Muziki: Penda Mwili Wako
Jumapili inaishiria wadau, naamini kabisa tumekuwa na siku nzuri. Kila mmoja na siku yake, wapo waloenda church leo, wapo walioenda kazini na wapo waliokuwepokuwepo tu, lazy sunday. Na kizuri zaidi ni kuwa bado tunakutana hapa na kubadilisha mawili matatu. Kapuku Forum ni jukwaa bora kabisa kwa sababu wewe u sehemu yake. Unalijua hilo.
Easy and lazy sunday ndivyo nilivyoiona leo mimi, na hata maongezi ya humu ndo yamekaa kirahisirahisi tu ilmradi tu kufanya siku iende vizuri.
Mambo ya simu ha hahahahaha, Tecno werevaa (whatever right?) ndo imeshika chati leo, hongera sana wenye tecno werevaa maaana naonaoga hata mnaweza kutuma maua. Mimi simu yangu ina simu ndani ya simu, cover la singsung, betry LG, supika za motorola, na keypads ni za tecno werevaa bila kusahau ni screen tach ya Itel6 (inafanana na Iphone). Mwisho wa siku ninaweza kuweka signature na kuingia JF kufurahia KF. Una tatizo na simu yangu?
Muziki wa leo: Penda mwili wako, yeah, love your body maana ni wewe na huwezi kuwa mwingine, kama una kakitambi ka bia na machalali basi endelea kuongeza michemsho, mwili ni wako utunze maana ni wewe unaumiliki. Fanya mazoezi ya kiaina ili uwe mwepesi, kula misosi ya maana sio kila siku wewe karanga na fanta orange.
Tuburudike na Ed leo, kuikamilisha Jumapili yetu na kuombeana kuwa wiki hii iwe ni nzuri na yenye mafanikio kwetu.