Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: KKB

Leo napata ugumu kusalimia kwa maneno, tupeane tano ngumu ngumu kuashiria kuwa tumekuwa na siku nzuri kabisa siku ya leo bila kujali nini kilijiri kwa uzuri au ubaya. Nitakuwa faster leo maana mchana mzima beki zimekuwa hazikabi ipaswavyo hivyo imebidi kocha niingie uwanjani dakika za majeruhi angalau kutafuta droo, yeah, sio droo utie nguo na makorokoro bali sare angalau asubuhi staftahi ipatikane.

Ni bahati mbaya sana kusikia member mwenzetu keshakuwa mwendazake (RIP), ndo maisha hayo nasi hatuna cha kuzuia maana ardhi ni kubwa sana, akizikwa yeye si kwamba atatumalizia nafasi, makaburi hayajajaa kutufanya sisi tusife. Inauma sana. Pole kwetu

Sijui ni upepo wa kusi au kasi umepita nami leo nilitaka kuweka nyimbo ya 'kitotototo' yaani kucheza mwanzo mwisho unaelewa huelewi ilimradi tu vyombo vya muziki vinaposikika unajisikia kutingisha mwili na hasa mguu, usitingishe kiuno, bado ni mapema sana na ada zinazidi kupanda kila siku. Sakayo asante kwa uchaguzi huu

Mr Nice na si Mr Noise ndiye atakayetuburudisha leo, sina mengi juu yake maana ukiona Diamond ang'ara leo jua kuwa Mr Nice aliisimamisha Afrika Mashariki na Kati, hakuacha hata kitongoji kimoja katika nchi saba zinazotuzunguka. Wazazi iliwabidi watunge maneno ili kuwaelewesha watoto kuwa kuku akipanda baiskeli ujue anaenda kuchinjwa.

Hadi wakati mwingine. Nakupenda kapuku mwenzangu sababu wewe ni mtu muhimu humu, heshima yako sana



KKB- Kuku kapanda Baiskeli

Woyooooooo zilipendwa wa dada angu mie kama nakuona huko unavyofurahii umekulapo mahela yake na wewe lipa fadhila ujue
 
Ni changamoto kwa kweeli
Hii tabia nilivyo toka huko nilipata nafasi ya kutembelea baadhi ya viwanda vilivyopo pwani nikaona wanao Fanya kazi kwenye hivyo viwanda ni wahehe, wasukuma, na wanyakyusa nikauliza wenyeji vipi hawapo kazini wakasema wenyeji ni wataalamu wa kucheza bao tu na porojo nyingi mdomon
 
Nafikiri siku anamfunga Sauzi alikuwa kam eza dozi na watu tukaamini kapona
Leo kasahau kumeza dawa tuliokuwa tunamsifia wote tumeumbuka
Kichaa huwa haponi isipokuwa Siku nyingine huamka vizuri na Siku nyingine vibaya

Hata kitaani yupo baadhi ya siku huwa sawa ila siku nyingine kutembea uchi wa mnyama
Ni kosa kumwekea dhamana chizi
...



 
Hii tabia nilivyo toka huko nilipata nafasi ya kutembelea baadhi ya viwanda vilivyopo pwani nikaona wanao Fanya kazi kwenye hivyo viwanda ni wahehe, wasukuma, na wanyakyusa nikauliza wenyeji vipi hawapo kazini wakasema wenyeji ni wataalamu wa kucheza bao tu na porojo nyingi mdomon
Na huo ndo ukweli kabisaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom