesha kunipenda mimi zaidi na kujikuta nikishindwa kuendelea kuvunga.
“Anyway, najua hayo ni mambo ya ujana tuachane nayo lakini kubwa nahisi kama umewahi kutokewa na jambo kubwa sana linalokufanya uwe tofauti na binadamu wengine na ndiyo maana hapa umekwamisha tulichokuwa tunataka kukifanya. Inaonesha una nguvu kubwa sana ambazo pengine hata wewe mwenyewe hujui na ndizo zinazokutesa,” alisema na kuzidi kunichanganya kichwa.
“Unamaanisha nini unaposema nguvu zisizoonekana?”
“Kwani wewe uliposema hutaki kufa tena na ukavuruga kazi tuliyokuwa tunaifanya ulimaanisha nini?” mfumo wa swali juu ya swali uliendelea kutawala katika mazungmzo yetu.
“Umewahi kufika kuzimu?” aliniuliza swali lingine, nikatingisha kichwa harakaharaka kukataa lakini alinigundua kwamba kuna jambo namficha.
“Hapo kifuani umefanya nini?” aliniuliza, eti na mimi nikawa najitazama kama najishangaa, akajua kwamba nilikuwa na mambo mengi ninayoyaficha, akazungumza kwa sauti yenye mamlaka sasa”
“Sikia, kama bado huniamini huwezi kuwa na msaada wowote katika hili tunalotaka kulifanya, itabidi wewe ukakae sebuleni utusubiri mimi na hao wenzako tufanye kinachowezekana kumuokoa Shamila, haupo tayari kushirikiana na sisi, yaani ni kama nakulazimisha hivi.”
“Hapana, siyo hivyo.”
“Siyo hivyo nini? Muda unazidi kuyoyoma, Shamila yupo kwenye matatizo, kila nachokuuliza unanichenga sasa unataka nifikirie nini?” alisema huku akisimama, akionesha kuchukia.
Siyo kwamba sikuwa tayari kumjibu maswali yake lakini alichonichanganya alikuwa akitaka kujua vitu vingi kwa wakati mmoja, wakati mambo yenyewe hayakuwa mepesi kuyafafanua mpaka mtu akaelewa.
“Nataka kumsaidia Shamila,” nilisema.
“Nijibu maswali yote niliyokuuliza.”
“Nitakujibu lakini itakuwa ni baada ya kumaliza kazi ya kumsaidia Shamila.”
“Hapana, wewe una nguvu kubwa sana ambazo mwenyewe hujui namna ya kuzitumia, unaweza kufanya tena kama hiki ulichokifanya hapa ukasababisha tudhalilike huko nje tunakokwenda.”
“Hapana, nitajitahidi naomba uniamini.”
“Unaniahidi?”
“Ndiyo,” nilisema kwa kujiamini, akanitazama usoni kisha akaenda mlangoni na kufungua, akawaita Raya na Firyaal, wakaingia ndani na tukakaa tena kama tulivyokuwa tumekaa mwanzo, kazi ikaanza upya huku akinisisitiza kuwa makini na kuishinda hofu ndani ya moyo wangu, nikatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana naye.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 50
ILIPOISHIA:
“Ndiyo,” nilisema kwa kujiamini, akanitazama usoni kisha akaenda mlangoni na kufungua, akawaita Raya na Firyaal, wakaingia ndani na tukakaa tena kama tulivyokuwa tumekaa mwanzo, kazi ikaanza upya huku akinisisitiza kuwa makini na kuishinda hofu ndani ya moyo wangu, nikatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana naye.
SASA ENDELEA...

Kazi ilianza upya, akatusisitiza kila mmoja awe anavuta pumzi ndefu kwa kutumia tumbo na siyo kifua kama wengi tunavyopumua, pia akatutaka kuhakikisha kila mmoja akili yake aielekeza eneo la tukio.
Muda mfupi baadaye, ile hali ilianza kunitokea tena, nikawa najihisi kama naelea angani huku mwili mwingine ukiwa palepale tulipokuwa tumekaa. Hofu ilianza kunijia tena lakini nilipokumbuka maneno ya yule mwanamke, nilijitahidi kuishinda hofu.
Nikaendelea kutuliza kichwa na kufumba na kufumbua, nilijikuta nikiwa pale hospitalini nilipokuwa nimelazwa. Niliweza kuona kila kitu kilichokuwa kikiendelea, wagonjwa waliokuwa wakiingia na kutoka, manesi na madaktari waliokuwa wakikimbizana huku na kule kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano.
Upande wa Kaskazini kulikuwa na magari matatu ya polisi yaliyokuwa yamepaki huku askari wengi wenye silaha wakirandaranda huku na kule.
“Kumetokea nini kwani leo hapa?”
“Nasikia kuna wagonjwa wametoroshwa usiku sasa ndiyo polisi wamekuja kutafuta wahusika.”
“Mh! Yaani wagonjwa kutoroshwa tu ndiyo zije difenda kibao na askari utafikiri kuna vita?”
“Nasikia huyo mgonjwa mmoja ni mtoto wa kigogo mmoja mkubwa ndiyo maana unaona hali ipo hivi,” niliwasikia watu wawili wakihojiana, wakiwa wamesimama chini ya kivuli cha mti.
Ghafla nikasikia vishindo vya mtu akitembea kwa kasi nyuma yangu, nikageuka, katika mazingira ambayo sikutegemea, nilimuona askari mmoja mwenye bunduki, akiwa ananifuata pale nilipokuwa nimesimama, nikajua ameshaniona na kunitambua, nikawa natetemeka.
Cha ajabu, ni kwamba alinipita akiwa ni kama hajaniona na kuwafuata wale watu waliokuwa wakiendelea na majadiliano pale chini ya mti, nikamsikia akiwapa amri kwamba hatakiwi mtu yeyote asiyekuwa na shughuli maalum kuonekana ndani ya hospitali hiyo, akawataka watoke nje ya geti na kwenda nje kabisa.
Kidogo nilishusha pumzi kwani nilikumbuka mara nyingi ninapokuwa kwenye hali kama ile, huwa siwezi kuonekana kwa macho ya kawaida. Harakaharaka nikawa nawafuata wale manesi na madaktari kule walikokuwa wanaelekea kwa lengo la kwenda kuona kinachojadiliwa.
Cha ajabu zaidi, nilipofika kwenye mlango wa kuingilia kwenye ule ukumbi, nilimkuta yule mwanamke, mama yake mdogo Shamila naye akiwa ameshafika, nikamtazama nikiamini yeye hawezi kuniona. Cha ajabu na yeye aligeuka haraka na kunikazia macho, tukawa tunatazamana.
Nilijifunza kitu kingine kwamba kumbe ukiwa katika hali ambayo huwezi kuonekana kwa macho ya kawaida, akija mtu mwingine ambaye naye anakuwa kwenye hali kama yako, mnaweza kuonana vizuri, yaani yeye akakuona na wewe ukamuona ingawa watu wengine wa pembeni wanakua hawana uwezo wa kumuona yeyote kati yenu.
Alinisogelea na kunigusa, kingine cha ajabu ni kwamba nilihisi kabisa kwamba nimeguswa na mtu, akanivutia pembeni na kuanza kuzungumza na mimi kwa sauti ya chini, akaniambia Shamila yuko ndani na amewekwa chini ya ulinzi, amejaribu kumtorosha lakini ameshindwa peke yake, akaniomba tukaunganishe nguvu ili tumtoe haraka iwezekanavyo.
“Sasa tutafanyaje” nilimuuliza huku hofu ikianza kuniingia kwani kwa mbali niliwaona askari wengine wawili wenye silaha wakija, akaniambia tukiingia niwe namfuatisha kila anachokifanya, nikatingisha kichwa kuonesha kukubaliana naye. Akaniminya mkono na kunitazama usoni, akaniambia natakiwa niishinde hofu ndani ya moyo wangu. Nadhani aliniona jinsi nilivyoanza kuingiwa na wasiwasi, nikatingisha tena kichwa.
Pale kwenye geti la kuingilia, alinionesha ishara kwamba tunatakiwa kuingia kinyumenyume, tukafanya hivyo na muda mfupi baadaye tayari tulikuwa ndani. Madaktari na manesi walikuwa tayari wameshakaa kwenye nafasi zao huku wengine wakiendelea kuingia.
Mbele kabisa kulikuwa na meza kuu ambako walikuwa wamekaa watu walioonesha kuwa viongozi wa juu wa hospitali hiyo pamoja na askari aliyekuwa na nyota nyingi mabegani, nadhani alikuwa ni kiongozi wa polisi.
Upande wa kushoto, alikuwa amekaa Shamila huku amezungukwa na askari wawili wa kike, mmoja kila upande. Pembeni kidogo, walikuwa wamekaa wale walinzi tuliowapita getini usiku wakati tukitoroka, ambao nao ilionesha wamewekwa chini ya ulinzi. Tulipita mpaka mbele kabisa huku mtu yeyote akiwa hatuoni.
Akanipa ishara kwamba tunatakiwa kuwazunguka wale askari waliokuwa wamemuweka chini ya ulinzi Shamila mara saba kwa uelekeo tofauti, yaani mimi nianzie kulia kwenda kushoto na yeye kushoto kwenda kulia.
Tulianza kufanya kazi hiyo huku kukiwa hakuna mtu yeyote aliyekuwa akielewa kinachoendelea. Tulizunguka mzunguko wa kwanza, wa pili na hatimaye mizunguko saba ilitimia, akanionesha ishara kwamba inatakiwa tuwaguse vichwani wale askari, kweli tulifanya hivyo.
Katika hali ambayo sikuitegemea, nilishangaa kuwaona wale askari wawili wa kike, wote wakishikwa na usingizi wa ghafla, Shamila naye akawageukia mmoja baada ya mwingine, akashangaa akiwa haelewi chochote kinachoendelea.
Wakati hayo yakiendelea, pale meza kuu daktari mmoja alikuwa akizungumza kwa kutumia kipaza sauti, akielezea jinsi tukio la kutoroshwa wagonjwa wawili lilivyofanyika usiku.
Hatukuwa na muda wa kupoteza, alionesha ishara kwamba tukamshike Shamila, mmoja kwenye bega la kushoto na mwingine bega la kulia, tukafanya hivyo kisha akanionesha ishara kwamba akihesabu mpaka tatu, tupige mguu wa kushoto chini kwa nguvu na kufumba macho na nisifumbue mpaka atakaponiambia.
Akaanza kuhesabu, moja! Mbili! Taaatu, nikakanyaga mguu wangu wa kushoto chini kwa nguvu, sawasawa na yeye, mara umeme ukakatika jengo zima, nikafumba macho kama alivyoniambia huku nikiwa nimemshikilia Shamila kwa nguvu, nikahisi kama tumezolewa na kimbunga chenye nguvu kubwa.
“Fumbua macho,” alisema, nilipofumbua macho, sikuamini nilichokiona. Tulikuwa tumerejea ndani ya kile chumba tulichokuwemo mwanzo lakini tofauti na awali, safari hii kila mmoja alikuwa amelala sakafuni, kuanzia mimi, yule mwanamke, Raya na Firyaal huku akiwa ameongezeka mtu mwingine kati yetu, Shamila.
Bado wale wenzetu wote walikuwa kama wamepitiwa na usingizi mzito isipokuwa mimi na yule mwanamke pekee, nikajivutavuta na kuinuka pale nilipokuwa nimelala, nikashangaa mwili wangu ukiwa umechoka kupita kiasi huku viungo vyote vikiniuma.
Yule mwanamke naye aliinuka na kukaa kwa kujiegemeza ukutani, naye akionesha kuchoka kuliko kawaida.
“Kweli wewe ni mwanaume wa shoka, njoo nikupongeze,” alisema kwa sauti ya kichovu, nikajikokota na kusimama, nikasogea mpaka pale alipokuwa amekaa, akanionesha ishara kwamba nikae chini pembeni yake, nikafanya hivyo huku sote macho yetu yakiwa kwa Shamila.
“Sikuwahi kudhani kwamba unaweza kuwa na nguvu kubwa kiasi hicho, hongera sana, utanifaa sana wewe,” alisema huku akipitisha mkono wake mmoja begani kwangu kichovu kisha akanigeukia, tukawa tunatazamana. Katika hali ambayo sikuitegemea hata kidogo, nilishangaa yule mwanamke akinibusu, tena mdomoni, nikashtuka mno.
“Hongera sana, ila inabidi upunguze mambo ya wanawake, utakuwa na nguvu zaidi ya hizi ulizonazo,” aliniambia huku akinitazama usoni.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 51
ILIPOISHIA:
“Sikuwahi kudhani kwamba unaweza kuwa na nguvu kubwa kiasi hicho, hongera sana, utanifaa sana wewe,” alisema huku akipitisha mkono wake mmoja begani kwangu kichovu kisha akanigeukia, tukawa tunatazamana. Katika hali ambayo sikuitegemea hata kidogo, nilishangaa yule mwanamke akinibusu, tena mdomoni, nikashtuka mno.
“Hongera sana, ila inabidi upunguze mambo ya wanawake, utakuwa na nguvu zaidi ya hizi ulizonazo,” aliniambia huku akinitazama usoni.
SASA ENDELEA...

“Sijakuelewa,” nilimwambia, akashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri pale juu ya zulia. Bado si Raya, Shamila wala Firyaal waliokuwa wamezinduka.
“Utanielewa tu,” inabidi kwanza tukaoge kuondoa uchovu halafu tuwasaidie na hawa nao warudi kwenye hali yao ya kawaida, tuna kazi nyingine ya kumsaidia Shenaiza, ni lazima arudiwe na fahamu zake, tena ikiwezekana haraka iwezekanavyo,” alisema mwanamke huyo kisha akapiga miayo mfululizo na kujinyoosha.
“Kwa kawaida, kila binadamu huwa anazalisha nguvu, nadhani hilo nilishakueleza kutoka mwanzo ingawa ni wachache sana wanaolitambua hili.
“Yaani ni kama kupepesa kope, unajua ni mpaka mtu akukumbushe kwamba muda wote macho yako yanapepesa kope ndiyo unakumbuka?” alisema, nikawa sioni chochote kipya kwenye mazungumzo yake kwa sababu ni jambo ambalo nilikuwa nimeshalisikia sana maishani mwangu kwamba kila binadamu anazalisha nguvu zisizoonekana.
“Nguvu tunazozalisha huwa zinatengeneza kitu kinachoitwa aura ambacho wengine huwa wanakiita ni mwili usioonekana juu ya mwili unaoonekana. Sasa kwa mtu mwenye utambuzi wa nguvu hizi, anao uwezo wa kuuona mwili huu.
“Kwa mtu ambaye anaishi maisha ya kitakatifu, yaani hanywi pombe, havuti sigara, hafanyi zinaa, hawasemi vibaya watu wengine, hana wivu wala kinyongo, ana upendo wa dhati kwa watu wote na ambaye moyo wake uko safi, hii aura huwa na kawaida ya kung’aa sana. Mtu akikutazama tu anaiona nguvu inayokuzunguka.
“Lakini vilevile kama mtu anaishi maisha ya hovyo, pengine ni mlevi sana, anafanya ngono hovyohovyo, ana wivu, hasira, vinyongo na tabia mbayambaya, kwa kawaida huwa aura yake inafifia sana na kama una utambuzi wa nguvu hizi, ukimtazama tu unamjua ndiyo maana nilikwambia vile,” alisema yule mwanamke na kuzidi kunishangaza.
Kitu alichokisema sikuwa nimewahi kukisikia sehemu yoyote, nikabaki nimepigwa na butwaa, akaendelea:
“Japokuwa watu wengi huwa hawaelewi kuhusu aura kwa hiyo hawajui umuhimu wa kuishi kitakatifu hata kama huna dini, siyo kitu cha mchezomchezo. Aura ya mtu huanza kuishi kabla mtu hajazaliwa na huendelea pia mpaka mtu anapokufa. Ndiyo maana mtoto anapokaribia kuzaliwa, tafiti zinaonesha kwamba huwa ana uwezo wa kuelewa kinachoendelea kwenye ulimwengu wa nje.
“Hii ni kwa sababu tayari mwili wake ambao hauonekani unakuwa umeshaingia kwenye ulimwengu wa kawaida. Akishazaliwa, huwa inatakiwa mwili wake halisi uungane na hii aura na hiyo hufanyika katika kipindi cha siku arobaini tangu mtoto azaliwe ndiyo maana kuna tamaduni nyingi kwamba mtoto anatakiwa kuanza kutolewa nje baada ya siku arobaini kwani pale inakuwa tayari aura yake na mwili halisi vinakuwa vimeungana hivyo anakuwa na kinga dhidi ya mambo mabaya yasiyoonekana kwenye ulimwengu wa kaiwada.
“Hiyo pia hutokea pale mtu anapokufa ambapo nafsi inapotengana na mwili, aura huwa inaendelea kuishi mpaka baada ya siku arobaini ndiyo nayo hutoweka, ndiyo maana pia huwa kuna tamaduni za kufanya arobaini ya marehemu kwani pale ndiyo uhai huwa unakuwa umefikia mwisho.”
Maelezo hayo yalinifanya nikune kichwa kwani siyo siri yalikuwa yamenichanganya sana akili. Ni mambo ambayo sikuwahi kuyasikia kabla lakini kwa jinsi alivyokuwa akiyafafanua, ilionesha dhahiri kwamba ni kweli. Hata mimi sikuwahi kupata jibu la kwa nini mtoto anatakiwa atolewe nje baada ya siku arobaini tangu azaliwe na kwa nini mtu akifa, msiba huwa unahitimishwa baada ya siku arobaini.
“Lakini mamdogo...”
“Usiniite mamdogo, ningependa zaidi uniite kwa jina langu halisi ambalo ni watu wachache huwa wanalijua. Nina majina mengi lakini jina langu halisi ni Junaitha,” alisema huku akiinuka pale alipokuwa amekaa.
“Hakuna cha lakini... punguza wanawake ili aura yako ing’ae na kukuongezea nguvu, mimi sijui nina mwaka wa ngapi simjui mwanaume,” alisema huku tayari akiwa amesimama, akanipa mkono kama ishara ya kutaka anisaidie kuinuka.
Nilibaki kumtazama tu usoni, mambo mengi yalikuwa yakipita ndani ya kichwa changu.
“Mbona unanitumbulia macho? Amka twende ukaoge, bado kuna kazi kubwa leo,” alisema yule mwanamke, nikampa mkono, akanishika na kunivuta kidogo, nikasimama.
“Halafu inatakiwa pia uwe makini na vyakula unavyokula, inaonesha mwili wako hauna uzito unaotakiwa, hata hao wanawake unaotembea nao hovyo huwa unawaridhisha kweli? Wanaume wa siku hizi wana tatizo kubwa la upungufu wa nguvu za kiume, na wewe usije kuwa miongoni mwao,” alisema huku akitabasamu.
Japokuwa mwenyewe alichukulia kama masihara lakini kwa hulka za kiume, niliona kama amenidharau sana. Maneno yake ni kama yalikuwa yakihitaji nifanye kitu fulani kumthibitishia kwamba sikuwa mtu wa mchezomchezo bali mwanaume niliyekamilika.
Nilipounganisha na tukio la yeye kunibusu kwenye midomo yangu wakati akinipongeza, akili nyingine zilianza kupita ndani ya kichwa changu.
“Kwa hiyo unaishije bila mume?”
“Kwani wewe unapata faida gani kubadilishabadilisha wanawake?” aliniuliza swali juu ya swali ambalo lilinifanya nijiulize sana kwa nini alikuwa akinikomalia kuhusu suala la mimi kuwa na wanawake wengi. Elimu aliyonipa ilikuwa imetosha kunifanya nijitambue lakini kwa nini alikuwa akiendelea kuulizauliza kuhusu mimi kuwa na wanawake? Sikupata majibu.
“Mbona unakuwa mkali sana kwangu Junaitha? Au kuna kitu nimekuudhi?”
“Ndiyo umeniudhi, kwa nini kijana mtanashati kama wewe usitafute mwanamke mmoja tu anayejitambua ukatulia naye?” nilijikuta nikishindwa kujizuia, nikaangua kicheko kwani tayari nilishaanza kupata picha ya kilichokuwa kikiendelea ndani ya kichwa chake.
“Kwa hiyo unanidharau si ndiyo? Yaani mi naongea mambo ya maana wewe unacheka,” alisema, akatoka na kuniacha nimesimama palepale, nikiwaangalia wale waliokuwa wamelala juu ya zulia, kila mmoja akiwa hajitambui kwa uchovu.
“Hebu njoo huku,” nilisikia sauti ya Junaitha ikitokea chumbani kwake, harakaharaka nikatoka pale na kuelekea kule sauti ilikokuwa inatokea.
“Ingia tu mlango upo wazi,” alisema, nikageuka huku na kule kwanza kwa sababu sikuona kama ni heshima kwa mtoto wa kiume kuingia chumbani kwake, hasa ukizingatia ukweli kwamba alikuwa amenizidi sana umri. Nikapiga moyo konde na kuingia ndani ya chumba hicho cha kisasa kilichokuwa na vitu vingi vya thamani.
“Chukua taulo pale kabatini ingia bafuni ukaoge,” alisema akiwa amekaa juu ya kitanda kikubwa cha kisasa akihangaika kufungua zipu ya gauni alilokuwa amevaa, nikaelekea pale kwenye kabati aliponielekeza, nikachukua taulo na kuanza kuelekea kwenye lile bafu la ndani kwa ndani kule chumbani kwake.
Nililazimika kuingia na nguo zote bafuni kwani nilikuwa naona aibu kuvua hata shati mbele ya macho yake.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
d4d9d786fd041742ef85fdae0bbe993e.jpg
 
‹The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 53
ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA...

Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.
“Najua unampenda binti yangu Togo, lakini nakuomba sana mwanangu, ukifanya naye mapenzi tutampoteza, yeye si miongoni mwa jamii yetu na mwili wake hauna kinga yoyote, hebu zingatia sana ninachokwambia, nakuomba usimguse,” baba yake Rahma alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkubwa.
Tofauti na baba ambaye kila akiongea alikuwa akifokafoka, baba Rahma alikuwa akizungumza kwa utaratibu sana na nikajikuta nikimuelewa sana.
Jambo ambalo nilishindwa kulikataa ndani ya moyo wangu ni kwamba nilikuwa nikimpenda sana Rahma kwa hiyo akili za harakaharaka zilianza kunituma kufikiria namna ninavyoweza kukivuka kikwazo kilichokuwepo kati yetu kwani kiukweli sikuwa tayari kumpoteza.
“Kwa hiyo na yeye akiwa miongoni mwetu tutaruhusiwa kuoana?” niliuliza swali ambalo liliwafanya baba na baba Rahma watazamane kwa sekunde kadhaa.
“Lakini si unajua kwamba mwenzako anasoma na siku chache zilizopita mama yake alikuwa akifuatilia mambo ya chuo?”
“Hata akimaliza hakuna shida,” nilijibu huku nikiwa na wasiwasi na atakachokisema baba.
“Wewe mtoto mpumbavu sana, yaani umeshupalia kabisa, ina maana hujui kama nyie mmeshakuwa ndugu? Halafu hiyo michezo ya mapenzi umeianza lini wakati wewe bado mdogo?”
“Lakini baba mimi nampenda Rahma.”
“Unampenda? Unajua maana ya kupenda wewe? Toka lini wewe ukampenda mtu? Hebu toa wendawazimu wako hapa, yaani badala uelekeze nguvu kwenye ulimwengu mpya tuliokufunulia unaanza mambo yako ya mapenzi hapa, una akili wewe?” baba alinifokea.
“Hapana, huna haja ya kuwa mkali mzee mwenzangu,” baba yake Rahma alimkatisha baba kisha akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa.
“Unampenda kwa kiasi gani?”
“Nampenda sana baba.”
“Lakini nyie mmeshakuwa ndugu?”
“Mbona undugu wetu siyo wa damu?”
“Kama kweli unampenda, nakuomba uzingatie nilichokwambia, hayo mengine tuachieni sisi wazazi wenu,” baba yake Rahma alisema kwa upole. Ilihitaji ujasiri mkubwa kuzungumza mambo yale mbele ya baba lakini kwa kuwa baba Rahma alikuwa mwelewa, na mimi nilijikuta nikipata nguvu.
Majibu aliyonipa, yaliufanya moyo wangu ufurahi sana, nikajiapiza kwamba sitakutana naye tena kimwili kwa kuhofia kumpoteza lakini nikawa nafikiria mbinu nyingine mbadala na harakaharaka akili zangu zilinituma kutafuta muda wa kutosha wa kukaa na Rahma na kumweleza ukweli kuhusu mimi, baba na baba yake na mwisho nimshawishi na yeye ajiunge kwenye jamii yetu.
Tayari nilishaanza kuona dalili za ushindi, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu, hisia tamu zikawa zinapita kwenye mishipa yangu huku nikivuta picha ya miaka kadhaa baadaye, nikiishi na Rahma kama mume na mke halali.
“Kilichotuleta hapa siyo hiki tulichokuwa tunakizungumza,” baba yake Rahma alivunja ukimya, baba akawa anatingisha kichwa kukubaliana naye huku akiwa amenitolea macho ya ukali.
“Leo umefanya kitu cha ajabu sana na kama isingekuwa nguvu za ziada kutumika, ungeweza hata kuuawa kule Mlandizi, kama hiyo haitoshi umesababisha majanga mengine ambayo hayakuwepo kwenye ratiba, umesababisha yule dereva wa bodaboda amepoteza maisha,” alisema baba yake Rahma, kauli ambayo ilinishtua kuliko kawaida.
Kilichonishtua zaidi ni kusikia kwamba yule dereva wa bodaboda amekufa, moyo ulishtuka kuliko kawaida.
“Kibaya zaidi umesababisha watu hapa mtaani waanze kututilia mashaka, kwa nini umeenda kumroga huyo kijana dereva wa Bajaj hapo nje? Hujui kama ni hatari sana watu kujua kama unajishughulisha na haya mambo ya giza? Mtoto mpumbavu sana wewe,” baba aliongezea kwa ukali, nikajiinamia kwani kiukweli nilikuwa nimefanya makosa makubwa.
“Lakini nilikuwa nataka kujifunza,” nilijibu kwa sauti ya chini, baba yake Rahma akaniambia kwamba mambo hayo huwa hujifunzi kama unavyojifunza mambo mengine, bali kuna utaratibu wake.
Akaniambia kwamba nilichokifanya kilikuwa makosa makubwa kwa watu wa jamii yetu na kama zilivyo sheria, yeyote anayeenda kinyume lazima akumbane na rungu la Mkuu. Kauli hiyo ilizidi kunitisha moyoni mwangu, nikajaribu kuvuta taswira ya Mkuu, yule kiongozi wa watu wa jamii yetu, hofu ikazidi kunijaa.
“Ili kumfurahisha, inabidi usiku wa leo ufanye juu chini nyama zipatikane, tukifika tutaenda kukuombea msamaha na kwa kuwa utakuwa na mzigo, bila shaka atakupa adhabu ndogo, kinyume na hapo anaweza hata kuamuru uliwe nyama ukiwa hai,” alisema baba yake Rahma, nikajikuta nikitokwa na kijasho chembamba.
Baba Rahma aliniona hali niliyokuwa nayo, akaniambia nisijali watanisaidia lakini kitu cha kwanza, ilikuwa ni lazima nikatoe sadaka ya kitu ninachokipenda zaidi, nje ya familia yangu.
Sikumuelewa kauli yake hiyo, akanifafanulia kwamba wanaposema kitu, kwenye imani yao wanamaanisha mtu kwa hiyo ilikuwa ni lazima nimfikirie rafiki yangu ninayempenda zaidi ambaye ndiye angetolewa kafara usiku ili mimi nisamehewe na Mkuu kwa kitendo changu cha kwenda kwenye msiba wa mtu ambaye tumemla nyama na mimi ndiye niliyesababisha kifo chake.
“Mimi sina rafiki hapa mjini, kwanza sijazoeana na mtu yeyote,” nilijitetea, baba akaniambia kwamba anawajua marafiki zangu wengi tu Chunya.
“Sasa nitaendaje Chunya?”
“Hutakiwi kuhoji kwa sababu hakuna kisichowezekana, unachotakiwa ni kututajia mtu, vinginevyo wewe ndiyo utaaliwa leo,” baba alisema, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi huwa na kawaida ya kuwatoa kafara watu wao wa karibu na ndiyo maana watu wakishajua kwamba wewe ni mchawi wanajitenga na kukuogopa sana lakini nilikuwa naona kama ni hadithi za kufikirika tu, lakini sasa yalikuwa yamenifika.
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Sakayo leo zimewekwa nimewahii siti ya mbeleee
The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 54
ILIPOISHIA:
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
SASA ENDELEA...

“Lakini baba...”
“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.
Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.
“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.
Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.
Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.
Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.
Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.
Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.
Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.
Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.
“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.
“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.
“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.
Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.
Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.
“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.
Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.
“Umeshajiandaa?”
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.
“Haya nifuate.”
“Lakini bado sijala.”
“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.
Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.
Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!
Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.
Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.
Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.
Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.
Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.
“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.
“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Sakayo story tamu jitahidi usome
 
‹The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 53
ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA...

Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.
“Najua unampenda binti yangu Togo, lakini nakuomba sana mwanangu, ukifanya naye mapenzi tutampoteza, yeye si miongoni mwa jamii yetu na mwili wake hauna kinga yoyote, hebu zingatia sana ninachokwambia, nakuomba usimguse,” baba yake Rahma alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkubwa.
Tofauti na baba ambaye kila akiongea alikuwa akifokafoka, baba Rahma alikuwa akizungumza kwa utaratibu sana na nikajikuta nikimuelewa sana.
Jambo ambalo nilishindwa kulikataa ndani ya moyo wangu ni kwamba nilikuwa nikimpenda sana Rahma kwa hiyo akili za harakaharaka zilianza kunituma kufikiria namna ninavyoweza kukivuka kikwazo kilichokuwepo kati yetu kwani kiukweli sikuwa tayari kumpoteza.
“Kwa hiyo na yeye akiwa miongoni mwetu tutaruhusiwa kuoana?” niliuliza swali ambalo liliwafanya baba na baba Rahma watazamane kwa sekunde kadhaa.
“Lakini si unajua kwamba mwenzako anasoma na siku chache zilizopita mama yake alikuwa akifuatilia mambo ya chuo?”
“Hata akimaliza hakuna shida,” nilijibu huku nikiwa na wasiwasi na atakachokisema baba.
“Wewe mtoto mpumbavu sana, yaani umeshupalia kabisa, ina maana hujui kama nyie mmeshakuwa ndugu? Halafu hiyo michezo ya mapenzi umeianza lini wakati wewe bado mdogo?”
“Lakini baba mimi nampenda Rahma.”
“Unampenda? Unajua maana ya kupenda wewe? Toka lini wewe ukampenda mtu? Hebu toa wendawazimu wako hapa, yaani badala uelekeze nguvu kwenye ulimwengu mpya tuliokufunulia unaanza mambo yako ya mapenzi hapa, una akili wewe?” baba alinifokea.
“Hapana, huna haja ya kuwa mkali mzee mwenzangu,” baba yake Rahma alimkatisha baba kisha akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa.
“Unampenda kwa kiasi gani?”
“Nampenda sana baba.”
“Lakini nyie mmeshakuwa ndugu?”
“Mbona undugu wetu siyo wa damu?”
“Kama kweli unampenda, nakuomba uzingatie nilichokwambia, hayo mengine tuachieni sisi wazazi wenu,” baba yake Rahma alisema kwa upole. Ilihitaji ujasiri mkubwa kuzungumza mambo yale mbele ya baba lakini kwa kuwa baba Rahma alikuwa mwelewa, na mimi nilijikuta nikipata nguvu.
Majibu aliyonipa, yaliufanya moyo wangu ufurahi sana, nikajiapiza kwamba sitakutana naye tena kimwili kwa kuhofia kumpoteza lakini nikawa nafikiria mbinu nyingine mbadala na harakaharaka akili zangu zilinituma kutafuta muda wa kutosha wa kukaa na Rahma na kumweleza ukweli kuhusu mimi, baba na baba yake na mwisho nimshawishi na yeye ajiunge kwenye jamii yetu.
Tayari nilishaanza kuona dalili za ushindi, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu, hisia tamu zikawa zinapita kwenye mishipa yangu huku nikivuta picha ya miaka kadhaa baadaye, nikiishi na Rahma kama mume na mke halali.
“Kilichotuleta hapa siyo hiki tulichokuwa tunakizungumza,” baba yake Rahma alivunja ukimya, baba akawa anatingisha kichwa kukubaliana naye huku akiwa amenitolea macho ya ukali.
“Leo umefanya kitu cha ajabu sana na kama isingekuwa nguvu za ziada kutumika, ungeweza hata kuuawa kule Mlandizi, kama hiyo haitoshi umesababisha majanga mengine ambayo hayakuwepo kwenye ratiba, umesababisha yule dereva wa bodaboda amepoteza maisha,” alisema baba yake Rahma, kauli ambayo ilinishtua kuliko kawaida.
Kilichonishtua zaidi ni kusikia kwamba yule dereva wa bodaboda amekufa, moyo ulishtuka kuliko kawaida.
“Kibaya zaidi umesababisha watu hapa mtaani waanze kututilia mashaka, kwa nini umeenda kumroga huyo kijana dereva wa Bajaj hapo nje? Hujui kama ni hatari sana watu kujua kama unajishughulisha na haya mambo ya giza? Mtoto mpumbavu sana wewe,” baba aliongezea kwa ukali, nikajiinamia kwani kiukweli nilikuwa nimefanya makosa makubwa.
“Lakini nilikuwa nataka kujifunza,” nilijibu kwa sauti ya chini, baba yake Rahma akaniambia kwamba mambo hayo huwa hujifunzi kama unavyojifunza mambo mengine, bali kuna utaratibu wake.
Akaniambia kwamba nilichokifanya kilikuwa makosa makubwa kwa watu wa jamii yetu na kama zilivyo sheria, yeyote anayeenda kinyume lazima akumbane na rungu la Mkuu. Kauli hiyo ilizidi kunitisha moyoni mwangu, nikajaribu kuvuta taswira ya Mkuu, yule kiongozi wa watu wa jamii yetu, hofu ikazidi kunijaa.
“Ili kumfurahisha, inabidi usiku wa leo ufanye juu chini nyama zipatikane, tukifika tutaenda kukuombea msamaha na kwa kuwa utakuwa na mzigo, bila shaka atakupa adhabu ndogo, kinyume na hapo anaweza hata kuamuru uliwe nyama ukiwa hai,” alisema baba yake Rahma, nikajikuta nikitokwa na kijasho chembamba.
Baba Rahma aliniona hali niliyokuwa nayo, akaniambia nisijali watanisaidia lakini kitu cha kwanza, ilikuwa ni lazima nikatoe sadaka ya kitu ninachokipenda zaidi, nje ya familia yangu.
Sikumuelewa kauli yake hiyo, akanifafanulia kwamba wanaposema kitu, kwenye imani yao wanamaanisha mtu kwa hiyo ilikuwa ni lazima nimfikirie rafiki yangu ninayempenda zaidi ambaye ndiye angetolewa kafara usiku ili mimi nisamehewe na Mkuu kwa kitendo changu cha kwenda kwenye msiba wa mtu ambaye tumemla nyama na mimi ndiye niliyesababisha kifo chake.
“Mimi sina rafiki hapa mjini, kwanza sijazoeana na mtu yeyote,” nilijitetea, baba akaniambia kwamba anawajua marafiki zangu wengi tu Chunya.
“Sasa nitaendaje Chunya?”
“Hutakiwi kuhoji kwa sababu hakuna kisichowezekana, unachotakiwa ni kututajia mtu, vinginevyo wewe ndiyo utaaliwa leo,” baba alisema, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi huwa na kawaida ya kuwatoa kafara watu wao wa karibu na ndiyo maana watu wakishajua kwamba wewe ni mchawi wanajitenga na kukuogopa sana lakini nilikuwa naona kama ni hadithi za kufikirika tu, lakini sasa yalikuwa yamenifika.
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
..ujue haipendezi kuquote story kama hii, natest mitambo ya kuqoute
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom