Makapuku Forum

Makapuku Forum

MICHIRIZI YA DAMU -7

“Hujioni? Nenda kachukue kioo halafu jiangalie,” alisema Keith huku akimwangalia Fareed.
“Hapana!”
“Niamini!”
Safari zake za kutafuta wanaume hazikuisha, aliendelea kuizunguka dunia, kila alipoambiwa na wakala wake kwamba kulikuwa na mwanaume aliyekuwa akimtaka, alikwenda huko, alizunguka sehemu mbalimbali na hakutaka kabisa Godfrey ajue kile kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
“Upo wapi Fareed,” aliuliza Keith kupitia ujumbe mfupi kwenye Mtandao wa WhatsApp.
“Ubelgiji!”
“Nahitaji nikuone.”
“Lini?”
“Hata kesho!”
“Mh! Mbona haraka hivyo?”
“Kwa sbabu nimekumisi.”
“Basi naomba tufanye wiki ijayo. Nitakuja tu rafiki yangu,” alisema Fareed.
“Basi sawa. Nakusubiri kwa hamu!”
“Kuna nini lakini?”
“Hakuna kitu! Nataka nikuone tu.”
“Mmh! Sawa,” alisema Fareed na kukata simu, hakuamini kama kulikuwa na kitu cha kawaida, alijua kabisa kwamba kulikuwa na kitu mwanaume huyo alikuwa akikihitaji kutoka kwake. Hivyo akajiandaa.
****
Bilionea Keith alikuwa nyumbani kwake ametulia, aliyafikiria maisha yake, tangu siku alipopata ufahamu mpaka hapo alipofika. Alipitia mengi, alipata matatizo makubwa lakini yote hayo baadaye yakageuka na kuwa changamoto katika maisha yake.
Alifanya ushenzi wa kila aina kupitia fedha zake. Alitembea na wanawake wa kila aina, alifanya ujinga wote mpaka kuona kwamba hakukuwa na ujinga ambao hakuwahi kuufanya katika maisha yake mpaka sasa.
Aliyatathmini maisha yake na mwisho kugundua kwamba kwenye ushenzi wote aliokuwa ameufanya, kulikuwa na ushenzi mmoja tu ambao hakuwa ameufanya na ndiyo ambao ulimfanya kumpigia simu Fareed na kuomba kuonana naye.
Mwili wake ulimsisimka, hakutaka kuona kitu kingine tena zaidi ya kutembea na Fareed ambaye kwa muonekano wake tu ulimtamanisha kupita kawaida. Siku iliyofuata akampigia simu na kutaka kuonana naye kitu ambacho hakikuwa kigumu kwa Fareed, akamwambia kwamba wiki inayofuata angeonana naye na kutaka kusikia kile alichokuwa amemuitia.
Kuanzia siku hiyo, Keith akawa na mawazo mengi, moyo wake haukutulia, ilikuwa ni kama Fareed alikuwa na majini kwani kipindi cha nyuma alimuona kuwa mtu wa kawaida lakini muda huo alibadilika, alianza kupata nguvu sana moyoni mwake.
Mwanaume tata huyo kila siku akawa akiwasiliana naye na kumuuliza ni kitu gani hicho alitaka kumwambia lakini Keith hakutaka kufumbua mdomo wake na kumwambia zaidi ya kumpa taarifa kwamba angemwambia kama angekwenda nchini Marekani.
“Jamani! Unaniweka kwenye presha mwenzako!” alisema Fareed kwenye simu kwa sauti yake ya kike.
“Usijali! Utakuja na kuona tu,” alisema Keith.
Siku zikakatika na hatimaye siku ya kwenda nchini Marekani ikawadia. Njiani, Fareed alikuwa na mawazo mengi, hakufikiria kitu kuhusiana na mapenzi, alimwamini mwanaume huyo na kwake alikuwa mmoja wa marafiki zake wakubwa.
Ndege hiyo ilichukua saa zaidi ya ishirini ndipo wakafika nchini Marekani, gari la kifahari lilimfuata, likamchukua na kuelekea katika jumba jingine la Keith ambapo huko aliambiwa asubiri na mwanaume huyo angefika siku hiyo.
Lilikuwa jumba kubwa mno, alizunguka katika kila chumba lakini hakuweza kulimaliza, kila chumba alichoingia kilikuwa kikubwa, alitembea mpaka kuchoka hivyo akaamua kwenda kupumzika katika bwawa la kuogelea.
Walinzi waliokuwa humo walikuwa wakimwangalia Fareed. Hawakuelewa kama huyo waliyekuwa wakimwangalia alikuwa mwanaume au mwanamke. Wengi wakahisi kwamba alikuwa mwanamke, kwa jinsi alivyokuwa mzuri na mikogo yake lakini kitu cha ajabu kabisa, kifuani hakukuwa kama mwanamke, kifua chake kilinyooka kama mwanaume.
“Is he a girl?” (ni mwanamke?) aliuliza jamaa mmoja huku akiwa amemtumbulia macho Fareed.
“I don’t know!” (sifahamu) alijibu jamaa mwingine, yeye mwenyewe alivyomwangalia Fareed, hakumuelewa hata kidogo.
Baada ya kukaa kwa saa tatu ndipo Keith akafika nyumbani hapo. Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kwenda katika chumba alichompangia Fareed na kumkuta huko.
Mapigo yake ya moyo yalikuwa juu, alimwangalia mwanaume huyo, mwili wake ulikuwa ukisisimka kupita kawaida, alijishangaa kwani kipindi cha nyuma hakuwa hivyo, japokuwa alikuwa mwanaume tata lakini kwake bado aliendelea kuwa mwanaume ila kwa siku hiyo alikuwa hoi kabisa.
Akamsogelea na kumkumbatia, mapigo yake ya moyo yalizidi kudunda kwa nguvu kiasi kwamba mpaka Fareed akashtuka kwani haikuwa kawaida kwa mwanaume huyo kuwa katika hali hiyo.
“What the hell wrong with you?” (una nini jamani?) aliuliza Fareed huku akimwangalia Keith.
“I got nothing!” (hakuna chochote)
“No! Tell me the truth!” (Hapana! Niambie kweli)
“That’s the truth! I got nothing. I just missed you,” (huo ndiyo ukweli! Sina kitu, nilikukumbuka tu) alijibu mwanaume huyo huku kwa mbali kijasho chembamba kikianza kumtoka.
Walikaa na kuzungumza mambo mengi, muda mwingi alikuwa akimwangalia Fareed, mapigo yake ya moyo hayakuacha kudunda na kwa jinsi Fareed alivyokuwa na makusudi, akaanza kukaa mikao ya hasarahasara pale kwenye kochi.
Moyo wake ulikuwa kwenye maombi mazito, kila alipomwangalia Fareed jinsi alivyokaa pale kwenye kochi, aliona kabisa shetani alikuwa akimzidi nguvu, tena kwa kasi kubwa.
Alipambana lakini kila alipotaka kujivika ujasiri aliisikia sauti ikimwambia moyoni mwake kwamba kwa nini asimwambie ukweli Fareed na kumpa kile alichokitaka? Lakini wakati akifikiria hivyo, pia upande mwingine, sauti nyingine ikamwambia kwamba hakutakiwa kufanya hicho alichokuwa akikifikiria kwani lilikuwa chukizo mbele za Mungu wa mbinguni.
“Nitaweza kweli kumshinda shetani? Mungu! Sina nguvu zako moyoni mwangu! Kweli nitaweza kumshinda shetani?” aliuliza Keith huku akimwangalia Fareed ambaye hakuuonekana kuwa na wasiwasi pale kwenye kitanda alipokuwa amekaa, ndiyo kwanza akazidi kuvianika vipaja vyake vilivyopakwa losheni na kukolea hasa.
“Haya niambie sasa…” alisema Fareed.
“Umenikumbusha! Kuna kitu nilitaka kukwambia,” alisema Keith huku akimsogelea Fareed kitandani pale.
“Kitu gani?”
“Ninahitaji ukafanyiwe upasuaji!”
“Upasuaji! Wa nini?”
“Uwekewe makalio makubwa na hata kifua chako kitunishwe, kiwe kama cha mwanamke,” alisema Keith huku akimwangalia Fareed.
Hilo ndilo alilokuwa akilitaka, alitamani kuonekana kama mwanamke. Alitamani kubadilisha jinsia yake na kuwa mwanamke lakini alishindwa, aliogopa kwa kuhisi kwamba angeweza kupata matatizo makubwa.
Akakubaliana na Keith kwamba akafanyiwe upasuaji na kuwekewa muonekano wa kike. Fareed akafurahi sana kiasi kwamba akasimama pale alipokuwa na kumfuata Keith kisha kumkumbatia kwa furaha kubwa.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Siku hiyohiyo Keith akawasiliana na Dk. Fabby wa Hospitali ya New Lucas Medical Center ambaye alikuwa mtaalamu wa upasuaji kwa watu waliokuwa wakihitaji kuwekewa muonekano wa jinsi nyingine. Wakakubaliana na hivyo kitu cha kwanza kabisa alichokitaka ni kuonana na huyo mtu.
Fareed akapelekwa hospitalini hapo. Dk. Fabby alipomuona, hakuamini kama mtu huyo alikuwa mwanaume, alimwangalia kwa makini, alionekana kama mwanamke kwa jinsi alivyokuwa akijiweka.
Akamuita ofisini kwake na kukaa kisha kuzungumza naye. Fareed aliulizwa maswali kadhaa ambayo aliyajibu bila kuwa na hofu yoyote ile kitu kilichomfurahisha daktari huyo.
“Na huyu ni bwana wako?” aliuliza Dk. Fabby!
“Hapana! Ni rafiki yangu!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Unajua wewe ni mzuri sana!” alisema Dk. Fabby huku akimsogelea Fareed pale alipokaa, akamshika mkono, kijana huyo akashtuka kwani hakutegemea kumuona dakatri huyo akiwa amebadilika ghafla kama alivyokuwa.
“Unataka kufanya nini?” aliuliza Fareed, alijua kile alichokitaka kukifanya daktari huyo ila alimua kumuuliza kama kumtega.
“Dhambi iliyofanya Sodoma na Gomora kuteketezwa kwa moto,” alisema Dk. Fabby huku akimvua shati laini alilolivaa Fareed ambaye naye bila kipingamizi akamsaidia dokta huyo kuliondoa kabisa mwilini mwake.
“Mh! Leo kazi ipo! Kama hii hospitali haitopaa leo kwa ufirauni ninaotaka kuufanya, basi nitakuwa na bahati,” alijisemea daktari huyo huku akimwangalia Fareed, tena wakati mwingine alitoa pumzi nzitonzito.
***
Godfrey alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, moyo wake ulimuuma sana kwani kwa jinsi mambo yalivyokuwa yakiendelea, alihisi kabisa kuna jambo baya nyuma yake.
Alijaribu kumtafuta Fareed kwenye simu, hakuwa akipatikana, alimtumia meseji nyingi sana WhatsApp lakini mwanaume huyo hakujibu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, akili yake ilimwambia kwamba wakati huo alikuwa na mwanaume mwingine kitandani kitu kilichouchoma moyo wake vilivyo.
Hakutaka kukata tamaa, aliendelea kumtafuta zaidi na zaidi lakini hakufanikiwa hata kumpata. Kwa kuwa aliwafahamu baadhi ya marafiki zake, akaanza kuuliza huko lakini hakupata majibu, kila aliyemuuliza alisema kwamba hakumuona kitu kilichomuuma sana.
Akakosa furaha, hata kula hakuwa akila, mkewe alimshangaa, alihisi kwamba mume wake alikuwa mgonjwa hivyo kumuuliza mara kadhaa juu ya kilichokuwa kikimsumbua lakini hakuwa radhi kukisema.
“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Theresa huku akimwangalia mume wake usoni.
“Moyo unauma sana!” alijibu huku akishika upande wa moyo wake.
“Kwa nini unauma? Umeanza lini kuuma? Twende hospitali,” alisema Theresa huku akimwangalia mume wake ambaye hakuzungumza kitu zaidi ya kukaa kimya tu.
Aliwahi kuumia maishani mwake lakini maumivu aliyoyapata siku hiyo yalikuwa ni zaidi ya maumivu. Hakukuwa na kitu kilichokwenda sawa, muda mwingi alikuwa akihuzunika, alipokuwa akilala, alimuona Fareed akiwa na mwanaume chumbani kitu kilichouchoma moyo wake vilivyo.
“Haiwezekani! Nitamtafuta mpaka nimpate!” alijisemea.
Alichokifanya siku iliyofuata ni kumtafuta kijana mkali wa kompyuta na kuanza kuzungumza naye. Alimwambia dhumuni lake kwamba ni kumtafuta mtu ambaye alikuwa akitumia simu aliyompa namba zake. Mwanaume huyo akachukua na kuziingiza kwenye kompyuta yake.
Ilikuwa kazi kubwa lakini aliona ilikuwa ni lazima kumsaidia mwanaume huyo kwani kwa jinsi alivyoonekana, alihitaji msaada wake kuliko kitu chochote kile.
Alichokifanya jamaa ni kuiweka programu moja iitwayo Hack My Phone kisha kuziweka namba zile. Hilo wala halikuwa tatizo kwani baada ya nusu sana, GPRS ilionyesha mahali alipokuwa Fareed, alikuwa Los Angeles nchini Marekani.
“Nimempata!” alimwambia Godfrey ambaye alimsogelea.
“Yupo wapi?”
“Los Angeles!”
“Sehemu gani?”
Akamwambia sehemu alipokuwa, hilo halikuwa tatizo alichokifanya ni kuchukua maelezo yote na kuiscreen shot eneo alilokuwa Fareed na hivyo kupanga siku ya kwenda Marekani.
“Unakwenda Marekani? Mbona ghafla hivyo?” aliuliza Theresa huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Kuna kitu nakwenda kufanya.”
“Kitu gani?”
“Nimesema kuna kitu nakwenda kufanya!” alisema Godfrey kwa sauti kubwa yenye ukali.
Theresa akahisi kwamba kulikuwa na tatizo kubwa hivyo akamuacha mumewe, kitendo cha kumjibu namna ile kilimaanisha kulikuwa na jambo kubwa nyuma yake.
Hakutaka kuzungumza sana, aliogopa kumkorofisha hivyo kumuacha afanye alichotaka kukifanya. Usiku mzima Godfrey hakulala, alichanganyikiwa na kichwa chake alikiona kuwa kizito sana.
Alipokamilisha taratibu zote za safari, hakutaka kuendelea kubaki nyumbani, akaondoka zake kuelekea Marekani. Ndani ya ndege, alikuwa kimya kabisa, alikuwa na mawazo mengi, hata mtu aliyekaa pembeni yake hakutaka kumuongelesha kwani kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa mtu wa mawazo tele.
Ndege ilichukua saa ishirini na mbili mpaka kufika nchini Marekani, katika Jiji la New York ambapo akateremka na kuunganisha ndege mpaka jijini Los Angeles katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa LAX na kuteremka.
Akaichukua simu yake, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuiangalia ile picha aliyokuwa ameiscreen shot, picha iliyomuonyesha sehemu ambapo mpenzi wake alipokuwepo. Alipopaangalia vizuri, akaelekea hotelini.
Hakuacha kumtafuta Fareed, aliendelea kumtafuta zaidi lakini hali haikubadilika, ilikuwa vilevile kwamba hakumpata na hata alipomtumia meseji, hazikujibiwa kitu kilichomchanganya zaidi.
“Huyu atakuwa na mwanaume tu! Yaani wewe subiri! Nitaua mtu,” alijisemea. Japokuwa alikuwa amechoka, hata kulala hakuweza kulala, kichwa chake kilivurugwa na ilikuwa ni lazima ajue kitu gani kilikuwa kikiendelea.
****
Baada ya dakika arobaini na tano, kila mmoja alikuwa hoi. Dk. Fabby alimwangalia Fareed, moyo wake ukajisikia hukumu nzito na kulaumiwa kwa kile alichokuwa amekifanya. Hakujua ni shetani gani alimuingia mpaka kumpelekesha namna ile na kuamua kufanya ushenzi mkubwa kama ule.
Alijuta moyoni mwake, alishindwa kumwangalia Fareed, akaelekea choooni. Huko, alibaki akilia kwa maumivu mazito, huzuni kubwa ilimuingia na hakuamini kama ingetokea siku ambayo angefana ushenzi mkubwa kama huo.
Alimlaumu shetani, alimpa tamaa mbaya ambayo ilimfanya kuusaliti moyo wake na Mungu wake. Kule chooni hakutoka haraka, alikuwa akilia kwa majuto makubwa.
Fareed alipoona Dk. Fabby anachelewa kutoka, akausogelea mlango na kuugonga. Daktari huyo alishtuka na kukumbuka kwamba kulikuwa na kazi aliyotakiwa kufaya, hivyo harakaharaka akanawa uso na kutoka nje.
Hakutaka kumchangamkia Fareed, alichokifanya ni kumpeleka kitandani, akamlaza na kisha kumchoma sindano iliyokuwa na dawa ya kuyaongeza makalio yake kidogo na kifua chake, awe na muonekano kama mwanamke mbichi.
“Tayari!” alisema Dk. Fabby huku akimwangalia Fareed.
“Nashukuru mpenzi!” alisema Fareed huku akimshika kidevu Dk. Fabby lakini akajikwepesha.
“Eeh! Jamani una nini?” aliuliza Fareed.
“Nenda nyumbani!”
“Sawa. Lakini usikose kunipigia. Nitakumiss sana,” alisema Fareed, Dk. Fabby hakuzungumza kitu chochote kile, akamuondoa Fareed chumbani humo.
Hilo hakutaka kulijali sana, Fareed ni akaondoka hospitalini hapo. Moyo wake uliridhika kwani hicho ndicho kitu alichokifanya kila siku. Aliuchukia muonekano wake na alipogundua kwamba baada ya siku chache angekuwa na muonekano wa kike, akafurahi zaidi.
Alipofika nyumbani, akaelekea chumbani na kutulia kitandani. Akachukua simu yake na kuanza kumpigia Dk. Fabby lakini mwanaume huyo hakuhitaji mazoea tana.
“Lakini mbona unanikataa?” aliuliza Fareed.
“Naomba uniache!”
“Nikuache upumzike?”
“Yaani uniache moja kwa moja. Usinijuejue,” alisema Dk. Fabby na kukata simu.
Fareed alihuzunika lakini hakuwa na jinsi, hakutaka kuwasiliana na Dk. Fabby kwani hakumpenda kama alivyompenda Keith ambaye alikuwa tayari kumpa kiasi chochote cha fedha japokuwa hakutaka kumwambia ukweli.
“Haina shida.”
ITAENDELEA
 
MICHIRIZI YA DAMU -1 NYEMO CHILONGANI

GIZA, Misri
Zilisikika kelele kutoka ndani ya piramidi moja lililokuwa katika Mji wa Giza uliokuwa nchini Misri. Watu waliokuwa humo ambao asilimia kubwa walikwenda kutalii wakatoka huku wakikimbia kwani mbali na kelele hizo, piramidi hilo halikuwa la kawaida, lilikuwa linatisha kiasi kwamba hata watalii waliokuwa wakiingia, walishikana mikono kama njia mojawapo ya kutokutana kuuawa na majini yaliyosadikiwa kwamba yalikuwepo ndani ya piramidi hilo.
Mwanamke yule aliyekuwa amepiga kelele akatoka huku akitetemeka, kijasho chembamba kikimtoka, walinzi waliokuwa mahali hapo wakamsogelea kwa lengo la kutaka kufahamu kilichomfanya mpaka kupiga kelele kiasi hicho hadi kuwaogopesha watu wengine.
Walipomuuliza mwanamke huyo wa Kiingereza akawaambia kwamba aliiona maiti ndani ya piramidi hilo kitu kilichomtisha kila mtu.
“What?” (nini?) aliuliza mwanaume mmoja.
“A deadbody!” (maiti)
“Are you sure?” (una uhakika?)
“Yes!” (ndiyo) alijibu mwanamke huyo huku akiendelea kutetemeka kwa hofu.
Watu wote waliotoka ndani ya piramidi hilo wakaanza kumwangalia mwanamke yule, wengine hawakuridhika, wakamsogelea na kumuuliza kilichokuwa kimetokea ndani ya piramidi lile, hakuficha, aliwaambia wazi kwamba aliiona maiti ikiwa chini kitu kilichomfanya kupiga kelele na kukimbia.
“Siyo kwamba umeona mauzauza?” aliuliza jamaa mmoja.
“Kwani mauzauza siyajui? Nimeona maiti!”
“Sasa kwa nini ulikuwa peke yako na wakati hairuhusiwi?” aliuliza mwanaume mwingine.
“Niliingia na mume wangu! Yeye alikwenda upande mwingine na mimi kwenda mwingine,” alijibu mwanamke huyo na mumewe kutokea hapo, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumkumbatia mkewe.
Walinzi waliokuwa hapo wakachukua tochi zao na kuingia ndani ya piramidi hilo, walitaka kuona kile alichokiona mwanamke huyo. Kwa miaka mingi, tangu karne ya ishirini ilipoingia hakukuwa na mtu yeyote aliyekufa ndani ya piramidi hilo japokuwa kulikuwa na tetesi za kuwepo kwa majini. Kama hakukuwa na mtu aliyekufa! Iliwezekanaje mwanamke huyo kuona maiti humo?
Wakaingia mpaka ndani, wakaanza kumulika huku na kule, wakaelekea kule mwanamke yule alipokwenda huku wakiwa makini kuangalia chini. Kama alivyosema mwanamke yule ndivyo walivyokuta, macho yao yakatua katika mwili wa mwanaume mmoja uliokuwa chini, ulichomwa visu mara tatu kifuani na tumboni, mbali na hivyo, maiti yake iliburuzwa na kuachwa michirizi ya damu pale chini.
Kila mmoja alishtuka, hawakuamini kile kilichotokea, ilikuwaje mwanaume huyo auawe ndani ya piramidi hilo halafu muuaji asionekane? Kitu cha kwanza kabisa, hawakuigusa maiti ile, wakatoka ndani na kuelekea katika kompyuta zao na kuangalia orodha ya watu walioingia ndani ya piramidi lile dakika chache zilizopita kwani hata maiti ile ilivyoonekana, haikuonekana kama iliuawa muda mrefu uliopita.
“Mmeangalia jina lake?”
“Hapana!”
“Hebu kampekueni, mnaweza kuona hata kitambulisho,” alisema mwanaume aliyeshika kompyuta mpakato na hivyo walinzi hao kurudi ndani ya piramidi lile huku watu wengine wakiwa nje na idadi kubwa ya watu ikizidi kuongezeka.
Walipoingia humo, wakampekua mfukoni na kukuta ‘business card’ iliyomtambulisha kwa jina la Benjamin Keith, mwanaume wa Kimarekani aliyekuwa akimiliki kampuni kadhaa ikiwemo kampuni ya mavazi ya Cotton Keith.
“Kumbe ni Keith!” alisema mwanaume mmoja kwa mshangao.
“Ndiye nani?”
“Yule bilionea wa Kimarekani!”
“Unamaanisha yule mwenye utajiri wa dola bilioni kumi na mbili?” aliuliza mlinzi mwingine.
“Ndiyo!”
“Mh! Hebu nione hiyo kadi.”
Akakichukua na kuanza kukiangalia, kama alichokiona mwenzake na yeye alikiona hivyohivyo. Kila mmoja alishangaa, hawakuamini kile walichokuwa wakikiona, waliwafahamu sana matajiri, kila kona walipokuwa wakienda, walikwenda na walinzi wao, ilikuwaje Keith aende huko peke yake mpaka kuuawa? Kila walipojiuliza wakakosa majibu.
Wakatoka nje wakiwa na ile kadi na walipomuonyeshea jamaa aliyekuwa na kompyuta, akaangalia jina lile, akagundua kwamba Keith alikuwa ameingia ndani ya piramidi lile na msichana, mrembo aliyeitwa kwa jina la Maria Ogabugu aliyekuwa na asili ya Nigeria.
“Aliingia na mwanamke humu ndani,” alisema jamaa huyo.
“Hebu tuone.”
Akaangalia kwenye kompyuta ile kwa lengo la kujiridhisha, kile alichoambiwa ndicho alichokiona kwamba bilionea huyo aliingia na mwanamke aliyejulikana kwa jina hilo ndani ya piramidi hilo. Hawakujua mwanamke huyo alikuwa wapi kwani walikuwa na uhakika kwamba yeye ndiye aliyemuua Keith na kisha kukimbia.
Wakawasiliana na polisi ambapo baada ya dakika kadhaa wakafika na kuingia ndani ya piramidi lile. Wakaelekea mpaka kule kulipokuwa na maiti ile kisha kuiangalia. Ilionyesha kwamba hakuuawa muda mwingi uliopita, na hata kama muuaji alikimbia, hakuwa amefika Cairo.
Wakaupiga picha mwili ule kisha kuubeba kwa lengo la kuondoka nao ila kabla hawajaondoka, wakaona kipande cha karatasi kikiwa chini, kilikuwa kimezibwa na mwili ule, wakakichukua kikaratasi hicho kilichoandikwa kwa maneno machache kwa Kifaransa yaliyosomeka C’est fait yakiwa na maana ya kukamilika kwa jambo au ‘done’ kwa Lugha ya Kiingereza.
Hilo likaibua maswali mengi, hakukuwa na mtu aliyejua maana ya neno lile lililoandikwa. Mwili ukachukuliwa na kupelekwa hospitali ambapo familia yake ikapigiwa simu na kuambiwa kile kilichokuwa kimetokea.
Taarifa hiyo ikawekwa kwenye mitandao ya kijamii na kutangazwa sana katika vituo vya televisheni na radio. Kila mtu aliposikia habari hiyo alishangaa, hawakuamini kama bilionea Keith aliuawa ndani ya piramidi nchini Misri kwani alikuwa mtu mwema ambaye kila mtu alijua kwamba angeishi miaka mingi kwa ajili ya kuendelea kuwasaidia watu masikini.
Serikali ya Marekani haikutaka kukubali, mawasiliano yakafanyika kwenda nchini Misri na kuwaambia kwamba wafanyaje kila linalowezekana mpaka muuaji huyo apatikane, kama walikuwa na uwezo wa kwenda sehemu yoyote ile, ilikuwa ni lazima mwanamke huyo akamatwe.
Lilikuwa ni agizo kubwa na gumu, hawakujua mahali alipokuwa muuaji hivyo polisi kwenda kuulizia katika piramidi hilo na kuambiwa kwamba bilionea huyo alikuwa na mwanamke wa Kinageria aliyeitwa Maria Ogabugu.
“Huyu mwanamke ndiye anayetakiwa kutafutwa na kupatikana haraka iwezekanavyo,” alisema kamanda wa jeshi la polisi jijini Cairo.
“Sawa mkuu!”
Usikose sehemu ya pili hapa
Asante mumy
 
MICHIRIZI YA DAMU -8 NYEMO CHILONGANI

Akakaa na kumsubiria mzee huyo. Alimwambia kwamba angefika nyumbani hapo muda si mrefu. Akajiachia kochini huku moyo wake ukiwa na amani kwamba alifanikiwa kulala na Dk. Fabby, hata kama hakumtaka tena kwake wala hakulijali sana.
Baada ya saa moja, Keith akafika nyumbani hapo. Alipomuona Fareed, akamfuata na kumkumbatia. Alimkumbuka na muda wote alikuwa akimuwaza yeye tu. Walikaa na kuzungumza, Keith hakutaka kumwambia ukweli Fareed jinsi alivyokuwa akijisikia ila alijua kwamba mwanaume tata huyo alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
“Umefanikiwa?” aliuliza Keith.
“Ndiyo!”
“Safi sana, hebu nione,” alisema mwanaume huyo na kutaka kuonyeshewa.
Hilo halikuwa tatizo kwa Fareed, akavua nguo zake na kisha kumwangalia. Mapigo ya moyo wa Keith yalikuwa yakienda kasi, hakuamini kama alikuwa akimwangalia mwanaume huyo.
Mwili wake ukamsisimka, hakutaka kukubali, akamchukua Fareed na kwenda naye kitandani, hapo, akaanza kumwambia maneno mengi ya mahaba, jinsi alivyokuwa akimpenda, hakuacha kumsifia kwa kila kitu kiasi kwamba Faredd akajiona kuwa mzuri kuliko watu wote duniani.
“Kweli?”
“Ndiyo! Wewe ni malaika wangu, ni mrembo kuliko warembo wote waliowahi kutokea katika hii dunia!” alisema Keith maneno ambayo alikuwa na uhakika kwamba hayakuwa kweli bali alitaka kukamilisha kile alichokitaka.
Fareed akaachia tabasamu pana, akajiangalia, akahisi kwamba kweli alikuwa mrembo kuliko warembo wote waliowahi kutokea katika dunia hii. Akashikwa mkono, akaacha, akashikwa bega, akaacha, kila alipokuwa akishikwa huku na kule, aliacha na mwisho wa siku, baada ya saa moja wote kujikuta wakiwa hoi kitandani.
“Ahsante,” alisema Fareed huku akimwangalia Keith kwa uso uliokuwa na tabasamu pana.
“Umeridhika?”
“Sana mpenzi! Kumbe nilikuwa najichelewesha tu!” alisema Fareed huku akimwangalia mwanaume huyo.
Penzi jipya likaanzishwa, kila mmoja alikuwa bize na mwenzake, japokuwa Keith alikuwa na familia yake jijini New York lakini hakutaka kurudi huko, alitekwa na biashara zake zote alizihamishia huko, mahesabu akawa anapelekewa hukohuko alipokuwa.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, mapenzi ya jinsi moja yalimpeleka puta na hakukumbuka kitu chochote kile. Siku wiki moja baadaye akaamua kumfanyia sapraizi Fareed, alitaka kumnunulia gari jipya kwani hakutaka kuona akipata tabu yoyote ile.
Siku hiyo akakaa na kuzungumza naye mengi, ilipofika saa sita mchana, akamchukua na kisha kuondoka nyumbani hapo. Wakati wametoka ndani ya jumba hilo kubwa na kushika barabara, ghafla akaliona gari moja likiwafuata kwa nyuma.
Wakawa na hofu kwa kuhisi kwamba inawezekana watu waliokuwa humo walikuwa majambazi waliotaka kuwaua au kuwaibia hivyo. Kila Keith alipokuwa iongeza mwendo, gari la nyuma likawa linaongeza kasi kiasi kwamba wakaona huo ndiyo ungekuwa mwisho wao.
Walichokifanya ni kuingia kwenye barabara kubwa ambapo walikwenda mpaka sehemu iliyokuwa na watu wengi, akalisimamisha gari hilo kwa kuamini kwamba hata kama watu hao wangeteremka kwenye gari na kuwafuata, wasingeweza kuwaua kutokana na wingi wa watu mahali hapo.
Gari lile la nyuma likasimama na mwanaume mmoja kuteremka. Hawakuzungumza kitu, walibaki wakimwangalia mwanaume huyo ambaye alionekana kuwa na hasira kubwa.
Fareed hakumtambua mpaka alipofika karibu, Keith akateremsha kioo, macho ya Fareed yakatua kwa mwanaume aliyekuwa akimfahamu, alikuwa Godfrey aliyeonekana kuwa mwenye hasira kupita kawaida.
Akaanza kuwaangalia wote wawili kwa macho yaliyokuwa na shari, kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa tayari kufanya jambo lolote lile kwani hata mwili wake ulianza kutetemeka kwa hasira kali.
****
“What can I help you, sir?” (nikusaidie nini bwana mkubwa?) aliuliza Keith huku akimwangalia Godfrey aliyekuwa na hasira kali.
“I want my bae,” (namtaka mpenzi wangu)
“Your bae? Who the hell is she?” (mpenzi wako? Ndiye nani huyo?) aliuliza Keith huku akimwangalia mwanaume huyo machoni.
Godfrey akayahamisha macho yake na kumwangalia Fareed ambaye alikuwa akitetemeka tu. Kwa kitendo kile cha kumwangalia Fareed, Keith akajua mtu aliyekuwa akizungumziwa na hivyo kumuuliza Fareed kama alikuwa akimfahamu mwanaume huyo.
“I don’t know him,” (wala simfahamu) alisema Fareed huku akimwangalia Godfrey kwa macho yaliyojaa mshangao, alionekana kama kweli hamfahamu mwanaume huyo.
“Fareed, look at my eyes! Don’t you know me? Look at my eyes bastard,” Fareed, yaangalie macho yangu! Hunifahamu? Yaangalia macho yangu mwanaharamu weee) alisema Godfrey huku akionekana kuwa na hasira kali zaidi.
Bado Fareed aling’ang’ania kwamba hakuwa akimfahamu mwanaume huyo na hiyo ndiyo siku ya kwanza kumuona machoni mwake. Keith hakutaka maswali zaidi, alichokifanya ni kumwambia dereva wake aliondoe gari mahali hapo na kufanya hivyo.
Godfrey alibaki akiwa amelowa, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea, kukataliwa na Fareed mchana kweupe namna ile kulimuumiza mno moyoni mwake. Watu wote walikuwa wakimwangalia, wengine walimpigia honi kumaanisha kwamba walimtaka aondoke mahali pale ili waendelee na safari yao.
Akarudi ndani ya gari, akaingia na kutulia kwenye usukuni, alikuwa na wazo tele na muda mwingine alikuwa akitokwa na machozi, kwa kile kilichokuwa kimetokea kwake kilionekana kuwa kama ndoto ya mchana. Hakukaa sana mahali hapo, akaondoka zake huku akiwa na hasira kifuani.
Moyo wake ukajaa ghadhabu, hakufikiria kitu kingine kama kumuua Fareed. Aliutesa moyo wake, hakuwa radhi kumuona mwanaume tata huyo akiendelea kuishi na wakati aliuumiza moyo wake kupita kawaida.
“Ni lazima nimuue, nitatumia gharama zangu zote kumuua huyu mpumbavu,” alisema Godfrey huku akionekana kuwa na hasira sana. Moyo wake ukapanga kumuua Fareed kama kumlipizia kisasi kwa kile alichokifanya.
***
Wanaume wote waliokuwa wakitembea na Fareed walichanganyikiwa, hawakuamini kama alikuwa akijua sana kitandani. Mioyo yao iliuchanganyikiwa, walipokutana naye, hawakutaka kumuacha, waliendelea kumtafuta zaidi na zaidi.
Kitendo cha kuwa na Keith kwake yalikuwa mateso makubwa, alibanwa sana kwani mwanaume huyo hakutaka kumuona akiondoka kuelekea sehemu yoyote ile.
Alipokea simu kutoka kwa matajiri wengi ambao walimuahidi kumpa kiasi kikubwa cha fedha lakini kuonana nao suala hilo lilikuwa gumu sana. Aliwasiliana nao kwenye simu, aliwatumia picha zilizokuwa zikionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa mzuri.
Hakuzoea kuwa na mwanaume mmoja, tangu alipompata wakala wake, Asteria, alikuwa akitoka na wanaume mbalimbali, hayo ndiyo yalikuwa maisha yake na hata alipoambiwa na Keith kwamba hakutakiwa kutoka, kwake yalikuwa mateso makubwa.
“Haiwezekani! Siwezi kukaa na mwanaume mmoja, kwani kanioa? Yeye mbona ana familia yake, lazima nitoke,” alisema Fareed huku akionekana kutokukubaliana na kile kilichokuwa kikiendelea.
Ndivyo alivyofanya, baada ya wiki moja huku akiwa amempa Godfrey mahaba mazito akaamua kuondoka na kuelekea Dubai. Hakuwa ameaga, alimtoroka kwani kitu alichokuwa akikiangalia ni kwa namna gani angeweza kuifurahisha roho yake.
Huko Dubai alikwenda kuonana na bilionea mwingine, Saed ambaye alikuwa akimsumbua sana kwenye simu. Walipoonana kwa mara nyingine, wakaelekea kitandani ambapo huko wakafanya mambo yote na kukumbushiana siku ya kwanza walipokuwa wameonana.
Hakutaka kuwasiliana na Keith, mwanaume huyo alimpigia sana simu kutaka kuzungumza naye lakini hakupokea, alinyamaza kimya na hata zile meseji alizokuwa akitumiwa, nazo hakuzijibu japokuwa aliziona na kuzisoma.
Akili na mawazo yake yalikuwa kwa Bilionea Saed tu ambaye hakuwa msiri, alimchukua Fareed na kumtamulisha kwa baadhi ya marafiki zake na kuwaambia kwamba alikuwa mpenzi wake wa kufa na kuzikana. Hilo lilimpa furaha Fareed kwa kuamini kwamba angeishi milele na mwanaume huyo.
Marafiki wa Saed nao hawakutaka kukubali, kwa kuwa Fareed alionekana kuwavutia tena huku kwa nyuma akianza kutuna na kifua kuonekana, hawakutaka kumuacha, walichokifanya ni kuanza kummendea kitu ambacho kilimfurahisha kwani akili yake ilifikiria fedha kuliko mapenzi.
Alipokea meseji nyingi kutoka kwa wanaume mbalimbali, wote walimtaka kimapenzi. Hakuwa mchoyo, alikubali kufanya nao na hivyo kukutana nao sehemu yoyote waliyotaka na kuwaridhisha.
Ndani ya mwezi mmoja akatembea na marafiki kumi wa Saed, hakuwa akijua, alipokuwa naye alikuwa akimsifia kwa marafiki zake kumbe ndiyo haohao waliokuwa wakimbadilikia kila alipowapa kisogo.
Wakati mwezi wa pili ulipokatika, ndipo akaingia kwenye umbo rasmi la kike, alikuwa na muonekano kama wa wanawake wengine, alikuwa na kifua kikubwa, wowowo, mavazi ya kile, alijitahidi kuibadilisha sura yake kwa kuipaka sana poda, akaseti nywele zake, kwa kifupi alikuwa mwanamke kamili isipokuwa sehemu za siri ambapo alishindwa kuibadilisha.
“Hivi huyu mpumbavu Keith anaendelea kunisubiri au? Asahau! Mimi siwezi kuwa na bwana mmoja. Kwanza ukila ugali kila siku utachoka, siku nyingine kula wali, ukiuchoka, kula pilau, nalo ukilichoka, nyonya koni,” alijisemea huku akiirambaramba midomo yake kama mwanamke aliyepewa ahadi ya kukutana na mwanaume kwenye nyumba ya wageni.
Wakati yeye akifikiria hayo yote, upande wa pili Keith alikuwa na hasira kali, hakuamini kama kweli Fareed alikuwa amemtenda kiasi hicho na wakati alikuwa ametumia kiasi kikubwa cha fedha kumgharamia.
Hakukubali, moyo wake ulijaza ghadhabu nzito na alikuwa tayari kufanya lolote lile kumshughulikia mwanaume huyo.
Alimtafuta, aliwaagiza vijana wake kila kona hapo Los Angeles kumtafuta na kumleta kwake. Vijana hao wakafanya kazi usiku na mchana, wakazunguka katika Cassino mbalimbali lakini hawakuweza kumuona. Hawakuishia hapo, wakazunguka kwenye miji mingine lakini napo hawakuweza kumuona kitu kilichowapa maswali mtu huyo alikuwa wapi.
“Tumemtafuta sana! Hatujamuona!” alisema kijana mmoja.
“Sawa. Ngoja nimpigie wakala wake,” alisema Keith na kumpigia simu Asteria, alitaka kufahamu mahali alipokuwa Fareed ili amuue, hata mapenzi aliyokuwa akiyataka, yakamtoka, hakuwa radhi kuona mtu aliyemgharamia akimchukua mwanaume mwingine.
“Na akisema yupo Tanzania tu, namfuata na kumuua hukohuko!” alisema Keith na kumpigia simu mwanamke huyo. Kwa kuwa Fareed hakumwambia kuhusu kumtoroka Keith, wala kumwambia kwamba alikuwa bwana wake mpya, mwanamke huyo akamwambia kwamba alikuwa Dubai akila maisha na bilionea Saed, maneno yaliyomchoma mno Keith.
“Yaani anakula maisha na mwanaume mwingine. Sasa atanitambua,” alisema Keith! Hapohapo akawapigia simu vijana wake. Alitaka kuzungumza nao, mezani kulikuwa na jambo moja tu. Kumteka Fareed na kumuua.
***
Huko Dubai maisha yalikuwa ni ya raha kabisa, Fareed hakuishia kwa wanaume hao tu, alichokuwa akikiangalia kilikuwa pesa tu. Siku zikakatika huku akiendelea kupata fedha, alilala katika mahoteli makubwa na ya kifahari ambayo alipangiwa na mabwana zake.
Alisahau kabisa kama kulikuwa na shida katika dunia hii, alifurahia kwa kuwa aliona kwamba hakukuwa na kitu alichoshindwa kukifanya kwa sababu alikuwa na pesa ya kufanya kitu chochote kile.
Baada ya wiki mbili akapigiwa simu na mwanaume mmoja, alikuwa mwanaume wa Kizungu aliyemwambia kwamba alitaka kuonana naye, mwanaume huyo alijitambulisha kwa jina la Mickey Downford.
Kwanza Fareed hakutaka kukubali, lilikuwa jambo gumu kukutana na mwanaume huyo, alihisi kwamba hakuwa na fedha za kumpa kwani yeye aliwazoea mabwana wa Kiarabu ambao walikuwa radhi kutoa kiasi chochote cha pesa ili kupata wanachokihitaji.
Kwa kipindi cha wiki nzima Mickey alikuwa akiomba kuonana na Fareed lakini alikuwa akikataa na wakati mwingine alimwambia kwamba hakuzoea kutembea na Wazungu, yeye aliwapenda Waarabu tu.
“Lakini nina pesa!” alisema Mickey kwenye simu.
“Nitaamini vipi?”
“Subiri! Nipe namba yako ya benki,” alisema Mickey na hivyo kupewa namba hiyo.
ITAENDELEA
 
MICHIRIZI YA DAMU -9

Ndani ya dakika kumi, simu ya Fareed ikalia kuonyesha kwamba kulikuwa na ujumbe, haraka sana akaichukua na kuangalia, ilikuwa ni meseji kutoka katika huduma ya kibenki ambayo ilimwambia kwamba alikuwa amepokea kiasi cha dola elfu hamsini, zaidi ya milioni mia moja na nusu kwa fedha za Kitanzania.
Akakaa chini, hakuamini kile alichokuwa amekiona, hakujua kama alitumiwa na mwanaume ambaye alimpuuzia kila alipomwambia kwamba walitakiwa kuonana. Kiasi hicho kilikuwa kikubwa sana kwake, kwa kawaida aliwatoza wanaume kiasi cha dola elfu moja mpaka elfu mbili, kitendo cha kupewa kiasi kikubwa cha fedha kilimchanganya. Wakati akiwa kwenye hali ya furaha, Mickey akampigia simu.
“Nadhani umeona mabadiliko kwenye akaunti yako!” alisema Mickey.
“Nimeona mpenzi!”
“Huo ni mwanzo. Na nimekupa kiasi kidogo kwa sababu tu huniamini!” alisema Mickey.
Kichwa cha Fareed kilichanganyikiwa, hakuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa amemtumia kiasi kikubwa cha fedha. Hapo ni kwamba hawakuwa wamekutana na kuzungumza, hawakulala kitandani alimgawia kiasi hicho cha fedha, kama angemfanyia kama wengine angepata kiasi gani?
Alipojiuliza, akajikuta akianza kuvutiwa na Mickey. Hakutaka kubaki hotelini, haraka sana anawasiliana na mwanaume huyo kwa miadi ya kuonana na kumwambia kwamba walitakiwa kuonana sehemu tulivu, katika ufukwe wa Kite uliokuwa Magharibi mwa mji huo.
Ndani ya saa moja, tayari Fareed alifika mahali hapo. Alikuwa akiangalia huku na kule akimtafuta mwanaume aliyekuwa amepanga naye miadi ya kuonana.
Baada ya dakika kadhaa, akaliona gari la kifahari, Bugatti la watu wawili likifika mahali hapo. Alilikodolea macho, lilikuwa gari la gharama kubwa na ilionyesha kwamba mtu aliyekuwa humo ndani hakuwa wa mchezomchezo kuhusu masuala ya pesa.
Mlango ukafunguliwa, ukafunguka kwa kwenda juu na mwanaume mmoja aliyevalia suti kuteremka. Watu wote waliokuwa katika ufukwe huo walikuwa wakimwangalia, hawakuamini kama kijana mdogo aliyeteremka ndiye aliyekuwa akiendesha gari hilo la kifahari.
“Mmh! Kuna watu wana hela bwana!” alijisemea Fareed, hakuwa amejua kwamba mwanaume huyo ndiye alikuwa Mickey aliyekuwa akimsubiri.
Moja kwa moja Mickey akaifuata meza ya chakula iliyokuwa katika eneo la kulia chakula, akachukua simu yake na kumpigia Fareed kwa ajili ya kumpa taarifa kwamba alikuwa amefika.
“Mbona sikuoni?” aliuliza Fareed.
“Unaliona hilo gari lililosimama hapo ufukweni?”
“Ndiyo! Hili la kifahari?”
“Yaap!”
“Sasa wewe upo wapi?”
“Umemuona dereva aliyeteremka?”
“Ndiyo!”
“Huyo ndiye mimi!”
“Ndiye wewe? Unaendesha Bugatti?”
“Yeah! Naomba unifuate! Bila shaka unajua hapa nilipokuja kukaa,” alisema Mickey na kisha kukata simu.
Fareed hakuamini, alimdharau mwanaume huyo lakini kumbe alikuwa bilionea mkubwa tu. Wakati anapiga hatua kuelekea kule kulipokuwa na meza ile, macho yake hayakuacha kuliangalia gari lile, lilimpagawisha na kujiona kama yeye ndiye mmiliki halali.
Alipofika katika meza hiyo, kitu cha kwanza Mickey akasimama na kumkumbatia. Ilikuwa vigumu kuamini kama mtu huyo alikuwa mwanaume kwani alivalia gauni refu, kilemba na nyuma alijazia kwani zile sindano alizokuwa amechomwa zilifanya kazi vizuri na hata kifua chake kilijaa.
“U mzuri sana,” alisema Mickey huku akimkumbatia Fareed.
“Nashukuru sana mpenzi!” alisema Fareed, akatoa tabasamu la kike na kutulia kwenye kiti.
Walizungumza mambo mengi huku Mickey akimwambia kwamba alikuwa bilionea kutoka nchini Australia na alifika hapo kwa ajili ya mambo yake ya biashara ila alipomuona klabu siku za nyuma ndizo zilimpagawisha na kuitafuta namba yake ambayo kwa maelezo yake alimwambia kwamba aliinunua kutoka kwa mtu kwa dola elfu mbili.
“Jamaniiiii!”
“Ndiyo ukweli!”
Walizungumza mambo mengi mno huku muda wote Mickey akizungumza kama bilionea mkubwa. Walichukua saa moja, walipomaliza, wakaelekea katika Bugatti ile, wakaingia na kuondoka mahali hapo.
Njiani, Fareed alipagawa mno, moyo wake ulijuta kutofahamiana na mwanaume huyo tangu kitambo kwani alikuwa mzuri wa sura na kubwa zaidi ni kwamba alikuwa na pesa kitu kilichokuwa ugonjwa wake mkubwa kama mtu aliyezaliwa benki.
Wakafika hotelini, Mickey hakutaka kuwa na haraka, aliamini kwamba huyo alikuwa wake hivyo alichokiifanya ni kumuacha huku akimpa dola elfu mbili na kuondoka zake pasipo kufanya kitu chochote kile.
Fareed alichanganyikiwa, alipoingia hotelini, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo tu. Hakuamini kama kweli alikuwa amefanikiwa kuwa na mtu aliyekuwa na pesa, ambaye hakuwa mchoyo kama alivyokuwa Mickey.
Akaanza kuwa msumbufu, kila wakati alikuwa akimpigia simu mwanaume huyo na kumuuliza alikuwa akiendeleaje, alitaka kuonana naye na kumpa haki yake na si kutumia pesa zake tu.
“Tutaonana tu mpenzi kabla sijarudi Australia! Utakuwa na nafasi usiku wa leo nikufuate twende klabu?” aliuliza Mickey.
“Yeah! Tena nitakuwa mpweke sana. Naomba uje kunichukua mpenzi!” alisema Fareed.
“Sawa. Nitakuja!” alisema Mickey na kukata simu.
Usiku huohuo Mickey akafika hotelini hapo, hakutaka kuchelewa, akamchukua Fareed na kuondoka naye. Walizungumza kama wapenzi, aliongea kama mwanamke na hata mapozi aliyokuwa akiyafanya pale kitini alipokaa alikuwa kama mwanamke.
Saa 8:12 usiku Mickey akamrudisha Fareed hotelini na kisha kuondoka zake. Njiani, hata kabla hajafika katika hoteli aliyochukua chumba, akachukua simu yake na kupiga upande wa pili ambapo baada ya sekunde kadhaa, ikapokelewa.
“Umefikia wapi?” iliuliza sauti ya upande wa pili.
“Kila kitu kipo poa. Kama itawezekana basi kesho tumuue,” alisema Mickey.
“Haina shida. Waambie wenzako kesho mfanye hayo mauaji! Au subiri mpaka nije. Kesho jioni nitaingia, nitahakikisha namuua kwa mkono wangu,” alisema mwanaume upande wa pili na kisha kukata simu.
***
Keith hakutaka kubaki nchini Marekani, aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine ilikuwa ni lazima Fareed afe kama alivyokuwa amepanga hivyo ilikuwa ni lazima aondoke na kuelekea Dubai.
Njiani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mwanaume huyo, aliuumiza moyo wake vilivyo, alitumia kiasi kikubwa cha fedha kumlea lakini kama kunguru vile alishindwa kufugika kabisa.
Aliamua kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuua ili kuupa furaha moyo wake. Wakati mwingine aliiona ndege ikienda taratibu sana, alitamani hata kuiongezea kasi kwani ilikuwa ni lazima afike mapema, amuue Fareed na kurudi zake nchini MArekani.
Baada ya saa zaidi ya ishirini, ndege ikatua uwanja wa ndege ambapo moja kwa moja akaondoka na kuelekea hotelini. Akawasiliana na Mickey, kijana wake aliyempa kazi ya kufanya mauaji na kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima waonane hotelini na vijana wenzake kwa ajili ya kupanga ni kwa namba gani wangeweza kufanya mauaji hayo.
Ndani ya dakika ishirini, vijana wote walikuwa hotelini humo. Akazungumza nao na kuwaambia mipango iliyokuwepo, wakajadili ni kifo cha namna gani mwanaume tata huyo alitakiwa kufa, wakakubaliana kwamba ilikuwa ni lazima abakwe, aingizwe kwenye boti, iende katikati ya bahari huku akiwa amefungwa miguu kwa jiwe kubwa kisha kufa hukohuko.
“Sawa. Wewe endelea kuwasiliana naye,” alisema Keith.
Hapo akawa na amani moyoni mwake, Mickey hakuwa na hofu alijua kwamba Fareed hawezi kutoka mikononi mwake hivyo ilikuwa ni lazima kufanya kama alichoambiwa.
Ili kumtia mshawasha Fareed, siku hiyo alizima simu siku nzima kitu kilichomnyima raha Fareed na kumpigia kila wakati lakini simu haikuweza kupatikana.
Ilipofika saa moja usiku na Fareed kupiga simu, ikawa inaita, mapigo yake ya moyo yakawa juu, hakuamini kama kweli simu hiyo ilikuwa hewani. Alikumbuka Mickey, hakujua kama mwanaume huyo alikuwa mtu mbaya aliyetaka kumuua baada ya kumbaka yeye na wenzake.
Kitendo cha Mickey kupokea simu, Fareed akaanza kuongea kwa sauti ya kulialia kwani alitaka abembelezwe sana, apozwe kama mwanamke aliyekuwa akihitaji faraja kutoka kwa mwanaume aliyekuwa akimpenda kwa dhati.
“Nisamehe mpenzi! Nilikuwa sehemu fulani hivi,” alisikika Mickey kwenye simu.
“Nimekukumbuka jamani! Mpaka nikataka nijiue kwa ajili yako,” alisema Fareed kwa sauti yake ya kuwapagawisha wanaume.
Wakazungumza mengi na mwisho wa siku wakakubaliana kwamba lingekuwa jambo jema kama wangekutaka katika Klabu ya Dubai Night kwa ajili ya kuburudika na kuzungumza mengi. Hiyo ilikuwa furaha kwa Fareed kwani kitu pekee alichokuwa akikitaka kwa kipindi hicho ni kuonana na mwanaume huyo tu.
“Nakuja bebi!”
“Sawa.”ITAENDELEA
 
d0de2ceb25e04c44a234478beb4f50fc.jpg
 
Nakusalimia sana kapuku uliyeamshwa na uzima kwa siku ya leo na hii salam inaenda sambamba na shukrani za dhati kwa anko wangu Obe usiku wa jana kukulaza na kitu cha fally ipupa akipendacho BlessedHope...ata mama d najua alienjoy japo bahati mbaya baada ya kuweka mziki anko wangu alinyanganywa simu na kibonge wake make kafanya usajili mpya na kujifanya mtu mwema kwake ndo kaamua lain yake wanayomsumbua wengi hasa wale wahamiaji haramu anipe mimi nipambane kwa niaba yake ....huyo ndo anko

Soon kitu UF chawajia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom