MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 12
ENDELEA.......
Sheby akiwa na furaha ya kwenda india peke yake, huku akianza kuwaandaa akina zaituni na shadi kwa ajili ya safari, na sababu ya kusafiri na shadi ni ili kwenda kutoa msaada mdogo mdogo kwa zai, pale atakapokuwa hospitali, hivyo ndio mana mpaka shadya kaombwa aende nae,...
Wakati kijana huyo anapanga begi la nguo katika gari, ghafla simu yake ikaita, kuangalia jina alikuwa ni baba yake mzazi... Aliipokea na kumuuliza
"haloo mzee, kuna nini tena"
"subiri hapo hapo nakuja twende, nimepewa ruksa na dokta mkuu,.. Hivyo kuliko nibaki, ni bora twende wote"
Sheby alishangaa nani kampa ruksa mzee wake, na hapo ndio kwanzaa hata Airport hawajafika, na akitangulizana na baba yake itabidi zai na shadi wabaki,...
"sasa mzee, mbona mi nimeshaondoka na ndege ya saa 12,.. Yaani nipo mbali mno"
"aaahhhhhh shit, kwanini uwahi kiasi hicho"
"mambo ya kazi mzee, lazima ubembeleze kazi"
"shit.... Aaahhhh"
Simu ilikata, sasa sheby bila kuchelewa alipaki vitu haraka haraka katika gari,...
Nusu saa mbele wapo Airport,.. Maskini shadi hajawahi hata kufika Airport, yaani licha ya kupanda ndege, bali hata kufika Airport hajawahi... Zaituni yeye ndio kwanza hata hajui hapo tupo wapi,.. Sheby bila kuchelewa alifanya taratibu zote za usafiri mana yeye ni mzoefu kiasi flani mana sio mara ya kwanza kusafiri kwa ndege,... Baada ya muda mfupi walikamilisha kila kitu,.. Mpaka hapo zaituni hajui yupo wapi, ila anajua kuwa tunasafiri lakini hajui ni usafiri gani wanaoutumia kwa wakati huo,....
Shadya yeye ndio aliokuwa akiona kila kitu,.. Lakini katuliaaa, kama maji ya mtungi vile
Tukija huku ofisini kwa akina sheby, na leo ndio siku ya kuanza kazi wale akina mary na rose, mana tayari walishafundishwa na kijana sheby wameiva vizuri ila wanaingia kazini pasina mwenyeji wao ambae ni sheby,... Mapokezi iliwapokea na kuwaonyesha vitengo vyao mana kazi walishapata wiki iliopita sema wakadanganyiwa na sheby kiwa walipata msiba, hivyo waende msibani kwanza misha warudi kuendelea na kazi,.. Lakini haikuwa msiba kweli, bali ilikuwa ni ujanja ujanja wa kijana sheby ili awafundishe kazi, hivyo mpaka sasa wadada hao wameshajua kazi na leo ndio siku ya kuanza kazi,
"karibuni"
Alikuwa ni Secretary ndie aliewakaribisha katika ofisi zao wanazotakiwa kufanyia kazi.. Secretary aliwapeleka mpaka kwa boss mkubwa ambae ni baba yake na kijana sheby
"boss? hawa ni wale wasichana wa juzi"
"ooohhh sawa sawa kabisa,.... Habari zenu"
"salama boss shkamoo"
"marahaba hamjambo"
"hatujambo boss"
"ok... Poleni sana na msiba"
"tumeshapoa boss"
Akina rose na mary walikuwa na heshima mno kwa baba yake na sheby, mana mzee huyo ni mkali sana katika kazi zake...
"aaahhhh amina unaweza kuwapeleka katika ofisi zao,.... Na chumba ni kimoja ila chumba hicho kina patision (kimegawanywa) hivyo kila mtu na ofisi yake"
"sawa boss, ahsante"
"naombeni kazi ifanyike, sitaki mchezo na kazi"
"sawa boss"
Secretary aliwapeleka akina mary mpaka ofisini kwao, na kuwaelekeza baadhi ya vitu vidogo vidogo vya hapo ofisini... Mpaka hapo rose na mary wameshapata kazi
Tukija huku kwa mama yake na sheby akiwa nyumbani kwake na mama yake mkwe aliomtembelea kwa siku hio,...
"kweli mama kuna kitu kinaniuma sana katika moyo wangu"
Aliongea mama yake sheby huku akitamani hata kulia
"kuna nini tena mama"
Aliingea bibi yake sheby ambae ni mama wa baba yake na sheby,..
"baba sheby anataka kumpa mke sheby na umri huo kweli"
Aliongea mama huyo huku akitamani hata kugombana kwa swala la mume wake kutaka Sheby aoe,..
"lakini mbona mjukuu wangu ni mkubwa tu"
"mama??.. Miaka 22 ni mkubwa kweli, mjukuu wako bado mdogo mama"
Mwajabu hataki kabisa mtoto wake aoe na umri huo, mana anaona bado ni mtoto mdogo sana na umri wa kuoa bado haujafika,..
"hata mimi sijapenda, lakini kumbuka baba ni baba mwanangu, kama kaamua hivyo sawa,.. Wacha mtoto azoee maisha ya ndoa mapema, mana kama ni pesa mnazo sasa mwahofia nini"
"lakini mama, huyo mschana ni mkubwa, yaani hata mwanangu rehema ni mdogo kabisa yani"
Rehema ni mtoto wa kwanza kwa huyu mama yake sheby... Na sheby ni mtoto wa pili, kisha anafuata Rajabu akiwa ni mtoto wa mwisho katika familia hio...
"mmmhhh kwanini lakini afanye hivyo"
"mimi sijui,... tena nilitaka kuja nyumbani kukupa habari hizi, lakini mmhhh"
"mwajabu, punguza hasira, ngoja nitaongea nae vizuri"
"sawa mama"
Moyo wa mama huyo ulitulia baada ya mama mkwe wake kusema kuwa ataongea nae vizuri
BAADA YA MASAA 10 KUPITA
Na sasa akina sheby wakiwa ndio wanaingia ndani ya hospitali hio yenye matibabu ya kimataifa,.. Walipokelewa vizuri sana lakini sasa sheby alikuwa anatafuta njia ya kuwakabidhi hapo hospitali ili atoke kufuata kazi iliomleta huku india, mana kuja hospitali ni ziada yake tu, lakini kikubwa ni kazi, na huko kwenye kampuni wanafunga mida ya saa 11 hivyo akichelewa tu, imekula kwake.. Zaituni alichukuliwa na kupelekwa katika wodi ya wagonjwa wa macho, alianza kufanyiwa vipimo na madaktari bingwa katika hospitali hio,
"ivi dokta, kuna uwezekano wa kupona kweli?"
"aahhh mbona hajaathilika sana huyu, kunaletwa wagonjwa hapa mpaka tunahaha, lakini nimempima huyu ni lazima apone"
Aliongea dokta huyo huku akiahidi kupina kwa zai...
Huku india kiukweli kila kona anayopita kinana sheby kulitakiwa kuandikwe kwa Kingereza, lakini ili nisiwachanganye mashabiki zangu katika kusoma.. Basi itabidi niandike Kiswahili, lakini ilitakiwa Kingereza kwa huku india, hivyo hata sheby anapoongea anaongea Kingereza lakini mwandishi kaifanya tu kama kiswahili tu....
"itachukuwa siku ngapi"
"wiki moja tu"
"aahhh ok sawa"
Wakati sheby anaendelea kuongea na dokta, ghafla simu yake iliita, kuangalia jina alikuwa ni mr mageshi, tajiri mwenye mzigo unaotakiwa kufika dubai
"ndio mkuu"
"mbona hufiki, muda unakwenda huu"
"ok nafika hapo mara moja"
Kijana sheby alimaliza kila kitu hapo hospitali, lakini ilikuwa ni kisiri siri hata shadi hajaona pesa ilivyotoka,.. Alipomaliza kulipa malazi ya wiki nnzima mpaka matibabu yote,.. Alimfuata shadya..
"sasa mama, chukuwa hii laki moja kwa ajili ya kulinda mfuko.. Mana chakula malazi kila kitu ni hapa hapa, hivyo kaa karibu na mgonjwa"
"sawa kaka... Sasa unaenda wapi.. Mana mi mwenzio sijui wanavyoongea hawa watu"
Sheby ndio anastuka kuwa kumbe shadya hajui kuongea hata Kingereza, duu kazi ilikuwepo kwa kijana sheby
"kwaioooo, dahh, lakini sio tabu mimi narudi sasa hivi"
"sawa usichelewe basi"
Aliongea shadya huku akiingia katika chumba cha kulala ambacho ni kama hostel humo humo kwa ajili ya wauguzi wanaowaseidia wagonjwa wao...
Sheby aliingia mahari na kubadiri nguo zake za kawaida kisha akavaa nguo za asili yake,.. Mara moja anachukuwa tax iliomfikisha katika kampuni ya mr mageshi,..
"yes boss"
"umechelewa sana lakini hakuna shida"
Aliongea mr mageshi huku wakielekea katika godown lenye mashine inayotakiwa kusafirishwa,..
"sasa kama unavyoiona Mashine ni kubwa na itatakiwa kusafirishwa na ndege kubwa"
"ookee na documents zote zipo tayari"
Sheby aliuliza kana kwamba alitamani sana kuambiwa bado,
"ndio, hapa ni wewe usaini, kisha niite ndege ije ipakie mzigo uondoke"
Aahhh kijana alichoka baada ya kusikia kila kitu kipo tayari,..
"ok nadhani kesho itatakiwa ifike dubai"
"yes, yes,.. Tena ina haraka sana"
"ok unaweza ita ndege ije kupakia"
"malipo yao unayo kabisa"
"ndio"
Haikupita muda ndege kweli imefika mpaka katika kiwanda hicho kinachotengeneza injini za vyombo vyote duniani, hivyo kuna injini ya meli toleo jipya, ambayo ina injini nne ndani lakini zipo sehemu moja, mana ndege na meli hua zinakua na injini zaidi ya moja, lakini hii ni moja lakini imekusanya injini nne,.. Ina ukubwa wa nyumba yenye rumu mbili...
"imeshalipiwa vibali vyote"
Sheby alizidi kuuliza ili tu kimoja wapo kikosekane aweze kuendelea kuwepo karibu na hospitali...
"kila kitu, yaani ni wewe kupanga unaondoka saa ngapi"
"itabidi niondoke kesho"
Sheby alikwenda kuongea na wahusika wa ndege kuhusiana na usafirishaji..
"kiasi cha transporter kinakwenda vipi"
"milioni mia mbili"
"duuuuu... Mr mageshi.. 200 milion from here to dubai?"
"tena hapo umefanyiwa fea sana, wanachajiwaga mpaka 300"
"mmhhh ok, tutaondoka kesho saa mbili"
Kila kitu kilienda sawa, malipo ya usafiri,.. Mashine yenyewe inauzwa bilioni 15 za kitanzania, na hapo ni tofauti na usafirishaji,.... Hivyo bilioni 5.7 watalipwa akina sheby kwa kufisha mzigo na kufanya kila kitu mpaka mzigo kufika eneo husika..
Mara moja baada ya kila kitu kwenda sawa, sheby alisaini mikataba yote kila kitu, kasoro mkataba wa pesa ndio bado hajasaini...
Baada ya kufanya hivyo kifuatacho ni kwenda hospitali,.. Alipofika alimkuta zaituni kafungwa mabandeji katika macho yake,..
"usijali mgonjwa wako atatoka salama"
Aliingea dokta huku akiendelea kufanya mambo yake ya kidokta,..
"ok hakuna shida.... dokta, kuna yule mschana nilikuja nae hapa atakuwa kalala"
Aliuliza hivyo kwasababu ilikuwa ni kagiza kameshaanza kutanda,..
"kwani ulikuja na mschana mwingine"
"ndio, mweupe mweupe hivi"
Mara ghafla kuna nesi kaja na kusema kuwa
"kuna mschana wa kiafrika yupo mochwari"
"unasemaje wewe nesi??"
Sheby alishtuka kwa kusikia hivyo, hata mapigo yake ya moyo yalianza kwenda mbio
"ndio.. Alidondoka baada ya kuona mtu kajeruhiwa vibaya, alifanyiwa vipimo vyote, lakini ameonekana keshapoteza maisha"
"Mungu wangu shadya wa watu"
Sheby alilalamika huku akipelekwa chumba cha watu waliokufa (mochwari)..
"si ndio huyu hapa"
Aliongea dokta mmoja huku akinyoosha kidole, kuashiria ndio huyo waliokuwa wakimsemea... Kijana sheby alitoa macho kama mjusi aliobanwa na mlango
"mungu wangu... shadya wewe, nitakwenda kujibu nini kwenu mimi"
Sheby aliongea hivyo huku akiinama chini, kumkagua vizuri.... Lakini sheby akiwa anaendelea kumkagua shadya pale chini, ghafla simu yake inaita, kucheki jina alikuwa ni baba yake..
"haa... Ha... Haloo mzee"
Kinana aliipokea na kusema haloo lakini huku akiwa na kwikwi za kulia
"we una nini mbona unalia?? ... Afu mbona GPS yaxngu inanionyesha upo hospitali ya india, umefata nini huko"
Je? Nini kitaendelea??...