MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 19
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
Sasa huku kwa shadi kumbe hata shadi alikuwa akizisikia hizo sauti za akina sheby na zai...
Huezi amini nae alikua akijitomasa katika kifua chake... Sasa swali linakuja hivi, Kama shadi ni malaya, sasa mbona anazishangaa sana na kuzifurahia sauti hizo, kana kwamba hajawahi hata kuzisikia wala kukutana nazo, na wakati yeye ni malaya.... Mi sijui twendeni mbele
Tukirudi huku katika chumba cha akina sheby na zai,.. Sheby alisitisha denda kwanza na kuanza kuongea mambo ya ndoa yao, mana zai ndio kaanza
"we sheby umeamua kuvunja kiapo, lakini sawa tu kwani kuna nini"
Hapo ndipo sheby akasitisha kumnyonya mate mpenzi wake
"aaahhhh nisamehe zai"
"No, mi nipo tayari kama utataka"
"zai... Kuna kitu nataka kukuambia ila sjui kama utakasirika"
"we bwana kama wataka mapenzi ina haja gani uniambie, we nisukumie kitandani nipe vyangu, mi ni mkeo mtarajiwa huna haja ya kusema nataka.. We nivute ule vyako jamani sheby"
"sio hilo"
"nini kwani.... Au umeanza tabia mbaya, mana nyie wanaume wa siku hizi manpenda sana tabia mbaya..."
"tabia gani tena sisi tunaipenda"
"si kurukana hovyo hovyo... Mi naomba hilo lisikupate mme wangu"
"zai.... Mi mwenzio nimeoa"
Zai ana macho makubwa yalimpendeza kutokana na umbo lake, lakini kwa maneno hayo alioyaongea sheby, macho ya zai yamekuwa makubwa zaidi... Mpaka sheby aliogopa huenda yakapasuka..
Lakini sasa kumbe......
ENDELEA.........
Mapenzi ni upofu, mapenzi hayana utani hata kidogo, na pia mapenzi nzi hayana heshima unaweza ukajikuta unapenda bila ya wewe kujijua, unashtukia tu una mpenzi, kupenda kubaya sana tena haswa akipenda mwanamke hua mpaka aje aseme itachukua muda mrefu sana, labda awe malaya, lakini kama ni mtu anaejiheshimu hawezi kumtongoza mwanaume hata siku moja, yeye atabaki kuwa kimya muda wote, akisubiri wewe mwanaume uanze kumsemesha....
Kijana sheby na mpenzi wake zai wakiwa katika ya mahaba mazito, lakini wakati huo kijana huyo alikuwa tayari kumwambia ukweli zai kuwa ameoa,
"zai.... Mi mwenzio nimeoa"
Zai ana macho makubwa yalimpendeza kutokana na umbo lake, lakini kwa maneno hayo alioyaongea sheby, macho ya zai yamekuwa makubwa zaidi... Mpaka sheby aliogopa huenda yakapasuka..
Lakini sasa kumbe Maneno hayo hayakumuumiza zai peke yake bali hata shadi yalimuumiza katika moyo wake, ukumbuke shadi anasikia kila kitu kule alipo, si unajua mambo ya nyumba za udongo hazinaga siri, labda mnong'onezane skioni, lakini bila ya hivyo ni lazima msikiwa na mtu wa upande wa pili, huezi amini shadi kshikilia kifua chake huku roho ikimuuma kwa kusikia sheby kaoa,.. Kwahio kumbe hata shadi anampenda sheby sema anaogopa kumwambia afu istoshe ana mpenzi wake ambaye ni zai,...
"mume wangu, ivi hio ni story au ni kweli"
Aliuliza zaituni huku akiivuta kanga yake avae
"sitaki kukudanganya, ni kweli nimeoa na nina mwezi wa tatu sasa toka nioe"
"sheby mume wangu, kwaio mimi sina hadhi ya kuwa mkeo... Ahsante sana lakini"
Zai alianza kulia na kukata tamaa ya kuolewa,.. Sheby akaona kumbe zai anampenda sana na anatamani siku moja waishi wote..
"nimekudanganya bwana sina mke wala nini"
Ilibidi amdanganye kuwa hajaoa, lakini ukweli tunaujua kuwa sheby ana mke,..
Sasa huku kwa shadi kuskia hivyo tu alijikuta anaropoka kwa nguvu
"afafhali huna mke jamani"
Sheby aliskia lile neno lakini zai hajaskia vizuri
"nani kasema afadhali"
"aahhh ni watu huko nje sjui wanadaiana"
Aliongea hivyo, lakini sheby kajua hio afafhali imetokea wapi..
Basi kijana sheby aliondoka zake mpaka kwenye vituo vya mikokoteni na kumpa mwenye mkokoteni wake, kisha kaingia hoteli na kuvaa nguo zake za asili yaa uhalisia wake, kama kawaida kachukuwa gari yake na kuingia zake ofisini,.. Kiukweli kijana sheby anateseka sana,..
"mary namsikia boss sjui kaingia sasa hivi"
"ebu kamcheki basi"
"mmmhhh subiri tuone kwani si lazima atembelee wafanyakazi wake"
Kweli sheby hua ana tabia ya kutembelea wafanyakazi wao ili kujua aliopo na ambae hayupo,..
"za saa hizi boss"
Ilikuwa ni sauti ya amina ikimsalimia sheby
"salama tu hali yako"
"safi tu"
Alizunguka ofisi nzima kisha akarudi kuketi katika ofisini yake, wakati huo mzee wake bado hajafika kazini,..
Sasa huku uswahilini baada ya sheby kutoka, shadi karudia kuvaa nguo zake zile zile za kimalaya kisha akachukua kipochi chake na kutoka..
"shadi unaenda wapi saa 5 hii"
"heeeeeeee mi sio golikipa mwenzangu naenda kufanya kazi"
"lakini shadi, kwanini usitafute mwanaume mmoja tu utulie"
"heeeeeeee we zai, mwanaume mmoja atanipa nini mimi, wanaume wenyewe ndio hawa wanaotembeza viazi na mikokoteni"
"no simaanisha Mchumba wangu, we tafuta yeyote yule, kwani lazima auze viazi kama sheby wangu"
"mmmhhh Eti sheby wangu.... Funguka akili wewe, unaweza ukakuta mwenzio kaoa tayari huyo, unafanywa mchepuko tu apo"
"sawa wacha niwe mchepuko tu... Lakini siwezi kumwacha sheby wangu... Shadi, mimi nilikuwa sioni mimi nilikuwa kipofu, lakini kwa uwezo wa mungu, kamjaalia mpenzi wangu akaniseidia... Siwezi kumsaliti"
"utabakia hivyo hivyo"
Shadi aliondoka tena kwa kuita tax,.. Wakati huo sasa ndio anaonyesha makucha yake...
Zai aliingia zake ndani na kuangalia mazingira ya nyumba hiyo akiangalia kitanda, akiangalia makochi ya mbao
"hivi hivi nitaishi nae tu"
Aliongea zai huku akijilaza kitandani,. Zai ni mschana mrembo sana, yaani ana umbo la kipekee sana yani...
Sasa huku kwa akina mama yake na zai aikiwa na Zainabu, pacha wake na zaituni..
"ivi mama, kwanini zaituni hajui kama mpenzi wake ni tajiri"
Aliongea Zainabu huku wakiwa wanakula, yaani mama anawapenda sana watoto wake, japo huyu mmoja ni katili lakini bado anampenda tu..
"afu wewe ndio uliompa umbea kuhusu huyo mwanaume wake"
"wala mimi sijaongea nae mwanao.. Labda alisikia tukiongea"
"naomba uache umbea wako, japo mimi sijui kwanini huyo kijana hataki ajulikane na zaituni"
"we mama weee, usije ukamuuza mwanao"
"kwa jinsi alivyofanya yule kijana, nimemuamini kwa asilimia zote"
Mama Aliongea ukweli wake juu ya kumwamini kijana huyo,..
"mmmhhhhh haya, afu dada hajaja siku nyingi nimemmisije"
Aliingea Zainabu kana kwamba anamemisi sana dada yake wa kwanza mana huyo kaolewa na keshatulia na ndoa yake,...
BAADA YA SIKU KADHAA KUPITA
Rehema ambae ni dada yake na sheby akiwa yupo nyumbani, alikuwa akishangaa sana kuskia mdogo wake kaoa,... Japo alijulishwa kwa simu akiwa chuoni..
"mama, umekubali vipi sheby aoe, huoni kuwa bado ni mdogo yule mama"
Aliuliza rey huku akiwa mkali juu ya mdogo wake kuoa akiwa na umri mdogo..
"mwanangu rey, mimi nimeongea lakini sijasikika kabisaa"
"huyu sheby ana akili kweli, yaani anadiliki vipi kuoa.. Atilist angelikuwa hata na miaka 25"
"heeeeeeee, kwani kaamua yeye, ni baba yako ndio kamlazimisha aoe"
"ati nini... Yaani baba ndio kamwambia aoe"
"sio kumwambia tu, na kumchagulia mke kabisaa kisa ni mtoto wa rafiki yake"
"na wewe mama ukakaa kimya"
"mimi niseme nini na wakati baba yake kaamua kumpa mtoto wake mke"
"wanaishi wapi sasa"
"kule bondeni"
"ngoja nitakwenda kuwasalimia"
"ila staki fujo, sitaki fujo na huyo mwanamke, na kama unakwenda kwa fujo bora usiende"
Mama anamjua mtoto wake rey sio mtu wa kudharauliwa, kitu kidogo tu ngumi mkononi...
"naenda kumsalimia tu"
Ikiwa ni mida ya jioni hivi kama saa 11, Shadi akiwa anarudi mjini tena alikuwa kavaa nguo zingine tofauti na zile alizotoka nazo asubuhi..
"shost, we zai upo"
"heeeeeeee, shadi umebadili nguo tena"
"sasa je, nifanyeje na wakati pesa inaingia tu"
"mmmhhhh umependeza"
"hata wewe unaweza kupendeza tena zaidi ya mimi"
"mmmhhhhh lakini shadi kazi yako ngumu sana kwakweli"
"sikia wewe acha ujinga,.. Una sura nzuri una umbo zuri tena kuliko hata mimi, nashangaa unabweteka tu hapa na kula viazi vya kuchemsha kila siku"
Aliongea shadya kwa kumshawishi zai nae aingie katika kazi alionayo...
"mmmhhhh... Mi nampenda sheby, hivi kwa hiki alichonifanyia, afu leo ananikuta nina mwanaume ivi atanifanyeje"
Aliongea zai huku akiwa kama anaanza kukubali
"heeeeeeee kwani hujaona sheby alivyokuja mi nimebadilika ghafla... Na ni nani atampa taarifa,.. Tafuta pesa wewe acha kubweteka una vyanzo vya pesa nashangaa unavikalia tu"
"mmmmhhhhh... Sasa"
"sasa nini zai.... Hebu ngoja niite tax kwanza nikakunyuke pamba afu usiku tutoke au vipi"
"mmmhhhhh... Sheby atanioana bwana hapana"
"sheby na umaskini aliokuwa nao atawezaje kuingia sehemu za kitajiri? Hio pesa ya kuingilia hapo atatoa wapi"
"haaaa, ina maana wewe unafanyaga na matajiri"
"sasa si ndio mana nami nina pesa, unataka utembee na kapurwa ili iweje"
"mmmhhhh lakini.... "
"acha ujinga.. Ngoja niite taxi,.. Kwanza kila siku unaniomba buku buku zangu wakati hata wewe unaweza kuzipata..... Eeehh haloo Taxi, njoo hapa uliponishusha muda huu"
Tukija huku kwa mke wa sheby akiwa kakaa kwenye kioo huku anajipodoa, yaani meza imejaa vipodozi tu, hakuna mafuta ya mchezo mchezo hapo yote ni ya bei ghali mno....
"hodii"
Alisikia hodi ikibishwa huko sebuleni, wakati yeye alikuwa yupo chumbani kwake,..
"karibu"
Aliongea huku akiuendea mlango na kuufungua
Alikutana na sura ya dada yake sheby sema hamkumbuki vizuri ila dada yake sheby anamkumbuka mana ni watoto waliokuwa kuwa pamoja pamoja, lakini walipokuwa wakubwa kila mmoja alijua mambo yake,.. Na sababu ya hawa kujuana kidogo ni kwamba baba wa mwai na baba rey, ni marafiki toka zamani,..
"mambo"
Rehema alimsalimia mwai lakini mwai alikunja mdomo na kuitikia
"poa nikuseidie nini"
Rey kaingia mpaka ndani na kukaa bila hata kukaribishwa,.. Mwai hamkumbuki kabisa rey lakini rey anamkumbuka ila sio sana yaani kama taswira yake inamjia afu inapotea, si unajua mavipodozi yakiwa mengi usoni hata uhalisia wa sura hupotea,..
"we dada vipi, nakuuliza nikuseidie nini"
Aliongea mwai huku akimjia kwa ukali
"kwanza ungeuliza mimi ni nani afu uongee unavyotaka"
"sioni haja ya kukujua, we sema shida yako nikuseidie uende"
Mwai alikuwa akijibu vibaya kama jinsi anavyomjibu mume wake.... Lakini hahajua kama huyo ni dada yake na sheby
"kwa muda ulioolewa, natumai mpaka sasa hukosi mimba,.. Mana natamani niitwe shangazi"
Sasa mwai ndio anashtuka kwa maneno hayo, na kujua kuwa kumbe huyo alikuwa ni dada yake na mumewe....
"hahahahahaha, ni kweli ninayo ina mwezi mmoja"
Aliongea mwai huku akijichekesha baada ya kujua kuwa huyo ni dada yake sheby, hivyo ni wifi yake
"una uhakika"
"ndi... Nd.... Nd....ndi...ndiooo..."
Mwai alishikwa na kigugumizi cha ghafla, huku akishika tumbo lake
"nina kipimo hapa nimekuja nacho... Unajua mi napenda sana watoto, tena haswa haswa mtoto wako nitampenda sana"
Aliongea rehema kisha akakirusha kile kipimo kwenye meza, afu akamwambia...
"tuhakikishe wote... Mana natamani sana ulete mtoto wa kiume kama mumeo
Je? Nini kitaendelea??... Mwanaheri atafanya nini na hajawahi kufanya mapenzi na mume wake hata siku moja toka waowane... Na je rehema kajuaje kama mdogo wake hajawahi kufanya mapenzi na mkewe... Vipi kuhusu zai, kakubali kujiunga na shadi... USIKOSE