Makapuku Forum

Makapuku Forum

IMG-20171112-WA0014.jpg
IMG-20171112-WA0009.jpg
 
Zaburi 145

1 Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.

2 Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.

3 BWANA ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.

4 Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.

5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.

6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.

7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.

8 BWANA ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
 
Tuombe


Bwana Yesu tuna kila sababu ya kusema asante kwa ajili ya siku njema ya Jumapili ambayo umetupa leo.

Asante kwa ulinzi wako Mungu Mkuu.

Umetulinda Baba na hila zote za adui
Na umetuamsha tukiwa salama.

Mungu Jumapili ya leo tunakuomba ukaonekane ktk lbada zote
Mungu kutana na haja za mioyo yetu
Sema nasi Mungu kupitia neno lako Jehova.

Watumie watumishi wako katika Nguvu na Uweza wa Roho Mtakatifu
Bwana ukawaponye wagonjwa ,waliovunjika moyo ukawafariji Bwana.
Asante Mungu kwa kuwa utakuwa nasi katik Jina la Yesu Kristo wa Naomba na kushukuru
Amen.

JUMAPILI NJEMA ,IBADA NJEMA MBARIKIWE..NAWAPENDA SANA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom