Muziki: Wikend Ndefu, Jino Moja
..tumemaliza kusheherekea kuzaliwa kwa mtume, tulikuwa hapa Ruangwa na nitalala huku huku vinginevyo nichomoke mdogomdogo nikalale pale Ndanda ila kile kilima cha karibu na kwa Wabenedikitini kinasifika ka kuwa na chui, so bora nijitulize tu hapa nilipo. Sherehe kiufupi ilikuwa nzuri sana, hutba poa na lile jambo linalonifanyaga nisafiri lilikuwa zuri kiasi. Inabidi niseme tu yaani msosi ulikuwa pilau, limekaangwa vizuri sana ila tatizo viazi vilikuwa vingi kuliko nyama.
Unajua furahiday ikiangua siku ya mapumziko ninakuwa na siku tatu za kupumzika, sijui wewe! Kama nilivyosema niko ugenini na nimekaa hapa najiliwaza kwa moja moto moja baridi. Najua wapo mabingwa wa kujudge wenzao, nawakaribisha, ndiyo nimetoka kwenye swala na kisha nimekaa hapa naichangia kodi serikali yangu tena nina hasira za pilau kuwekwa viazi vingi kuliko nyama, sijui mpishi ana makusudi au vyuma no vimekaza maana hata mdalasini na karafuu zilikuwa nyingi hadi unahitaji ubunifu kuupata mchele.
Muziki sasa, wakati nimekaa ili nimjulishe anko ninaendeleaje ugenini, akaamua bila hata salamu kuniataka nidedicate wimbo kwa aunt yangu, sikutaka kumuhoji maana nilisikia sauti pembeni nikajua kabisa sio ya aunt yangu ila ndo nitasema nini tena kwa anko wangu. Nimefurahia kukuona
husna muba mpenzi wangu mwenyewe, ukifukua makaburi ukaona jina langu limehusishwa na BH basi jua kuna watu wana hila mbaya wananiandikisha nisiyotaka kuandika.
Nikutakie wikend njema
shululu ,
Tumosa ,
BlessedHope ,
Nyagei ,
Sakayo ,
Transcend ,
SHIMBA YA BUYENZE ,
ABJ ,
Mndali ndanyelakakomu mzeewakungoa Gentries ,
Lyon Lee ,
Shunie Bailly5 Werrason ,
Mussolin5 ,
mtugani wa wapi huyo ,
Clkey na wewe Kapuku unayesoma kipengele hiki.