Makapuku Forum

Makapuku Forum

BABA MUNGU wa mbinguni asante kutuamsha salama tutakase ,tuongoze,tufundishe Ee Roho Mtakatifu siku ya leo ibarikiwe,tunakuomba tuepushe na mabaya yote tuepushe na dhambi za aina yoyote kwa kunena ,kutenda hata kutotimiza wajibu..tunaomba tuwe wanyenyekevu miongoni mwetu na mbele yako kila mtu akamhesabu mwenzake kuwa ni bora na muhimu katika safari hii ya Kurudi kwako BABA,Safari ambayo inahitaji mshikamano na kutiana moyo,safari ambayo inahitaji nguvu ya Roho Mtakatifu ili tusirudi nyuma katika kumtumikia Mungu wetu.

BABA tunaomba ponya wagonjwa,fariji wafiwa ,wajane na yatima watie moyo waliopondeka na kukata tamaa wale waliorudi nyuma wainuke tena na wafahamu bado unatupenda na unatusamehe na kutufutia makosa yetu kila iitwapo leo.

Wabariki watoto wetu majumbani na mashuleni wawe na hofu ya MUNGU na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.waimarishe katika masomo yao wawe vichwa na si mikia.

Ponya ndoa,ponya mahusiano,ponya familia na imarisha upendo kati yetu MAKAPUKU

Tuimarishe katika kazi zetu na mipango yetu ikafanikiwe BABA kila mmoja wetu akafaidi matunda ya kazi za mikono yake.

Asante Baba kwakuwa unatupenda na utatenda sawa na mapenzi yako.

Katika jina la Yesu naomba na kushukuru

Amen,Asante.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE BARAKA

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
Amen,asante kwa sala mama Mchuchu na ubarikiwe pia
 
Pia....

Waziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi, ametahadharisha kwamba kuna changamoto nyingi, licha ya ushindi katika mapambano ya kuurudisha mji wa Mosul kutoka katika himaya ya wapiganaji wa Kiislamu.

Leo mkutano wa dunia kuhusu uzazi wa mpango unafanyika huko jijini London nchini Uingereza, ili kujadili jinsi ya kuboresha huduma za uzazi wa mpango duniani

Tume ya uchaguzi nchini Kenya yafikisha mahakamani suala la tata la utolewaji zabuni ya karatasi za kupigia kura

Rwanda imejaliwa vipaji vya muziki lakini muziki huo umeshindwa kuvuka mipaka ya nchi hiyo changamoto ikiwa ni lugha itumikayo

Tanzania ina azma ya kuelekea katika uchumi wa viwanda ikiwa ni ajenda kubwa ya serikali ya awamu ya tano.

Uganda imepeleka kikosi cha waniriadha 13 kwenye mashindano ya dunia IAAF vijana waliochini ya umri wa miaka 18.Timu hiyo imekuwa kambini kwa zaidi ya miezi miwili huku ikikabiliwa na changamoto kadhaa

Swala la usalama limeiponza Kenya, mwenyeji wa makala ya 10 na ya mwisho ya dunia ya mbio za vijana wasiozidi umri wa miaka kumi na nane yatakayoanza kesho mjini Nairobi Kenya. Mabingwa watetezi Marekani waliongoza mataifa mengine 5 kujiondoa huku wakihofia usalama wa wanariadha wao mjini Nairobi.
 
BABA MUNGU wa mbinguni asante kutuamsha salama tutakase ,tuongoze,tufundishe Ee Roho Mtakatifu siku ya leo ibarikiwe,tunakuomba tuepushe na mabaya yote tuepushe na dhambi za aina yoyote kwa kunena ,kutenda hata kutotimiza wajibu..tunaomba tuwe wanyenyekevu miongoni mwetu na mbele yako kila mtu akamhesabu mwenzake kuwa ni bora na muhimu katika safari hii ya Kurudi kwako BABA,Safari ambayo inahitaji mshikamano na kutiana moyo,safari ambayo inahitaji nguvu ya Roho Mtakatifu ili tusirudi nyuma katika kumtumikia Mungu wetu.

BABA tunaomba ponya wagonjwa,fariji wafiwa ,wajane na yatima watie moyo waliopondeka na kukata tamaa wale waliorudi nyuma wainuke tena na wafahamu bado unatupenda na unatusamehe na kutufutia makosa yetu kila iitwapo leo.

Wabariki watoto wetu majumbani na mashuleni wawe na hofu ya MUNGU na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.waimarishe katika masomo yao wawe vichwa na si mikia.

Ponya ndoa,ponya mahusiano,ponya familia na imarisha upendo kati yetu MAKAPUKU

Tuimarishe katika kazi zetu na mipango yetu ikafanikiwe BABA kila mmoja wetu akafaidi matunda ya kazi za mikono yake.

Asante Baba kwakuwa unatupenda na utatenda sawa na mapenzi yako.

Katika jina la Yesu naomba na kushukuru

Amen,Asante.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE BARAKA

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
Ameeen
 
Leo nimekuja na utafiti hewa

Ukiwa mvivu sehemu uliyo ajiriwa kwa kisingizio kuwa namtajirisha bosi basi amini umefeli kufikiri

Maana hata shughuli zako utazifanya kwa uvivu kwa kujidanganya mbona nimejiajiri

Jitume kwa chochote ufanyacho kwa faida ya maisha yako na familia yako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom