Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,013
Muziki: Wema na Ubaya, Cha Pili Kiache
Muda unakimbia sana Makapuku waheshimika, nani alijua kesho itakuwa ni Ijumaa! Ukisoma kiumakini utagundua kuwa sijauliza swali ila tu nimekuja kukusalimia wewe, yeah, wewe hapo unayenisoma muda huu. Pokea heshima nyingi sana usiku huu maana unastahili na stahili hii ni kwa sababu wewe unaunda timu inayoifanya KF iwe mahala pa kuvutia bila kutolewa mahari. Asante sana kwa kuwepo hapa.
Hivi kuna sababu yoyote ya kutofanya jambo zuri kwa mtu usiyefahamiana naye? Usiniambie kuwa dini zimetufundisha kuwa wema maana dini zetu hizi zina mazongo kibao, so weka pembeni jibu la dini yako jibu wewe kama wewe. Binafsi ninajiaminisha ukiwa mstaarabu (civility) huhitaji uijue dini ndo utende wema na uuchukie ubaya. Kuna bangi na bangili, hiyo ya kwanza inatibu sikio. Chukua hilo maana kubadilika ni tabia ya kila kiumbe hai. Hulazimishwi kubadilika, baki hivyo hivyo kama mother nature itakuruhusu.
Asanteni sana wadau mliotuamsha kwa magazeti, sala, BBC, kubwa 10, sogozi za mchana, michezo na zaidi asante kwa wageni waliotembelea hapa. Usijiulize mbona ninakaribisha sana kwani mimi ni nani hapa, mbona najidai kujua sana, well, la kwanza, mimi ni kama wewe tu, bando langu na kutaka kupata maarifa kwa kuwa hapa kunanifanya nije hapa na kuwaona wengine wakiwa hapa basi nawiwa kuwashukur maana maarifa yanaongezeka.
Muziki sasa, huwa nikimsikiliza nakumbuka mengi sana, mazuri na yenye utata ulionifanya nijiulize je hili nililolifanya (enzi hizo) ni sahihi. Hizi safari ziache tu na wengine tukiendaga ugenini lodging zina mapepo hatulali peke yetu, you know warra am saing'i. Ndivyo inavyokuwa na ndo unasema a blessing in disguise. Anaitwa Jose Chameleon, ana udokta wa heshima huyu kwa namna anavyotumia mali zake kusaidia wahitaji wanaomzunguka.
Burudika mdau
Binamu asante jamaan naomba nichague nyimbo binamu yangu

