Muziki: Kuchelewa Sifa Mbaya
Unaweza kushangaa ninavyojishangaa mar nyingi! Na ujue nini, hata sijui nini ninajishangaa maana kila nikianza lazima nianze na salamu, yeah kukusalimia wewe Kapuku unayelifanya jukwaa hili kuwa sehemu bora kabisa ya kuwepo. Asante nyingi kwako wewe unayenisoma sasa maana bila wewe hapa hapavutii.
Well, leo ni usiku mwingine na siku hii imekaa kireggae reggae tu nami bila hiyana sitaki kuchelwa maana kuchelewa si sifa nzuri. Usigune, maana kuna mtaa unaitwa Minuteman street wengi sana wamepanga maeneo haya maana ukitaka kupangishwa au kununua nyumba hucheleweshwi. Nimesema usigune kwani kuchelewa ni relative, wengine ukichelewa ndo unaonekana makini lakini ukiwahi sana ndo utaitwa majina lukuki. Mimi vyovyote iwe, nachelewa na kuwahi kutokana na mazingira sio mazingara nilipo na uhitaji wa wakati huo.
Muziki sasa, bado naendelea na Shaggy, ukimchoka unasema tunabadilisha