Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Huchoki Kusikiliza

Sitaki kusema sana leo, na nikishakusalimia tu naweka muziki ambao hauchoshi kusikiliza maana una jumbe nzuri na vyombo vimepangwa kwa ustadi mzuri. Sijaongelea sauti hapo bado, sauti ya studio ni tofauti na sauti ya mjomba wangu ambaye bila kuuma maneno ana sauti kama 700 na kila moja inaendana na nyumba zake nyingi. Inategemea muda huo atakuwa anaongea na nyumba ipi. Usishangae, huyo ndo mjomba wangu.

Sijaanza kukusalimia, nina salamu ndefu kama reli na kwa kuwa serikali inajipanga kujenga reli wanaiita SGR basi salamu yangu itakuwa fupi sana. reli ya mwendo kasi. Hebu ngoja kwanza, hivi hii reli imeshaanza? Maana anko wangu yule mdogo wa dar, sio huyu aliyeamua kuweka makazi Moshi mjini. Alisema reli ipo, ndo wanaijenga. Sijui kama ni kutaka kutudanganya au nini, mteja hajali masuala ya kiufundi, kama hii reli ni mafdanikio mbona hatuioni kwenye 'barabara' yake?!!

Muziki sasa, asante shululu kwa magazeti, asante mpenzi wangu husna muba kwa hadithi, asante Shunie aunty yangu ninayependa kukuona unafurahi kila wakati maana una moyo mvumilivu. Asante BlessedHope kwa sala za wakati wote, yaani unatuombea wote hadi makaveli10 na zaidi, asante wewe kapuku unayekuwa hapa maana bila wewe jukwaa hili si chochote lolote popote





...sasa hivi ni usiku sana kukusalimia. Nitakusalimia asubuhi nikishajiswaki

Shukrani mopao..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom