MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 27
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
"sheby kumbe ni tajiri, anajifanya kuuza viazi kumbe ni tajiri ana hela"
"we zai muongo wewe... Au katajirika kwa kuuza viazi"
"mi sijui.. Ila nakulaumu wewe umenifundisha kazi yako mpaka nimemkosa"
Aliongea zaituni huku akimnyooshea shadi kidole
"weeee ishia hapo hapo... We ulifikiri mimi na wewe nani kamfundisha mwenzie??"
Aliongea shadi huku akiwa kamshikia zai kiuno... Na wakati huo zai nae anashangaa kuskia kuwa hata yeye hakuwa malaya
"una maana gani kusema hivyo we shadi"
"tena unisikilize kwa makini.... Ulipokuwa malaya wewe mimi nilikuwa sio malaya, wewe ndio umenifanya mimi kuwa malaya"
Zaituni alizidi kushangaa kuskia maneno ya shadi
"we shadi unasemaje"
"sasa skia ukweli mpaka nikakusababishia kiwa malaya... Mimi ndio chanzo lakini nyuma yangu kuna mtu mwingine alionituma kwako"
"ati nini??.... "
"unakumbuka siku ile ulipoanza kuja kule uswahilini ukiwa bado ni kipofu??"
"ndio nakumbuka.... Kwani ilikiwaje"
"sikiliza sasa ukweli mpaka wewe ukaanza umalaya.... Mimi wakati ule shadi mimi sijui mwanaume wala sijui hata kuvaa nguo fupi,... Ila ile siku nilipokuwa nje... Ilikuwa hivi"
Sasa shadi anatoa ukweli juu ya kile kilichofanyika mpaka zai kuwa malaya,.. kumbe umalaya wa zai ulitafutwa, na sio kuwa alijikuta tu bali alikusudiwa, na huu ndio ukweli anaousema shadi....
ENDELEA..........
Katika maisha ya mwanadada shadi yeye hakufikiriga kabisa kama ipo siku atakuja kuuza mwili wake ili aweze kupata kipato cha kujikimu na maisha yake,... Lakini hutoweza kuamini kwamba shadi kajikuta akiingia katika kazi hio kutokana rafiki yake zai kufaidika kwa kupata mwanaume anaejiweza kimaisha.. Unaweza ukashangaa kwanini shadi kawa wapili kujiunga na zai wakati sisi tunajua shadi ndio wa kwanza... Siri nzito iliojificha siku zote lei ndio tunaijua na shadi mwenyewe ndio mropokaji wa siri hio....
kumbe umalaya wa zai ulitafutwa, na sio kuwa alijikuta tu bali alikusudiwa, na huu ndio ukweli anaousema shadi
KAMA UNAKUMBUKA SIKU ILE SHEBY ANAKUJA KUPANGISHA HIKI CHUMBA CHA USWAHILINI NA KUMKUTA SHADI AKIWA FUNDI CHEREHANI.... SASA KAZI ILIANZIA PALE.... NA ILI UELEWE VIZURI TUANZIE HAPA....... SIKU ILEEEE HATUKUJUA WALICHOONGEA AKINA SHASHA....
"karibu ukae kaka"
Yule dada aliongea hivyo ili hata kumshtua kijanja janja, mana anashindwa kumwambia asiangalie nguo yake,..
"Ahsante dada angu"
Sheby alikaa katika makochi yaliochakaa sana, yaani hata vitambaa vyake vimechanika afu yeye ni fundi,.. Mana hawezi kumaliza faida anayopata kwa ajili ya kushona vitambaa vya makochi yake,
"ok ahsante dada yangu.... Aaaahh Samahani sana, nikiwa naendelea kumsubiria baba mwenye nyumba, kuna jambo nataka tuliongee mana umeshakuwa jirani yangu sasa"
Aliongea kijana sheby huku nae akiwa na busara zake, sema busara hupotea pale anapoona nguo za kike,
"sawa tuongee haraka nirudi kazini"
Aliongea dada huyo huku akiwa kweli ana haraka ya kutoka hapo..
"lakini bado hatujajuana hata kwa majina mama"
"mmhhh.. Mimi naitwa Shadya ukipenda niite Shadi"
"waoooo jina lako limeanza kama jina langu vile"
"kwani we jina lako nani"
"mimi naitwa Sharbiny, ni mtoto pekee kwenye familia ya kita... Nooo... Kwenye familia ya kimaskini"
Sheby alitaka kukosea neno akajikuta anataka kuongea eti yeye ni tajiri... Basi shadya alipata kucheka kwa kigugumizi alichokipata sheby wakati wa kujitambulisha kwa Shadi (Shadya)...
"unanicheka si ndio"
"No, unajua nini? Ulitaka kujitambulisha hali za wenzako na wakati hali yako inaonyesha tu ulivyo"
"kwani mi nipoje"
"ulivyomalizia kujitambulisha ndivyo ulivyo, na ndivyo unavyoonekana"
Shadi alimaanisha kwamba sheby alionekana maskini kabisa, lakini weeee heeeee balaa tu, pesa zimelala hapo..
"sasa shadi, kuna kitu cha muhimu sana nahitaji kukuomba,.. Binafsi nahisi utanikubalia ombi langu"
"mmmhh kaka unanitisha, kwani ni ombi gani unalotaka kuniomba"
Maongezi yao hapa ndipo yanapoanza,
MAONGEZI YALIKATISHWA HAPO.. SASA TUYAENDELEZE HAPA CHINI
"nina mchumba wangu aitwae zai nataka kumleta aishi hapa,.. Lakini jirani mzuri atakuwa ni wewe"
Aliongea sheby huku akiwa kakaa bila wasiwasi katika geto la mtoto wa kike,...
"sasa kuna shida gani,.. Mana mimi sio mama mwenye nyumba kana kwamba nitakataa"
"shadi.... Huyo mchumba ni kipofu,.. Kiukweli nampenda sana yaani tena sana, ila nina kapesa changu kidogo ambacho nilitaka kujenga kibanda changu huko mtaa wa chini... Lakini kutokana na hali alionayo mchumba wangu, nimesitisha kujenga ili nimpeleke india akafanyiwe matibabu ya macho"
Aliongea hivyo kijana sheby, wakati huo shadi bado hajaelewa kitu chochote kile
"mpaka hapo mimi sina kizuizi bado... Ila binafsi wewe ni mwanaume pekee ambae ndio kwanza nakuskia umempenda kipofu, Sipati picha mtaishi vipi"
Aliongea shadi huku akichungulia kazi zake pale nje
"enheeee.... Sasa hapo ndipo pazuri... Mchumba wangu huyo nataka nikukabidhi wewe uniseidie kumpikia chakula, kisha utampatia na pesa ya chakula mimi nitatoa, kumuogesha nitamwogesha mwenyewe,.. Nguo nitamvisha mwenyewe, kikubwa tu ninachokuomba ni kumpatia chakula na kumpeleka toilet tu basi na ni kitendo cha wiki moja tu"
Shadi alichoka kwa hio kazi aliokuwa akipewa na kijana sheby, lakini sema shadi alikuwa ni mwanamke mwenye imani ya dini, hivyo kwake alihisi ni mitihani ya Mwenyezi Mungu,.. Shadi alikubali kupika chakula na kumpatia, na kumpeleka toilet...
"kiukweli ni kazi ngumu sana lakini nitamwomba Mwenyezi Mungu anipunguzie mana nayo ni mitihani yake... "
"nashukuru kwa kunielewa shadi.... Sasa nina ombi jingine"
"lipi tena"
"nataka hivi vitu vyako viwe kwake yaani haya makochi yako na kitanda chako viwe huko kwake atumie yeye"
Shadi alishangaa kuskia hivyo
"afu mimi nitalala wapi? Chini au?"
"hapana... Nitanunua vipya utaweka afu hivi vilivyochakaa tuviweke huko kwangu"
"mmmhhhh ivi unampenda mchumba wako kweli... Mana huezi kumuekea vitu vilivyochakaa ndani"
"nina maana yangu na utaijua tu"
"ok kwa hilo pia nimekubali, kwasababu una maana yako... Vipi kuna lingine"
Shadi aliuliza kama kuna ombi lingine ambalo sheby anataka kuomba kutoka kwa shadi...
"ndio ninalo ombi la mwisho kabisa"
Aliongea sheby na kumwacha shadi hoi kwa maombi yake yalivyokuwa mengi,...
"haya sema na hilo... Mana mwishowe utantongoza hapa mi sikuelewi eti"
"kwani we si mwanamke tu, nitashindwaje kufanya hivyo"
"we si una mchumba wako sasa untongoze wa nini tena"
"kwani mchumba haachwi"
"akaaa mi staki umuache mtu kwa ajili yangu"
Shadi kumbe tayari alishaanza kumpenda sheby...
"ok sasa skia... Ombi langu la mwisho ni hili... Baada ya kuona kwake, nataka uanze kumdanganya na mambo ya starehe, ili nijue kama kweli ataridhika na hali yangu au laa, mana nyie wanawake wa siku hizi mnapenda maisha mazuri sana na sijui ni kwanini"
"aahhhh hebu ngoja kwanza... Unasema nimdanganye na mambo ya starehe kama yapi"
"kwanza uwe unavaa vizuri na kumlingishia,... Afu akikuuliza unafanya kazi gani unamwambia nafanya kazi ya kujiuza"
"whaaaat....hapana sheby hio mimi siwezi, siwezi mimi"
"kwani unajiuza kweli??"
"hapana mi siwezi kuvaa nguo za kujiuza"
"sikiliza basi... Nguo unazivaa ukiwa nae lakini ukitoka unazivua au unavalia kanga kwa juu"
"no, no sheby siwezi..... Yaani sasa mimi nianze kumkuadia sasa"
"haswaaaaa... "
"sasa si utakuwa unamuuza mchumba wako"
"hapana.... Kama ana akili mimi ni nani na nilimtoa wapi na anataka awe nani yangu, basi kamwe hawwzi kukubali utakachomwambia... Lakini kama akili yake ni mbaya, atakubali unachomwambia"
"mungu wngu shadi mie, kazi gani unanipa sheby"
"naomba uniseidie shadi... Mimi siwezi kutambua mke wa kuoa, kuliko nioe ndio abadirike bora nimjue mapema"
Aliingea sheby huku akiwa sirias kweli,
"jamani sheby... Ok sasa hizo nguo mie nitatoa wapi"
"ninachukuwa pesa kidogo kwenye mtaji wangu wa viazi, ukanunue nguo zile za kichangudoa zile... Afu nitakuwa nakupa pesa kwa ajili ya kumringishia ringishia,.. Kama ana akili basi hawezi kubali ujinga wako lakini kama hana akili atakubali huo ujinga"
"sasa akisema na yeye anataka mwanaume kama mimi, haya nitampeleka au niamuache"
"mpeleke kwenye mijumba ya starehe huko lazima watamuona, akishakuwa hivyo tu basi huyo sio mke wa kuoa... Kikubwa nataka kujua kuwa ataridhika na hali yangu ya kuuza viazi"
"kazi ngumu sana.... Kazi ngumu sana.. Kwa mtu wa dini kama mimi kufanya hivyo,.. Hata kazi zangu zitakufa sasa"
"nitakulipa elfu 10 kila siku"
"ati unasemaje"
"ndio..."
"lakini mimi hata hayo majumba ya starehe siyajui hata moja"
"nitakuonyesha baadhi ya majengo... Yaani wewe kazi yako ni kumringishia mavazi yako na pesa, akitamani mpeleke afu unijulishe"
Maongezi kati yao yaliishia hapo lakini shadi alishampenda sheby hivyo kwa nafasi aliopewa ya kumringishia zai mavazi na pesa,.. Binafsi yake alisema atajiongeza zaidi
"napenda mwanaume mchapakazi kama wewe,... Natamani unioe mimi.. Na kazi yako nitajiongeza mara dufu ili tu niwe na wewe"
Aliongea shadi baada ya sheby kuondoka zake,....
BAADA YA SIKU MBILI KUPITA
sheby na zaituni walihamia katika nyumba hio, lakini wakati huo zaituni alikuwa bado ni kipofu,.. Kitanda kilichakaa makochi yalikuwa yameisha, na hivyo vitu ni vya shadi,..
BAADA YA WIKI TATU KUPITA,..
Wakiwa wamesharudi india, na zaituni alikuwa anaona vizuri kama zamani,.. Zai alikutana na hali ya mchumba wake kuishi kwenye nyumba ya udongo,... Sasa kazi ya shadi ndipo ilipoanza,.. Mara leo kavaa nguo mpya, mara kesha kaja na pesa, hivyo hivyo ikawa hivyo, nadhani tuliona vituko sema hatukujua tu... Ilifikia mpaka zaituni anatamani ile hali ya shadi kupendeza mara kwa mara bila kujua yeye ndio anategwa ili kujua ni mschana mwenye tamaa au laa.. Shadi na kazi yake alizidi kumdanganya zai,... Zai mwanzoni alikataa lakini mwisho wa siku alijikuta anatamani mavazi na pesa alizonazo,... Kumbe pesa alikuwa akipewa afanye hivyo, saa mingine anampa pesa kabisa ili kumwonjesha radha ya pesa.... Zai alijikuta nae anatamani ile hali, na kitaka kuunganishwa na kazi hio anayoifanya shadi... Kila hatua anayoifanya shadi alikuwa akimtaarifu sheby... Na kama unakumbuka kuna siku sheby aliwakuta njiani shadi na zai wakiwa wamevalia mavazi ya ajabu ajabu, wakati huo sheby akiwa na mkokoteni wake... Shadi alimpigia sheby simu na kumpa taarifa zote, mpaka zai akapata buzi la kumuoa kabisa na kumlipia kodi ya nyumba, uzuri ni kwamba hajajiuza bali alipata mwanaume aliopenda kabisa na kutaka kuweka ndani... Ilifikia mpaka hatua zaituni anahamia kwenye nyumba aliopangishiwa na buzi hilo.. Sheby alipata taarifa ya zai kuhamia nyumba mpya aliopangishiwa,..
Sheby yote hayo alikuwa akiyajua lakini alikuwa anajifanya hajui pale anapokutana na zaituni,.... Sasa baada ya sheby kujua zai keshamuacha, akajikuta kuwa na mawazo mengi sana juu ya zai kupoteza pesa zake nyingi sana afu mwisho wa siku anakuja kuwa na mwanaume mwingine....
"boss vp mbona una mawazo hivyo"
Alikuwa ni saidi aliomkuta boss wake akiwa kajiegemeza kwenye ustelingi wa gari
"we acha tu,... Ivi unaweza kugharamia kitu afu kikawa hasara tupu yani"
Aliongea sheby huku machozi yakimtoka kwa uchungu,...
"nini tena boss,.. Kuna mzigo umepotea"
"bora hata kungepotea mzigo... Kuna demu nimemgharamikia mwili wake lakini huezi amini kaniacha hivi hivi yani"
"aahhhhhh mbona kuna watu wanasomesha mademu zao lakini hawawaoi"
"kweli?"
"aahhhh wengi sana"
Sheby kuskia mbona kuna watu wanasomesha na hawaoni ndani kidogo hapo akapata imani kuwa kumbe hakuwa peke yake....
"aaahhhhh lakini mbona hata shadi ni mwanamke mzuri tu na anafaa kuoa yule"
Sheby alikua akiongea hivyo baada ya kuona zaitini keshakuwa na tamaa ya maisha,...
"kumbe ulikuwa na wengi vuta na huyo"
Saidi alikiwa akisapoti, bila kujua huyo huyo saidi ndio aliomchukuwa zaitini wakati walipokutana matembezi huko mjini kati time za usiku,...
"hawa wanawake hawaaminiki kabisa yani"
"aahhhh mi wangu katuliaaaaa"
"hebu ngoja nimpigie simu tukutane, na huyu staki kumsubirisha kama ni kunijua wacha anijue kuwa mi ni tajiri"
Aliongea hivyo sheby huku akiwa anatafuta namba ya shadi ili ampigie
Tukija huku geto kwa shadi ambako ni uswahilini, maskini kaachwa peke yake, zai keshahama kwenye jumba la maana,... Wakati zai akiwa anasubiria nguo za kushona mawazo yalimpeleka mbali sana
"nyumba ya mwenzangu nzuri, kila nikienda natamani kulala kwa zai... Mimi ndio chanzo cha maisha yake... Kama yeye kaweza mimi nitashindwa vipi....tena kwa bahati nzuri kapata mwanaume wa kumuoa, kwanini mimi nisipate,... Nampenda sana sheby lakini lakini keshanisahau kwasababu kazi yake imeisha.... Hapana, hata mimi ni mwanamke mzuri naweza kupata mwanaume kama mwenzangu zaituni..."
Shadya alikuwa akiongea mwenyewe huku nae akiitafuta namba ya zaituni. Wakati huo na sheby nae keshaipata namba ya shadi anataka ampigie ili amuite mahari wakutane.... Wakati huo na shadi nae keshapata namba ya zai ampigie wakutane ili amuulize kuhusu mwanaume ambae alishawahi kumuulizia...
Kwa bahati mbaya sheby alipopiga aliambiwa simu inatumika,... Sasa shadi alikuwa akiongea na zaituni
"eee shost mambo"
"safi shadi mzima wewe"
"salama tu... Nahisi upo nyumbani ee"
"yes nipo hapa naangalia tv huku nikipata juice baridiii"
Zai alikuwa akizidi kumringishia mwenzie na maisha mazuri, yaani sasa kule kwa shadi kumringishia mwenzie mavazi na pesa, sasa kumemgeukia yeye....
"ok sasa skia zai... Ivi yule kijana aliokuuliza kuhusu mimi vipi? Ivi bado anaendelea kukusumbua tu"
"yaani shadi umeikosa bahati wewe,.. Yule boy alinipigia jana, ila nikamwambia hutaki"
"ooohhh shit, sorry naomba namba yake nimcheki"
"ati nini"
Zai alishtuka kwa kuskia shadi kakubali kuwa na huyo kijana wanaomsemea
"nipe namba zake basi"
"ok poa ngoja nikutumie"
Zaituni aliitafuta namba ya huyo jamaa aliompenda shadi na shadi kukataa,.. Shadi alitumiwa namba ya huyo kijana na kuisevu kabisa,... Sasa akawa anasita kupiga, mana mwanamke kumtongoza mwanaume ni ngumu, sasa wakati huo huku kwa sheby nae akarudia tena kupiga, mana mwanzo aliambiwa kiwa namba aliopiga ilikuwa ikitumika,.. Wakati huo huku kwa shadi nae kabonyeza kitufe cha kupigia kana kwamba kaamua kumpigia huyo boy amwambie keshamkubalia.... Sasa hapo sijui kachelewa au kawahi, mana ikiingia simu ya sheby tu basi kapata bahati, lakini kama kawahi basi simu ya sheby hawezi kuipata tena... Sasa kila mmoja akawa anasikilizia kama itaita au vipi
Je? Itakuwaje ha