Muziki: Siku Rahisi, Smile.
Ninachoweza kusema ni kimoja tu, kwa wale mnaofanya kazi Mon-Fri hongereni sana na leo ndo mwanzo kabisa wa wikend. Ijumaa tunakutana tena hapa kabla ya kuamua Jmosi na Jpili tutafanya nini. Leo tunaburudika.
Siasa ni maisha, utaikuta kila mahali hata chumbani kuna siasa zake, siasa za chumbani. Wakati mwingine utahitaji kufanya propaganda ili tu siasa za chumbani ziweze kufanikiwa kitandani. Hongera sana kwa mlioweka makochi chumbani, nyie siasa zenu ni za karne ijayo.
Nimekaa tu hapa mtaani karibu na ninapojificha, well, mshahara ndo wiki yake hii na tayari bajeti nishaipiga na nakisi ndo nayoiteketeza muda huu. Karibu ujifiche, kinywaji cha kwanza juu yangu, kinachofuata ni juu yako.
Mara zote nimekuwa nikisema humu, muziki ni furaha, muziki ni upendo, muziki ni siasa, muziki kwa ufupi ni maisha. Muziki ni zaidi ya soka, muziki una lugha yake inayokubalika na masikio ya wenye masikio hata kama hawawezi kuchakata maneno yakaleta maana. Huo ndo muziki, usipatwe na jinamizi.
Tumwangalia Carlos Santana, gwiji wa gitaa la nyuzi sita ambaye huchanganya mapigo ya Ulatin, USA na Africa na hivyo kumfanya kuwa mpiga gitaa maarufu kabisa anayeishi. Alivutiwa sana na upigaji wa mkali BB King. Santana ana tuzo zaidi ya 10 za Grammy pamoja na nyingine nyingi.
Tumwangalie hapa clip ya YouTube akicharaza gitaa lake kwa uzuri kabisa