Makapuku Forum

Makapuku Forum

Seven Days In Hell (Siku Saba Kuzimu)- 6 AZIZ HASHIM
ILIPOISHIA:
Mara simu yake ilianza kuita mfululizo, akaishika na kutazama namba ya mpigaji lakini katika hali ambayo sikuielewa, aliiachia simu hiyo, ikadondoka chini na kufunguka betri ikaangukia kivyake, mfuniko kivyake na simu nayo kivyake. Akaanza kuangua kilio kwa uchungu huku akiniomba nimsaidie, nilibaki nimepigwa na butwaa.

SASA ENDELEA…
“Nikusaidie nini Shenaiza?” nilimuuliza huku nikiiokota ile simu na kuiunganisha upya.
“Nakuomba usiniache, fanya kila kinachowezekana unitoroshe hapa hospitalini usiku huuhuu, watakuja kunimalizia,” alisema msichana huyo na kuzidi kunichanganya.
“Watakuja kukumalizia? Akina nani? Na Kwa nini tutoroke wakati hali yako bado siyo nzuri?”
“Naomba ufanye nilichokuomba mengine utaenda kuyajua mbele ya safari,” alisema msichana huyo huku akiendelea kulia.
Nikiwa bado nimeduwaa, nikiwa sijui cha kufanya, nilishtuka kumuona akichomoa sindano ya dripu aliyokuwa amechomwa mkononi mwake na kusababisha damu zianze kumtoka mkononi, akajikongoja huku akionesha kuwa na maumivu makali, akanitaka nimpe bega langu ili apate balansi ya kutembea.
Sikuwa na cha kufanya zaidi ya kukubaliana na matakwa yake, japokuwa nilikuwa najua kwamba ninachokifanya ni hatari sana lakini sikuwa na namna zaidi ya kumsaidia msichana huyo ingawa mpaka muda huo sikuwa najua nini kinachomsumbua.
Huku damu zikimvuja na kudondokea sakafuni, nilimsaidia kutembea, tukatoka mpaka nje ya wodi hiyo huku mara kwa mara nikigeuka nyuma kutazama kama hakuna mtu aliyekuwa akitufuatilia.
Kwa bahati nzuri, kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, madaktari wengi walishaondoka sambamba na manesi ambapo waliosalia walikuwa ni wale wenye ‘shift’ ya usiku ambao nao hawakuwa wengi.
“Heeei! Mnakwenda wapi usiku wote huu,” mwanaume wa makamo ambaye bila hata kuuliza tulijua ni mlinzi wa hospitali hiyo kutokana na kuvalia sare huku mkononi akiwa na kirungu, alituuliza huku akifunga geti la kutokea nje.
Ilibidi nimdanganye kwamba nilimleta mgonjwa wangu kutibiwa majeraha aliyoyapata kwenye ajali lakini hatukumkuta daktari kwa kuwa alishaondoka, nikamdanganya kwamba tunaenda kujaribu kwenye hospitali nyingine lakini hakutaka kuelewa. Akasema hawezi kuturuhusu kutoka mpaka tupate kibali kutoka kwa daktari aliyekuwa zamu usiku huo.
Shenaiza ni kama alijua kilichokuwa ndani ya akili yangu kwani alianza kuugulia kama anayesikia maumivu makali, nikatumia kigezo hicho kuendelea kumshawishi yule mlinzi aturuhusu na alipozidi kukomaa, nilichomoa noti moja ya shilingi elfu kumi na kumshikisha, nikamuona akiachia tabasamu na kututaka kuwa makini.
Akafungua geti ambapo breki ya kwanza ilikuwa ni kwenye kituo cha teksi kilichokuwa nje ya hospitali hiyo, tukaingia kwenye teksi moja na kuondoka huku nikimuelekeza dereva kutupeleka nyumbani kwangu, Mikocheni.
Kwa kuwa ulikuwa ni usiku na hakukuwa na foleni, haikutuchukua muda mrefu tukawa tayari tumeshawasili Mikocheni, nilipotaka kumlipa dereva teksi fedha zake tulizokubaliana, Shenaiza ambaye muda wote alikuwa amejilaza huku kichwa chake akiwa amekiweka kwenye mapaja yangu, aliniambia nisilipe.
“Nina fedha za akiba kwenye pochi yangu ndogo, hebu fungua,” aliniambia, kweli nikafungua pochi yake ndogo aliyokuwa ameiweka kwenye mfuko wa gauni refu alilokuwa amelivaa. Nilipoifungua, nilishangaa kukuta kuna noti kadhaa za dola miamia za Kimarekani na noti mbili za shilingi elfu kumi, zote mpya.
Nikatoa na kumpa dereva na kutaka kurudisha pochi mahali pale lakini aliniambia kwamba nikae nayo mimi, nikakubali na kuiweka kwenye mfuko wa suruali niliyokuwa nimeivaa.
Wakati wa kushuka, kama ilivyokuwa wakati wa kupanda, ilibidi yule dereva teksi anisaidie kumtoa Shenaiza ambaye bado alikuwa akiugulia maumivu makali, akapitisha mkono wake kwenye bega langu na nikawa namsaidia kutembea kuelekea ndani kwangu.
Nilifungua mlango na kumkaribisha ndani, japokuwa alikuwa kwenye maumivu makali, nilimuona akiachia tabasamu hafifu kisha akanisifia: ”Mh! Jamani wewe msafi hadi raha, inatakiwa umpate mwanamke msafi kama wewe ndiyo awe mke wako ndiyo mtaendana,” alisema huku akikodolea macho huku na kule ndani ya sebule yangu.
Japokuwa sikuwa nimeoa lakini hakuna kitu nilichokuwa nakipenda kama kuiweka nyumba yangu katika hali ya usafi, kuanzia sebuleni mpaka chumbani huku nikinunua vitu vingi vya kisasa.
Nilimsaidia Shenaiza kukaa pale sebuleni kwenye sofa kisha nikamvua viatu alivyokuwa amevaa pamoja na koti alilovaa juu ya gauni lake na mtandio aliokuwa amejizibia lile jeraha la kichwani.
“Shenaiza mwenzio naogopa kulala na wewe ukiwa kwenye hali hiyo, ukizidiwa usiku itakuwaje? Kwa nini tusiende hospitali nyingine? Hapa siyo mbali na Hospitali ya Kairuki,” nilimwambia lakini alikataa katakata na kuniambia kwamba hospitalini haikuwa sehemu salama kwake kwa wakati huo.
“Basi kuna rafiki yangu anaishi hapo mtaa wa pili ni daktari lakini bado hajaajiriwa, anafanya ‘field’ hapo Kairuki, unaonaje nikamuite aje kutusaidia?”
“Hapana usijali, nitakuwa sawa kwa sababu kama ni damu nimeshaongezewa ya kutosha, ondoa hofu,” alisema huku akiinua mkono wake taratibu na kunigusa kwenye shavu langu la upande wa kushoto, akawa ananivutia pale alipokuwa amekaa.
Kwa tahadhari kubwa nikiogopa nisije nikamtonesha majeraha yake, niliulanisha mwili wangu, akanivutia mpaka nilipomsogelea kabisa, akanibusu kwenye shavu langu na kuninong’oneza.
“Ahsante sana kwa msaada wako, ni Mungu pekee ndiye atakayekulipa, upo tofauti sana,” nilitabasamu na kumtazama, macho yetu yakagongana, naye akaachia tabasamu hafifu.
Kwa kuwa sikuwa nimekula chochote, ilibidi nimuage kwamba naenda kubahatisha kama nitapa chipsi kwenye banda lililokuwa mtaa wa pili kutoka pale nilipokuwa naishi. Nilitoka huku Shenaiza akinisisitiza niwahi kurudi pia nifunge mlango kwa nje ikiwa ni pamoja na kuzima taa zote. Sikujua kwa sababu gani bado alikuwa na hofu kubwa kiasi hicho. Nilifanya kama alivyoniambia na kutoka, nikafunga mlango kisha nikafunga na geti la chuma kwa nje na kuondoka kuelekea mtaa wa pili.
Kwa bahati nzuri nilikuta bado hawajafunga, nikaagiza chipsi sahani mbili na vipande vya kuku kwani nilitaka nikambembeleze Shenaiza naye ale japo kidogo. Dakika kadhaa baadaye chakula changu kilikuwa tayari, nikalipa na kuanza kuondoka huku nikijitahidi kutembea haraka kwani nilipoteza muda mwingi pale kusubiria chakula.
Katika hali ambayo sikuitegemea, nilipotokeza kwenye uchochoro wa kuelekea kwangu, kwa mbali niliwaona wanaume kama watatu hivi wakiwa wamesimama mlangoni kwangu, mmoja akiwa anagonga mlango kwa nguvu.
“Mungu wangu, akina nani tena hao usiku wote huu?” nilijiuliza huku nikirudi nyuma na kujibanza pale uchochoroni, nikawaona wale wanaume wakiendelea kugonga mlango kwa nguvu. Ugongaji wao ulionesha dhahiri kwamba hawakuwa wamekuja kwa heri, nikawa natetemeka nikiwa sijui nitafanya nini.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Engine ya fiat au?

Kwanza mnaongelea nini, nisije kumkwaza mpenzi wangu.
Afu anko unasalimiwa na anko mkubwa akiwa pande za Moshi, anasema mbona kimya kimezidi?
Anko engine ya scania buldoza ....


Sasa anko mbona kama husobe ana michepuko mingi ? Kwenye kamati yenu anko hajawahi kujiandikisha ??


Moshi alafate nini wakati shunie anakaa boko au kuna moshi ya boko
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 7 AZIZ HASHIM
ILIPOISHIA:
“Mungu wangu, akina nani tena hao usiku wote huu?” nilijiuliza huku nikirudi nyuma na kujibanza pale uchochoroni, nikawaona wale wanaume wakiendelea kugonga mlango kwa nguvu. Ugongaji wao ulionesha dhahiri kwamba hawakuwa wamekuja kwa heri, nikawa natetemeka nikiwa sijui nitafanya nini.
SASA ENDELEA…

Mlango uliendelea kugongwa kwa nguvu, nikiwa nimejibanza palepale, nikitetemeka mno kwa hofu kwani nilishaona hatari iliyokuwa mbele yangu. Niliwaona wale watu wakijadiliana na muda mfupi baadaye, mmoja kati yao aliondoka eneo hilo. Muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amemkwida mtu ambaye nilipomtazama, nilimtambua haraka kuwa ni yule dereva teksi aliyetuleta.
Japokuwa sikuwa nasikia walichokuwa wakikizungumza lakini ilionesha wazi kwamba walikuwa wakimshinikiza awahakikishie kama pale ndipo tulipoingia.
Nikamuona akijitetea na kusisitiza kuwa ni penyewe, kufumba na kufumbua nilimuona mmoja kati ya wale watu akimpiga ngumi yule dereva iliyosababisha apepesuke na kutaka kuanguka, mwenzake akamdaka na kumsimamisha vizuri, wakawa wanaendelea kumhoji huku yule mwingine akiendelea kugonga mlango kwa nguvu.
Kwa ilivyoonesha, baada ya mimi na Shenaiza kuondoka hospitalini, watu wale walikuwa wakitufuatilia na ndipo walipofanikiwa kumpata dereva aliyetuleta pale nyumbani kwangu na kumteka. Nilijiuliza wale ni akina na nani na kwa nini walikuwa wakitufuatilia?
Niliendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu, nilimlaumu pia Shenaiza kwa kutonieleza ukweli wa kilichokuwa kinaendelea kwani mpaka muda huo, nilikuwa nimenaswa kwenye mtego ambao sikuwa naujua. Sikuwa najua Shenaiza ni nani? Ilikuwaje mpaka akajeruhiwa kiasi kile na aliyemjeruhi ni nani na wale watu walikuwa na uhusiano gani naye! Nilikosa majibu.
Kingine kilichonitisha, kama yule dereva tu ambaye hakuwa na hatia yoyote alikuwa akipigwa kiasi kile, hali ingekuwaje endapo wangenikamata na mimi? Kwa kuwa nilikuwa nimefunga mlango kwa kufuli, tena geti lilikuwa la chuma, niliamini hawawezi kumpata Shenaiza, kwa lugha nyepesi, Shenaiza alikuwa salama mle ndani, tatizo lilikuwa ni kwangu mimi.
Nilichoamua kukifanya kabla hawajanishtukia, ilikuwa ni kuondoka haraka eneo hilo na kwenda kutafuta hifadhi sehemu nyingine salama. Harakaharaka niliondoka, mkononi nikiwa na mzigo wangu wa chipsi na kutembea mpaka mtaa wa pili.
Nilitokezea kwenye kituo cha Bajaj na bodaboda ambapo nilimuita dereva mmoja wa bodaboda ambaye mara kwa mara huwa ananibeba.
“Vipi bro mbona usiku? Siyo kawaida yako!”
“Aah! Chukulia poa, nataka unipeleke Kijitonyama,” nilisema huku nikipanda kwenye bodaboda, nikawa nageuka huku na kule kuhakikisha kama hakuna mtu anayenifuatilia. Kwa jinsi nilivyokuwa natetemeka, ungeweza kudhani nimetoka kumwagiwa maji ya baridi.
Tuliondoka eneo hilo huku nikiendelea kujiuliza maswali yaliyokosa majibu. Sikujua hatma ya Shenaiza pale nyumbani kwangu. Niliamua kwenda Kijitonyama kwa rafiki yangu na mfanyakazi mwenzangu, Justice ili akanipe hifadhi lakini pia anipe ushauri wa nini cha kufanya.
Dakika kadhaa baadaye, tayari nilikuwa nimeshafika Kijitonyama, nikamlipa yule dereva wa bodaboda na kushuka, nikakaza mwendo kuelekea kwenye uchochoro wa kuelekea kwenye nyumba aliyokuwa anaishi Justice.
Kwa kuwa nilijua kwa muda ule watakuwa wameshafunga geti, nilienda kumgongea dirishani.
“Justice! Justice!”
“Mh! Nani tena usiku wote huu?”
“Ni mimi Jamal!”
“Jamal?” alihoji Justice kwa mshtuko, nikamuona akifungua pazia, akiwa ni kama haamini kwamba nimemfuata usiku huo. Alipohakikisha ni mimi, harakaharaka alienda kufungua mlango lakini nilipotaka kuingia ndani, alinizuia:
“Nipo na shemeji yako, vipi kwema utokako?”
“Dah!” nilijibu kwa kifupi, kauli yake kwamba alikuwa na mwanamke usiku huo ilinimaliza kabisa nguvu. Niweke wazi kwamba miongoni mwa matatizo ya rafiki yangu Justice, ilikuwa ni kupenda kubadilisha wanawake kama nguo. Mara kwa mara alikuwa na tabia ya kulala na wanawake tofautitofauti, jambo ambalo binafsi sikulifurahia.
Kibaya zaidi ni kwamba alikuwa akiishi kwenye chumba kimoja tu kwa hiyo akishakuwa na mgeni ndani, inakuwa vigumu kuingia, ikabidi nimwambie atoke ili tuzungumzie nje kwa sababu nilikuwa na matatizo makubwa.
Alirudi ndani kwani kwa muda huo alikuwa amejifunga taulo tu, alipotoka tena, alikuwa ameshavaa nguo.
“Samahani bwana sikujua kama utakuja, nisamehe kwa sababu tunazungumzia nje, si unajua tena,” alisema Justice huku akifunga vifungo vya shati lake, sikupoteza muda ikabidi nimueleza kwa kifupi kilichotokea.
“Mungu wangu, sasa itakuwaje?” alisema akionesha kupatwa na mshtuko mkubwa mno.
“Hata sielewi, ndiyo maana nimekuja kwako kupata ushauri.”
“Umeshaenda kuripoti polisi?”
“Sijaenda kwa sababu hata huyo msichana mwenyewe namna alivyofika nyumbani kwangu, ni kwamba nimefanya kumtorosha tu hospitalini,” nilimwambia lakini akasisitiza kwamba ni lazima twende tukatoe taarifa polisi ili chochote kitakachotokea, polisi wawe wanajua.
Kwa upande fulani nilikubaliana na alichoniambia, hatukuwa na muda wa kupoteza, alirudi ndani kumuaga msichana wake na alipotoka, tulielekea moja kwa moja kituo cha polisi. Kwa kuwa pale alipokuwa anaishi hapakuwa mbali na Kituo cha Polisi cha Kijitonyama au maarufu kama Mabatini, dakika kadhaa baadaye tulikuwa tumefika.
Tukaandikisha maelezo pale kaunta lakini kwa bahati mbaya zaidi, askari aliyekuwa zamu alisema askari wote wametoka kwenda kwenye doria kwa hiyo kama nahitaji msaada wa polisi, nisubiri mpaka warudi kutoka kwenye doria. Kutokana na hali ilivyokuwa, sikuwa na ujanja zaidi ya kubaki kusubiri hao askari warudi.
Kwa kuwa Justice alikuwa na mgeni wake, nilimruhusu aondoke kurudi kwake na kumshukuru kwa msaada aliokuwa amenipa. Akaondoka na kuniacha nimekaa kwenye benchi pale kituoni. Tayari saa ya kwenye simu yangu ilikuwa ikionesha kwamba ni saa sita za usiku.
Kutokana na pilikapilika nyingi, nilijikuta nimekaa muda mrefu bila kushika simu, nilipoishika nilikuta meseji kadhaa kutoka kwa rafiki zangu, moja ikiwa ni kutoka kwa Raya, msichana tuliyekuwa tukifanya naye kazi ambaye alitokea kunizoea sana.
Alikuwa ametuma ujumbe wa kunitakia usiku mwema kama ilivyo kawaida yake, nilishusha pumzi ndefu na kuendelea kutafakari hatma ya maisha yangu. Baada ya kukaa muda mrefu pale kituoni huku kukiwa hakuna dalili yoyote ya askari kuja, ilibidi niage na kuondoka kwa sababu kesho yake nilitakiwa kuwahi kazini kwani kuna kazi muhimu sana niliyokuwa natakiwa kuikamilisha.
Nikiwa naondoka, simu yangu ilianza kuita mfululizo, haikuwa kawaida mimi kupigiwa simu usiku huo, nikaitoa na kutazama namba ya mpigaji. Alikuwa ni Raya, nikashtuka kuona simu yake usiku huo, harakaharaka nikapokea.
“Vipi Jamal, umeshalala?”
“Hapana, bado sijalala Raya.”
“Mbona nakutumia meseji hupokei? Mpaka nimepatwa na wasiwasi.”
“Mh! Samahani kwa kuchelewa kujibu lakini usijali, niko poa na usiku mwema pia.”
“Haya ahsante, nilitaka nisikie tu sauti yako ndiyo nilale. Halafu mbona kama unatembea, unaenda wapi usiku wote huu?”
“Aah! Kuna mahali nimetoka ndiyo narudi nyumbani.”
“Jamal! Umetoka wapi usiku wote huu?” Raya alinibana kwa maswali. Jambo ambalo naomba niliweke wazi kuhusu Raya, japokuwa mimi nilikuwa namchukulia kama rafiki wa kawaida tu, alikuwa na hisia fulani juu yangu ambazo siwezi kuzielezea kwa urahisi.
Kwanza alikuwa anapenda sana kuwa karibu na mimi japokuwa mwenyewe nilikuwa nikimkwepa sana. Tukiwa kazini, alikuwa anapenda muda wa lanchi tutoke na kwenda kula pamoja na ikitokea nimeenda peke yangu, basi atanuna na kukosa raha siku nzima. Pia alikuwa anapenda hata wakati wa kutoka, tuongozane mpaka kituoni, ahakikishe nimepanda daladala kurudi kwangu ndiyo na yeye aende kwao kwani alikuwa akiishi Mwenge ya Mlalakua.
“Nipo Kijitonyama hapa jirani na Kituo cha Polisi cha Mabatini.”
“Please nakuomba tuonane usiku huuhuu, baba na mama wamesafiri tangu juzi, niko mwenyewe tu, nahisi haupo sawa na nahitaji kukusaidia, niambie nikukute wapi, nakuja na bodaboda sasa hivi,” alisema Raya, nikashusha pumzi ndefu.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Engine ya fiat au?

Kwanza mnaongelea nini, nisije kumkwaza mpenzi wangu.
Afu anko unasalimiwa na anko mkubwa akiwa pande za Moshi, anasema mbona kimya kimezidi?
Moshi ipiiii yupo anko wako eti
Anko engine ya scania buldoza ....


Sasa anko mbona kama husobe ana michepuko mingi ? Kwenye kamati yenu anko hajawahi kujiandikisha ??


Moshi alafate nini wakati shunie anakaa boko au kuna moshi ya boko
 
Wenye rangi zao za pepsi mirinda
6aeb37f4dc5353147ac0a7a05a28af7c.jpg
 
SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 8
ILIPOISHIA:
“Please nakuomba tuonane usiku huuhuu, baba na mama wamesafiri tangu juzi, niko mwenyewe tu, nahisi haupo sawa na nahitaji kukusaidia, niambie nikukute wapi, nakuja na bodaboda sasa hivi,” alisema Raya, nikashusha pumzi ndefu.
SASA ENDELEA…

Nilishindwa nimjibu nini Raya, ni kweli nilikuwa kwenye matatizo makubwa na nilihitaji mtu wa kunisaidia lakini nilipomfikiria Raya, nilijikuta nikikosa majibu. Nilikumbuka jinsi msichana huyo alivyokuwa anajitoa kwa ajili yangu, akihitaji ukaribu wangu tu.
Watu wengi walikuwa wakihisi kwamba huenda tupo kwenye uhusiano wa kimapenzi lakini haikuwa hivyo, nilimchukulia kama rafiki wa kawaida tu ingawa hata yeye alikuwa akiwaambia marafiki zake kwamba mimi ndiyo mumewe mtarajiwa.
Mara kwa mara alikuwa akinilazimisha sana aje nyumbani kwangu lakini nikawa nampiga chenga sana na hata akija, nahakikisha sipo peke yangu, namuita rafiki yangu Justice au Prosper kisha tunajumuika wote. Japokuwa alikuwa akionesha waziwazi anavyonipenda, nilikuwa namchukulia kama rafiki tu na sikutaka kabisa uhusiano wetu uvuke zaidi ya hapo.
Hata hivyo, hakuwahi kuchoka, naye akawa ananialika mara kwa mara niende nyumbani kwao lakini sikuwa tayari kwa hilo. Nilijiwekea mipaka kati yetu na kamwe sikutaka tuivuke zaidi ya kuwa marafiki wa kawaida. Japokuwa nilikuwa najua kwamba namkera sana Raya kwa misimamo yangu lakini sikujali.
“Mbona hunijibu Jamal? Au hutaki nije?” swali hilo la Raya ndilo lililonizindua kutoka kwenye lindi zito la mawazo. Nilishasahau kwamba nazungumza na simu, nilizama kwenye mawazo ya kumfikiria Raya na kushindwa kuamua nini cha kufanya kwa wakati huo.
“Ok… ok… njoo hapa jirani na kituo cha polisi Mabatini, nakusubiri,” niliamua kukubali kwani sikuwa na ujanja mwingine, akakata simu. Mitaa yote ilikuwa kimya kabisa usiku ule, kelele pekee zilizokuwa zinasikika ni za vyura waliokuwa wakikoroma, wenyeji wa Kijitonyama watakuwa wananielewa vizuri kwani maeneo hayo hasa nyakati za mvua, huwa kunakuwa na vyura wengi wanaopiga sana kelele nyakati za usiku.
Nilisogea pembeni ya barabara na kusimama, nikawa namsubiri Raya ambaye hata dakika kumi hazikupita, akawasili akiwa kwenye bodaboda. Alishtuka sana kwa hali aliyonikuta nayo, mkononi nikiwa bado nimeshikilia mfuko wa chipsi nilizokuwa nimeenda kununua kwa ajili ya kula na Shenaiza.
“Jamal! What’s wrong with you?” (Jamal! Umepatwa na nini) alisema Raya huku akinisogelea, akionesha dhahiri alivyokuwa na shauku ya kutaka kujua kilichonitokea. Nilimjibu kwa kifupi kwamba ni stori ndefu na nipo kwenye matatizo makubwa.
“Twende tukaongelee nyumbani, it’s not safe out here in this dark hours (siyo salama hapa nje muda huu wa giza) alisema Raya huku akinipokea ule mfuko wa chipsi, akanitaka tupande ‘mshikaki’ kwenye bodaboda iliyomleta. Huo ulikuwa mtihani mwingine kwangu lakini sikujali sana.
Alitangulia yeye, akakaa kwa mtindo wa kujibinua, nilijua anafanya vile kwa lengo gani. Na Mimi nikapanda na kukaa nyuma yake, tukawa tumesogeleana sana kiasi cha miili yetu kugusana.
Hata hivyo, sikupatwa na hisia zozote kwani akili zangu hazikuwa hapo muda huo, nilikuwa nikiendelea kuwaza kuhusu hatima ya Shenaiza kule nyumbani kwangu. Dakika chache baadaye, tuliwasili nyumbani kwa akina Raya.
Kama alivyonieleza kwenye simu, kweli wazazi wake hawakuwepo, akanikaribisha mpaka sebuleni kwao, akafunga milango na mageti yote kisha akataka nimueleze kilichotokea. Tayari saa ya ukutani ilikuwa ikionesha kwamba ni saa saba za usiku.
Ilibidi nimueleze Raya ukweli wa kila kitu. Kwanza alinishangaa sana na kuniuliza nilipata wapi ujasiri wa kwenda kumtorosha hospitalini mtu ambaye ndiyo kwanza nimejuana naye siku hiyohiyo. Akazidi kunishangaa kwamba kwa nini sikumlazimisha msichana huyo anieleze ukweli wa kilichosababisha akajeruhiwa kiasi hicho na zaidi akaendelea kunilaumu kwa nini nimempeleka nyumbani kwangu, tena usiku ule.
“Mimi kila siku nikikwambia nije kukutembelea kwako unakuwa na visingizio lukuki, hata nikija hutaki tukae wawili tu lakini huyo umeweza kumuingiza kwako, tena usiku, kwa nini Jamal?” Raya alianza kulia kwa wivu.
“Naomba tuachane na hayo kwanza Raya, hebu tulimalize hili lililopo mbele yetu,” nilisema kwa upole kwani japokuwa alikuwa akisumbuliwa na wivu, kuna mambo ya msingi kabisa aliyoyaongea ambayo hata mimi nilipofikiria vizuri, niligundua kwamba nilikosa umakini katika kulishughulikia suala hilo.
Tukaanza kujadiliana nini cha kufanya ambapo aliniambia kwa sababu muda umeshaenda sana na nimeshatoa taarifa polisi, kwa usalama nilale hapohapo nyumbani kwao mpaka asubuhi ndiyo tutajua nini cha kufanya.
Sikuwa na cha kufanya, pamoja na ujanja wangu wote nikawa nimenasa kwenye tundu bovu, Raya akainuka na kuniandalia chakula kilichokuwa kimesalia, akaniambia zile chipsi nilizoenda kununua nizitupe kwani zinaweza hata kuwa zimewekwa sumu, nikakubaliana naye.
Ilibidi nijilazimishe tu kula kwani bado nilikuwa nikisumbuliwa sana na mawazo, nikala huku Raya akijitahidi kunichangamsha na kuniambia nichukulie kila kitu kilichotokea kuwa ni mipango ya Mungu.
“Huenda Mungu amesikia kilio changu cha siku nyingi cha kutaka uje kwetu,” alisema na kucheka mwenyewe, nikatabasamu kiaina kwani bado moyo wangu ulikuwa na hofu kubwa mno. Baada ya kumaliza kula, alinipeleka kuoga kisha kinarudi pale sebuleni.
“Si tunalala wote kitanda kimoja?” alisema Raya, kauli iliyonishtua sana kwa sababu niliona haiwezi kuwa tabia njema kwa mimi kulala naye kitanda kimoja wakati hakuwa mpenzi wangu, na pia tukiwa nyumbani kwao. Nikamkatalia katakata!
“Basi usijali, wewe utalala chumbani kwangu halafu mimi nitaenda kulala chumba cha wageni,” alisema akionesha kupoteza furaha. Nilimwambia yeye akalale chumbani kwake kama kawaida halafu mimi nikalale huko kwenye chumba cha wageni, akawa hataki, tukabishana kidogo lakini baadaye alikubali.
Akanipeleka mpaka kwenye chumba cha wageni huku mara kwa mara akinishika mwilini, niliamua kujikausha kwani nilijua endapo nitamchekea tu, usiku huo hautaisha salama, lazima tutaangukia dhambini.
Kwa jinsi nilivyokuwa nimechoka kwa pilikapilika za siku nzima, nilipoingia tu chumbani na Raya kutoka, nilivua nguo na kubaki na bukta tu, nikajilaza kitandani ambapo muda mfupi baadaye, nilipitiwa na usingizi mzito.
Nilipokuja kuzinduka, nilishtuka mno baada ya kugundua kuwa sikuwa nimelala peke yangu bali kuna mtu mwingine, tena wa jinsia ya kike, na kibaya zaidi, hata ile bukta yangu niliyolala nayo, ilishavuliwa. Nilikurupuka kwa kasi lakini yule mtu aliyelala pembeni yangu akanituliza na kuniambia nisiogope.
“Mungu wangu,” nilisema baada ya kugundua kuwa kumbe alikuwa ni Raya, tena naye akiwa mtupu kabisa, akaniambia kwamba alikuwa anaogopa kulala peke yake na ndiyo maana amekuja kulala na mimi.
Sikupata hata muda wa kujibu chochote, Raya akanikumbatia kwa nguvu mwilini na kuanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu, japokuwa sikuwa tayari kwa alichokuwa anakitaka, nilijikuta kwenye wakati mgumu mno, kwani ukichanganya joto la mwili wake na uzuri aliokuwa nao, ukizingatia kwamba tulikuwa wawili tu, nilijikuta nikishindwa cha kuamua, ‘Jamal’ wangu naye akaanza usumbufu.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 9
ILIPOISHIA:
Sikupata hata muda wa kujibu chochote, Raya akanikumbatia kwa nguvu mwilini na kuanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu, japokuwa sikuwa tayari kwa alichokuwa anakitaka, nilijikuta kwenye wakati mgumu mno, kwani ukichanganya joto la mwili wake na uzuri aliokuwa nao, ukizingatia kwamba tulikuwa wawili tu, nilijikuta nikishindwa cha kuamua, ‘Jamal’ wangu naye akaanza usumbufu.
SASA ENDELEA…

Nilishindwa kujizuia, na mimi nikamkumbatia Raya, kitendo ambacho kilimfurahisha mno, akausogeza mdomo wake kwangu, nami nikafanya hovyohivyo, ndimi zetu zikagusana, nikamsikia akitoa migumo ambayo ilizidi kuipagawisha akili yangu.
Japokuwa sikuwa mtaalamu sana kwenye mambo ya kikubwa, nilijitahidi kadiri ya uwezo wangu kumuonesha Raya kwamba na mimi sikuwa mshamba, ‘amsha-amsha’ ziliendelea na hatimaye kipyenga kikalia kuashiria kuanza kwa mpambano wa kukata na shoka, usio na refa wala jezi, huku nikishindwa kuzidhibiti papara zangu.
Wakati nikijiandaa kusakata kabumbu, ghafla mawazo juu ya Shenaiza na kilichokuwa kinaendelea kule nyumbani kwangu yalipita kwa kasi kubwa ndani ya kichwa changu, nikashangaa ‘Jamal’ wangu ambaye muda mfupi uliopita alikuwa ngangari ile kinoma, akianza kunywea na kupoteza kabisa ukakamavu wake.
Raya ambaye tayari alishajiweka tayari kupokea ‘mashuti’ ya nguvu kutoka kwangu, alishtushwa na kilichotokea, akaacha kila alichokuwa anakifanya.
“Vipi tena jaman mpenzi wangu, na..ta…ka…,” alisema Raya kwa sauti iliyokuwa ikikatakata, ikitokea kwenye matundu ya pua zake.
“Subiri kidogo,” nilisema kwa aibu kubwa, sikuwahi kutokewa na hali kama hiyo hata mara moja, nikashangaa imekuwaje? Sikupata jibu. Ili kuzuga, ilibidi niamke na kujifanya nataka kwenda maliwatoni, nikamuacha Raya amelala palepale huku akiwa kimya kabisa, akionesha kuugulia maumivu ya ndani kwa ndani.
Harakaharaka nilitoka na kuelekea choo cha ndani, nikajifungia mlango na kuanza kutafakari kuhusu kilichotokea. Nilijisikia aibu sana kwani sikujua Raya atanichukuliaje kama amenitafunia kila kitu na kuniwekea kabisa mdomoni lakini nimeshindwa kumeza. Japokuwa ulikuwa ni usiku sana na kulikuwa na baridi, nilifungulia maji ya bomba la mvua na kuanza kujimwagia. Nilisimama huku maji yakiendelea kunimwagikia kwa zaidi ya dakika tatu mpaka nikaanza kutetemeka kwa baridi.
Nikafunga bomba na kurudi chumbani ambako nilimkuta Raya amelala vilevile kama nilivyomuacha. Nikawa najisemeshasemesha ili ‘kuua soo’, nikajifuta maji na kupanda kitandani, nikamvutia Raya kifuani kwangu ambapo alikuja mzimamzima, ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe alikuwa akilia.
Lawama zake kubwa kwangu ni kwamba sikuwa nikimpenda na ndiyo maana nilimfanyia hivyo lakini kiukweli, wala sikuwa nimepanga hayo yatokee bali nilijikuta tu nikiishiwa ukakamavu.
Nikawa nambembeleza kwa maneno matamu na kwa mara ya kwanza nikamtamkia kwamba nampenda sana japokuwa nilisema vile ili kumtuliza. Alifurahi sana aliposikia maneno hayo kutoka kwangu, nikamuona akitabasamu na kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu, na mimi nikawa naonesha ushirikiano.
Niliamini safari hii nitaweza kukata kiu yake kwani ‘Jamal’ wangu naye alishaanza kuonesha ushirikiano, akawa anafura kwa hasira na kunipa matumaini makubwa kwamba nitaifuta aibu kubwa iliyokuwa inataka kunikabili.
Tuliendelea kufanya ‘warm-up’ kwa dakika kadhaa lakini safari hii Raya alionesha kutotaka kuchelewesha tena mambo, kabla hata kipyenga cha kuashiria kuanza kwa mpambano hakijalia, yeye alitaka kujianzishia mpira mwenyewe.
Katika hali ambayo sikuitegemea, mawazo juu ya Shenaiza yalijirudia tena akili mwangu, nikawa sijui nini kilichoendelea baada ya mimi kuondoka, kama ilivyokuwa mwanzo, ‘Jamal’ wangu akanywea, jambo lililomkasirisha sana Raya, safari hii akawa analia kwa sauti kama mtu aliyepokea taarifa za msiba.
“Kwa nini unanitesa hivi Jamal? Kwani mimi nina kasoro gani mpaka unifanyie hivi?” alisema huku akilia, nikaanza upya kazi ya kumbembeleza huku nikijisikia aibu kubwa ndani ya moyo wangu. Haikuwa kazi nyepesi kumtuliza Raya mpaka atulie, nikawa najaribu kujikakamua na kumfosi ‘Jamal’ wangu arudi tena mchezoni lakini ilikuwa sawa na kazi bure.
Mpaka kunapambazuka, hakuna kilichofanyika zaidi ya kubembelezana, saa kumi na moja alfajiri, wote tulipitiwa na usingizi mzito na tulipokuja kuzinduka, tayari ilikuwa ni saa moja za asubuhi. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikajaribu kujikakamua tena kuona kama angalau naweza kufanya chochote lakini ilikuwa sawa na kazi bure, Jamal wangu alikuwa amelala doro, jambo lililonifadhaisha sana.
Muda mfupi baadaye Raya naye aliamka, macho yake yakiwa yamevimba na kuwa mekundu kutokana na kulia sana, akaenda chumbani kwake na kuniacha nikijiandaa. Baada ya kumaliza kujiandaa, nilitoka hadi sebuleni ambako nilimkuta Raya akiandaa kifungua kinywa.
Ule uchangamfu aliokuwa nao kwangu uliyeyuka kama theluji iyeyukavyo juani. Nilitamani sana ajue kwamba sikuwa nimemfanyia makusudi bali lilikuwa ni jambo ambalo lipo nje ya uwezo wangu lakini haikuwezekana, alichoamini Raya ni kwamba sikuwa nampenda na nilifanya vile kumkomoa.
Tulipata kifungua kinywa kimyakimya, kwa kuwa sikuwa najua kilichotokea nyumbani kwangu usiku ule, sikuwa na muda wa kuendelea kukaa pale, nilimuaga Raya na kumwambia tutakutana kazini baadaye lakini cha ajabu, alikataa katakata kuniacha niondoke peke yangu, akaniambia atanisindikiza na kama ni kuomba ruhusa kazini, niombe ya watu wawili, mimi na yeye.
Ulikuwa ni mtihani mkubwa sana kwangu kwa sababu kwa kilichotokea kati yangu na yeye, nilihitaji kupata muda wa kukaa peke yangu na kutafakari kwa kina kilichosababisha hali ile iliyonitokea usiku.
Lakini kubwa zaidi, sikutaka kumuingiza kwenye matatizo yangu na Shenaiza, kwa kuwa nilikuwa nimeyaanza mwenyewe, nilitaka nikayamalize mwenyewe. Hata hivyo, sikutaka pia kuendelea kumuudhi, ikabidi nimkubalie ambapo tulitoka na safari ya kuelekea nyumbani kwangu ikaanza.
Tukiwa njiani nilimpigia simu bosi kazini na kumueleza kwamba nilikuwa nimepatwa na matatizo makubwa na kwamba nitachelewa kufika kazini. Sikutaka kumfafanulia kilichotokea, kwa bahati nzuri alinielewa. Nilimpigia pia simu Justice na kumtaka asizungumze chochote kazini kuhusu nilichomwambia jana yake.
“Sasa mbona umeomba ruhusa peke yako? Kwa nini usiniombee na mimi kama tulivyokubaliana?” Raya aliniuliza kwa sauti ya chini, iliyoonesha dhahiri kwamba hakuwa na furaha, Nilishindwa cha kumjibu zaidi ya kumtaka apige mwenyewe simu na kuomba ruhusa kivyake ili tusije kuonekana kwamba tumepanga kutega kazi kwa makusudi.
Kwa bahati nzuri naye alikubaliwa, tukaendelea na safari ya kuelekea kwangu kwa kutumia Bajaj ambayo Raya ndiye aliyelipa, kadiri tulivyokuwa tunazidi kukaribia kwangu ndivyo mapigo ya moyo wangu yalivyokuwa yanazidi kuongezeka, sikujua nitakutana na nini.
Nilimuelekeza dereva njia ya kupita kwani sikutaka kutokezea upande wa mbele wa mtaa niliokuwa naishi, nilitaka tutokezee uchochoroni kwa sababu za kiusalama, kweli dereva yule alinielewa na safari iliendelea. Hatimaye tukafika kwangu, tukashuka kwenye Bajaj na kumwambia yeye aondoke zake, tukaanza kupita kwenye uchochoro unaotokezea kwangu.
Tulipokaribia kufika, huku mapigo ya moyo wangu yakizidi kupiga kiasi cha kunifanya nitokwe na kijasho chembamba japokuwa bado ilikuwa ni asubuhi na kulikuwa na kibaridi, nilishtuka zaidi baada ya kuona umati mkubwa wa watu ukiwa umekusanyika mbele ya nyumba niliyokuwa naishi.
“Mungu wangu,” nilisema huku nikifikicha macho na kutazama vizuri, kuna muda nilikuwa nahisi kwamba huenda nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo, sikuelewa pale kwangu kuna kilichosababisha watu wajae kiasi kile.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom