Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tanesco washenzi sana, nmeamka nakuta umeme hakuna, napata taarifa ni tanzania ya viwanda yote..
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA KWA WATEJA WALIOUNGWA KATIKA GRIDI YA TAIFA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake kuwa mnamo majira ya Saa moja na dakika mbili asubuhi imetokea hitilafu katika Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha Mikoa yote iliyo unganishwa katika Gridi kukosa umeme.

Jitihada zinaendelea kurejesha umeme kwa haraka na tutaendelea kutoa taarifa zaidi.

Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
www.facebook/tanescoyetultd /twitter.com/tanescoyetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu

30/11/2017
Ndio hivyo wamesema kuna hitilafu kwenye grid ya taifa

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom