Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Jamaan uchochezi wangu ni upi hapoJiangalie! Uchochezi huo! Serikali imepiga marufuku tabia ya kuchochea wananchi ili waje chuki!
Jamaan uchochezi wangu ni upi hapoJiangalie! Uchochezi huo! Serikali imepiga marufuku tabia ya kuchochea wananchi ili waje chuki!
Ebu nitumie kabisa zile heinken kwa tigo pesa jamaan
Sakayo leo zimewekwa nimewahii siti ya mbeleee‹The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 53
ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA...
Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.
“Najua unampenda binti yangu Togo, lakini nakuomba sana mwanangu, ukifanya naye mapenzi tutampoteza, yeye si miongoni mwa jamii yetu na mwili wake hauna kinga yoyote, hebu zingatia sana ninachokwambia, nakuomba usimguse,” baba yake Rahma alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkubwa.
Tofauti na baba ambaye kila akiongea alikuwa akifokafoka, baba Rahma alikuwa akizungumza kwa utaratibu sana na nikajikuta nikimuelewa sana.
Jambo ambalo nilishindwa kulikataa ndani ya moyo wangu ni kwamba nilikuwa nikimpenda sana Rahma kwa hiyo akili za harakaharaka zilianza kunituma kufikiria namna ninavyoweza kukivuka kikwazo kilichokuwepo kati yetu kwani kiukweli sikuwa tayari kumpoteza.
“Kwa hiyo na yeye akiwa miongoni mwetu tutaruhusiwa kuoana?” niliuliza swali ambalo liliwafanya baba na baba Rahma watazamane kwa sekunde kadhaa.
“Lakini si unajua kwamba mwenzako anasoma na siku chache zilizopita mama yake alikuwa akifuatilia mambo ya chuo?”
“Hata akimaliza hakuna shida,” nilijibu huku nikiwa na wasiwasi na atakachokisema baba.
“Wewe mtoto mpumbavu sana, yaani umeshupalia kabisa, ina maana hujui kama nyie mmeshakuwa ndugu? Halafu hiyo michezo ya mapenzi umeianza lini wakati wewe bado mdogo?”
“Lakini baba mimi nampenda Rahma.”
“Unampenda? Unajua maana ya kupenda wewe? Toka lini wewe ukampenda mtu? Hebu toa wendawazimu wako hapa, yaani badala uelekeze nguvu kwenye ulimwengu mpya tuliokufunulia unaanza mambo yako ya mapenzi hapa, una akili wewe?” baba alinifokea.
“Hapana, huna haja ya kuwa mkali mzee mwenzangu,” baba yake Rahma alimkatisha baba kisha akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa.
“Unampenda kwa kiasi gani?”
“Nampenda sana baba.”
“Lakini nyie mmeshakuwa ndugu?”
“Mbona undugu wetu siyo wa damu?”
“Kama kweli unampenda, nakuomba uzingatie nilichokwambia, hayo mengine tuachieni sisi wazazi wenu,” baba yake Rahma alisema kwa upole. Ilihitaji ujasiri mkubwa kuzungumza mambo yale mbele ya baba lakini kwa kuwa baba Rahma alikuwa mwelewa, na mimi nilijikuta nikipata nguvu.
Majibu aliyonipa, yaliufanya moyo wangu ufurahi sana, nikajiapiza kwamba sitakutana naye tena kimwili kwa kuhofia kumpoteza lakini nikawa nafikiria mbinu nyingine mbadala na harakaharaka akili zangu zilinituma kutafuta muda wa kutosha wa kukaa na Rahma na kumweleza ukweli kuhusu mimi, baba na baba yake na mwisho nimshawishi na yeye ajiunge kwenye jamii yetu.
Tayari nilishaanza kuona dalili za ushindi, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu, hisia tamu zikawa zinapita kwenye mishipa yangu huku nikivuta picha ya miaka kadhaa baadaye, nikiishi na Rahma kama mume na mke halali.
“Kilichotuleta hapa siyo hiki tulichokuwa tunakizungumza,” baba yake Rahma alivunja ukimya, baba akawa anatingisha kichwa kukubaliana naye huku akiwa amenitolea macho ya ukali.
“Leo umefanya kitu cha ajabu sana na kama isingekuwa nguvu za ziada kutumika, ungeweza hata kuuawa kule Mlandizi, kama hiyo haitoshi umesababisha majanga mengine ambayo hayakuwepo kwenye ratiba, umesababisha yule dereva wa bodaboda amepoteza maisha,” alisema baba yake Rahma, kauli ambayo ilinishtua kuliko kawaida.
Kilichonishtua zaidi ni kusikia kwamba yule dereva wa bodaboda amekufa, moyo ulishtuka kuliko kawaida.
“Kibaya zaidi umesababisha watu hapa mtaani waanze kututilia mashaka, kwa nini umeenda kumroga huyo kijana dereva wa Bajaj hapo nje? Hujui kama ni hatari sana watu kujua kama unajishughulisha na haya mambo ya giza? Mtoto mpumbavu sana wewe,” baba aliongezea kwa ukali, nikajiinamia kwani kiukweli nilikuwa nimefanya makosa makubwa.
“Lakini nilikuwa nataka kujifunza,” nilijibu kwa sauti ya chini, baba yake Rahma akaniambia kwamba mambo hayo huwa hujifunzi kama unavyojifunza mambo mengine, bali kuna utaratibu wake.
Akaniambia kwamba nilichokifanya kilikuwa makosa makubwa kwa watu wa jamii yetu na kama zilivyo sheria, yeyote anayeenda kinyume lazima akumbane na rungu la Mkuu. Kauli hiyo ilizidi kunitisha moyoni mwangu, nikajaribu kuvuta taswira ya Mkuu, yule kiongozi wa watu wa jamii yetu, hofu ikazidi kunijaa.
“Ili kumfurahisha, inabidi usiku wa leo ufanye juu chini nyama zipatikane, tukifika tutaenda kukuombea msamaha na kwa kuwa utakuwa na mzigo, bila shaka atakupa adhabu ndogo, kinyume na hapo anaweza hata kuamuru uliwe nyama ukiwa hai,” alisema baba yake Rahma, nikajikuta nikitokwa na kijasho chembamba.
Baba Rahma aliniona hali niliyokuwa nayo, akaniambia nisijali watanisaidia lakini kitu cha kwanza, ilikuwa ni lazima nikatoe sadaka ya kitu ninachokipenda zaidi, nje ya familia yangu.
Sikumuelewa kauli yake hiyo, akanifafanulia kwamba wanaposema kitu, kwenye imani yao wanamaanisha mtu kwa hiyo ilikuwa ni lazima nimfikirie rafiki yangu ninayempenda zaidi ambaye ndiye angetolewa kafara usiku ili mimi nisamehewe na Mkuu kwa kitendo changu cha kwenda kwenye msiba wa mtu ambaye tumemla nyama na mimi ndiye niliyesababisha kifo chake.
“Mimi sina rafiki hapa mjini, kwanza sijazoeana na mtu yeyote,” nilijitetea, baba akaniambia kwamba anawajua marafiki zangu wengi tu Chunya.
“Sasa nitaendaje Chunya?”
“Hutakiwi kuhoji kwa sababu hakuna kisichowezekana, unachotakiwa ni kututajia mtu, vinginevyo wewe ndiyo utaaliwa leo,” baba alisema, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi huwa na kawaida ya kuwatoa kafara watu wao wa karibu na ndiyo maana watu wakishajua kwamba wewe ni mchawi wanajitenga na kukuogopa sana lakini nilikuwa naona kama ni hadithi za kufikirika tu, lakini sasa yalikuwa yamenifika.
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Sakayo story tamu jitahidi usomeThe Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 54
ILIPOISHIA:
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
SASA ENDELEA...
“Lakini baba...”
“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.
Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.
“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.
Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.
Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.
Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.
Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.
Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.
Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.
Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.
“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.
“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.
“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.
Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.
Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.
“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.
Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.
“Umeshajiandaa?”
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.
“Haya nifuate.”
“Lakini bado sijala.”
“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.
Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.
Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!
Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.
Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.
Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.
Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.
Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.
“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.
“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Veep mbona hujaandika kitu
Naamini umeamka salama..ubarikiwe Obe ..mpira uliaje matokeo.
Niliyategemea hayo kwa wazee wa kuquote
Nina hamu na hiyo kitu na inavyotoa jasho acha niitafute tu![]()
Heineken za mtaani kwenu . Leo nipo huku mtaani kwenu.
..ujue haipendezi kuquote story kama hii, natest mitambo ya kuqoute‹The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 53
ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA...
Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.
“Najua unampenda binti yangu Togo, lakini nakuomba sana mwanangu, ukifanya naye mapenzi tutampoteza, yeye si miongoni mwa jamii yetu na mwili wake hauna kinga yoyote, hebu zingatia sana ninachokwambia, nakuomba usimguse,” baba yake Rahma alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkubwa.
Tofauti na baba ambaye kila akiongea alikuwa akifokafoka, baba Rahma alikuwa akizungumza kwa utaratibu sana na nikajikuta nikimuelewa sana.
Jambo ambalo nilishindwa kulikataa ndani ya moyo wangu ni kwamba nilikuwa nikimpenda sana Rahma kwa hiyo akili za harakaharaka zilianza kunituma kufikiria namna ninavyoweza kukivuka kikwazo kilichokuwepo kati yetu kwani kiukweli sikuwa tayari kumpoteza.
“Kwa hiyo na yeye akiwa miongoni mwetu tutaruhusiwa kuoana?” niliuliza swali ambalo liliwafanya baba na baba Rahma watazamane kwa sekunde kadhaa.
“Lakini si unajua kwamba mwenzako anasoma na siku chache zilizopita mama yake alikuwa akifuatilia mambo ya chuo?”
“Hata akimaliza hakuna shida,” nilijibu huku nikiwa na wasiwasi na atakachokisema baba.
“Wewe mtoto mpumbavu sana, yaani umeshupalia kabisa, ina maana hujui kama nyie mmeshakuwa ndugu? Halafu hiyo michezo ya mapenzi umeianza lini wakati wewe bado mdogo?”
“Lakini baba mimi nampenda Rahma.”
“Unampenda? Unajua maana ya kupenda wewe? Toka lini wewe ukampenda mtu? Hebu toa wendawazimu wako hapa, yaani badala uelekeze nguvu kwenye ulimwengu mpya tuliokufunulia unaanza mambo yako ya mapenzi hapa, una akili wewe?” baba alinifokea.
“Hapana, huna haja ya kuwa mkali mzee mwenzangu,” baba yake Rahma alimkatisha baba kisha akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa.
“Unampenda kwa kiasi gani?”
“Nampenda sana baba.”
“Lakini nyie mmeshakuwa ndugu?”
“Mbona undugu wetu siyo wa damu?”
“Kama kweli unampenda, nakuomba uzingatie nilichokwambia, hayo mengine tuachieni sisi wazazi wenu,” baba yake Rahma alisema kwa upole. Ilihitaji ujasiri mkubwa kuzungumza mambo yale mbele ya baba lakini kwa kuwa baba Rahma alikuwa mwelewa, na mimi nilijikuta nikipata nguvu.
Majibu aliyonipa, yaliufanya moyo wangu ufurahi sana, nikajiapiza kwamba sitakutana naye tena kimwili kwa kuhofia kumpoteza lakini nikawa nafikiria mbinu nyingine mbadala na harakaharaka akili zangu zilinituma kutafuta muda wa kutosha wa kukaa na Rahma na kumweleza ukweli kuhusu mimi, baba na baba yake na mwisho nimshawishi na yeye ajiunge kwenye jamii yetu.
Tayari nilishaanza kuona dalili za ushindi, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu, hisia tamu zikawa zinapita kwenye mishipa yangu huku nikivuta picha ya miaka kadhaa baadaye, nikiishi na Rahma kama mume na mke halali.
“Kilichotuleta hapa siyo hiki tulichokuwa tunakizungumza,” baba yake Rahma alivunja ukimya, baba akawa anatingisha kichwa kukubaliana naye huku akiwa amenitolea macho ya ukali.
“Leo umefanya kitu cha ajabu sana na kama isingekuwa nguvu za ziada kutumika, ungeweza hata kuuawa kule Mlandizi, kama hiyo haitoshi umesababisha majanga mengine ambayo hayakuwepo kwenye ratiba, umesababisha yule dereva wa bodaboda amepoteza maisha,” alisema baba yake Rahma, kauli ambayo ilinishtua kuliko kawaida.
Kilichonishtua zaidi ni kusikia kwamba yule dereva wa bodaboda amekufa, moyo ulishtuka kuliko kawaida.
“Kibaya zaidi umesababisha watu hapa mtaani waanze kututilia mashaka, kwa nini umeenda kumroga huyo kijana dereva wa Bajaj hapo nje? Hujui kama ni hatari sana watu kujua kama unajishughulisha na haya mambo ya giza? Mtoto mpumbavu sana wewe,” baba aliongezea kwa ukali, nikajiinamia kwani kiukweli nilikuwa nimefanya makosa makubwa.
“Lakini nilikuwa nataka kujifunza,” nilijibu kwa sauti ya chini, baba yake Rahma akaniambia kwamba mambo hayo huwa hujifunzi kama unavyojifunza mambo mengine, bali kuna utaratibu wake.
Akaniambia kwamba nilichokifanya kilikuwa makosa makubwa kwa watu wa jamii yetu na kama zilivyo sheria, yeyote anayeenda kinyume lazima akumbane na rungu la Mkuu. Kauli hiyo ilizidi kunitisha moyoni mwangu, nikajaribu kuvuta taswira ya Mkuu, yule kiongozi wa watu wa jamii yetu, hofu ikazidi kunijaa.
“Ili kumfurahisha, inabidi usiku wa leo ufanye juu chini nyama zipatikane, tukifika tutaenda kukuombea msamaha na kwa kuwa utakuwa na mzigo, bila shaka atakupa adhabu ndogo, kinyume na hapo anaweza hata kuamuru uliwe nyama ukiwa hai,” alisema baba yake Rahma, nikajikuta nikitokwa na kijasho chembamba.
Baba Rahma aliniona hali niliyokuwa nayo, akaniambia nisijali watanisaidia lakini kitu cha kwanza, ilikuwa ni lazima nikatoe sadaka ya kitu ninachokipenda zaidi, nje ya familia yangu.
Sikumuelewa kauli yake hiyo, akanifafanulia kwamba wanaposema kitu, kwenye imani yao wanamaanisha mtu kwa hiyo ilikuwa ni lazima nimfikirie rafiki yangu ninayempenda zaidi ambaye ndiye angetolewa kafara usiku ili mimi nisamehewe na Mkuu kwa kitendo changu cha kwenda kwenye msiba wa mtu ambaye tumemla nyama na mimi ndiye niliyesababisha kifo chake.
“Mimi sina rafiki hapa mjini, kwanza sijazoeana na mtu yeyote,” nilijitetea, baba akaniambia kwamba anawajua marafiki zangu wengi tu Chunya.
“Sasa nitaendaje Chunya?”
“Hutakiwi kuhoji kwa sababu hakuna kisichowezekana, unachotakiwa ni kututajia mtu, vinginevyo wewe ndiyo utaaliwa leo,” baba alisema, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi huwa na kawaida ya kuwatoa kafara watu wao wa karibu na ndiyo maana watu wakishajua kwamba wewe ni mchawi wanajitenga na kukuogopa sana lakini nilikuwa naona kama ni hadithi za kufikirika tu, lakini sasa yalikuwa yamenifika.
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Ndio mana nakupenda binamu...acha kuqoute anko, hasira zikipanda unajua hakuwekwi kitu humu

halaf kwenye story moja apo jina lao obe kumbe ni kufanya meditation
Endeleeeni mfyuuuu nimekusifia kumbe nawe ni wale wale..ujue haipendezi kuquote story kama hii, natest mitambo ya kuqoute