Makapuku Forum

Makapuku Forum

Sawa ni msimamo mzuri sana kwa imani tunayashinda yote ila uchawi upo

KUTOKA 7

8.BWANA akanena na Musa na Haruna ,akawaambia.

9.Farao atakaponena nanyi,na kuwaambia ,Jifanyieni miujiza ndipo utakapomwambia Haruni ,Shika fimbo yako ,uibwage chini mbele ya Farao,ili iwe nyoka .

10.Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao wakafanya hivyo kama BWANA Alivyowaambia ;Haruni akaobwaga fimbo yake chini mbele ya Farao ,mbele ya watumishi wake ikawa nyoka.

11.Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.

12.Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake nazo zikawa nyoka lakini fimbo ya Haruni ikameza fimbo zao.

13.Moyo wa Farao ukawa mgumu asiwasikilize kama BWANA alivyonena.

H ESABU 23

23.Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo wala hapana uganga juu ya Israel.

HESABU 24

1....hakwenda ..ili kutafuta uchawi....


1 SAMWEL 15

23.Kuasi ni kama dhambi ya uchawi......



2 WAFALME 17

17.Wakawapitisha watoto wao ,waume na wake ,motoni ,Wakapiga ramli wakafanya uchawi...wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa BWANA ,hata kumkasirisha


Y apo maandiko mengi yanayothibitisha uchawi upo,tunapaswa kumshika sana Mungu na kumuomba Mungu kutuepusha na mambo haya.

Shalom
Asante mama mchungaji kwa ufunuo wa uchawi
 
Ha hahahahhaha! Umekula lakini? Maana leo unahasira na siwezi kukujaji yaweza kuwa ni njaa au uko kwenye siku zako
Kimbelembele tu kujifanya ujuaji hata kwa yasiyokuhusu. Mwanaume mzima na mambo ya siku wapi na wapi? Umenunua kesi hiyo sasa hangaika nayo. Fala!
7f73c3b56a1982d3d83051495f870b74.jpg
 
1 SAMWEL 25

6.Na hivi ndivyo mtakavyomwambia huyu aishie salama,Amani iwe kwako,na amani nyumbani mwako,na Amani kwao wote ulio nao

Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu BWANA MUNGU wa Majeshi asante kutufikisha umbali huu,umetulinda mchana kutwa umetuepusha na hatari mbalimbali na ajali mbalimbali ,BABA tunaomba tusamehe yote tuliyotenda kwa mawazo,maneno na matendo kwa kukusudia au kutokusudia..tunawasamehe wote waliotukosea ili tuweze fanya toba ya kweli maana BABA tunakiri udhaifu sisi ni watu tu kuna wakati tunaghafilika..nyoosha mkono wako BABA uturehemu twakusihi BABA mwema ili tuende vitandani tukiwa salama na amani toka kwako.Asante kwa kuwa unatusamehe kila iitwapo leo.

BABA tunakualika usiku wa leo tuma malaika wako walinzi watuzingire,watulinde,tuzingire na ukuta wa moto wa damu ya Yesu,utukumbatie kama kuku anavyokumbatia vifaranga vyake.

Usiku waleo endelea kutuponya mioyo iliyopondeka,magonjwa,dhiki,taabu na kukata tamaa..tusaidie tuzidishe upendo kwa wale tunaodhani ni maadui wetu ili tuweze kuuona ukuu na utukufu wako
Asante Baba maana utatupa kushinda,utatuamsha salama na tutakutana tena kesho mahali hapa tukiwa tumeachilia mambo yote ya leo kesho iwe siku mpya na ya kukupendeza
Tunaomba yote katika jina la Yesu Mpatanishi na mwokozi wetu Amen Asante

MUNGU ANATUPENDA SANA,NAMI NAWAPENDA SANASANA MBARIKIWE USIKU MWEMA MAKAPUKU WOTE
 
JEREMIA 33

BWANA MUNGU ASEMA

3.Niite nami nitakuitikia,nami nitakuonesha mambo makubwa ,magumu usiyoyajua

BABA Asante kutuamsha salama,asante kwa zawadi hii nzuri kabisa ya uhai asante kwa kuitika kila tunapokuita,unatujua vyema na wala hujawahi kutuacha...tunakuona MUNGU wetu daima unatuitikia.
Tunaomba toba tunapoanza siku ya leo tuanze tukiwa tumeyaacha yote ya nyuma na kuanza upya maana ni siku mpya kabisa uliyoifanya BWANA.

Tunaomba utujalie afya njema,amani,mshikamano,msamaha,uvumilivu,upendo na yote yanayofanana na hayo.

Ponya wagonjwa,watie moyo waliopondeka mioyo,wafungulie wafungwa na wape faraja yatima na wajane.

Bariki kazi za mikono yetu na utufundishe kufanya kazi kwa bidii.

Tuopoe katika hatari zote za mwili na za roho,tuwe salama.

Asante BABA kwa kutuitikia

Tunaomba kwa
jina la Yesu Amen

MUWE NA SIKU NJEMA MBARIKIWE
 
JEREMIA 33

BWANA MUNGU ASEMA

3.Niite nami nitakuitikia,nami nitakuonesha mambo makubwa ,magumu usiyoyajua

BABA Asante kutuamsha salama,asante kwa zawadi hii nzuri kabisa ya uhai asante kwa kuitika kila tunapokuita,unatujua vyema na wala hujawahi kutuacha...tunakuona MUNGU wetu daima unatuitikia.
Tunaomba toba tunapoanza siku ya leo tuanze tukiwa tumeyaacha yote ya nyuma na kuanza upya maana ni siku mpya kabisa uliyoifanya BWANA.

Tunaomba utujalie afya njema,amani,mshikamano,msamaha,uvumilivu,upendo na yote yanayofanana na hayo.

Ponya wagonjwa,watie moyo waliopondeka mioyo,wafungulie wafungwa na wape faraja yatima na wajane.

Bariki kazi za mikono yetu na utufundishe kufanya kazi kwa bidii.

Tuopoe katika hatari zote za mwili na za roho,tuwe salama.

Asante BABA kwa kutuitikia

Tunaomba kwa
jina la Yesu Amen

MUWE NA SIKU NJEMA MBARIKIWE
Asantee mama kwa baraka
 
SEHEMU YA 11

[}"Pole sana Hussein. Laiti ungeishi kwa kuyakumbuka maneno yangu huenda ungeweza kupata maana ya maneno ya Mungu pale anapotwambia wanaume kuwa tuishi na wanawake kwa akili. Buriani kwako naamini kwa sasa umeelewa kwa vitendo. Wanawake ni wauaji."{]
Nuru na taswira ya bwana yule iliyeyuka. Fahamu zangu zilikata na moyo wangu kuanzia pale ndipo rasmi ulikiri na kutanabahi milele kuwa WANAWAKE NI WAUAJI.

||********||
Kilisikika tena kilio cha kwikwi. Kumbukizi zilizidi kutonesha moyo wa mzee Hussein bubu. Kamishna Shebby alijitahidi kumtuliza huku akiwa na shauku ya kuelewa zaidi kilichofatia baadae.
Machungu ya moyo wa Hussein yalijidhihirisha machoni. Huruma ilizidi kumvaa kamishna. Alijikuta naye machozi yakimponyoka pasipo kusudi. Nafsini alikiri kile alichokuwa anasimulia Hussein na kuamini miaka yote gerezani anatumikia kimakosa. Amedhulumiwa haki na bado amehukumiwa. Lakini alichojiuliza kamishna Shebby kama mke wa Hussein ndiye alipanga yote ilikuwaje hadi kukawa na uthibitisho wa maiti yake na mtoto? Ina maana naye aligeukwa ama? Na iweje huyo Zai mke wa Hussein afahamiane na hao watu hata amgeuke mumewe waliyeishi kwa amani? Ina maana kweli aliolewa na huyo Mr X? Na kama alimuoa kwanini awaue wote?
Maswali yalimkanyaga kichwani kamishna japo alikuwa mtaalamu sana kwenye kufikiri na kufumbua jambo lakini kwa maswali yale hakuweza kupata majibu ya haraka zaidi ya kumsihi mfungwa wake (Hussein) ajikaze ili aendelee kumsimulia kilichotokea baada ya kurudiwa na fahamu mpaka kukamatwa na kuhukumiwa.
Kwa sauti iliyobeba maumivu mazito moyoni mwake Hussein aliamua kuendelea kusimulia mapito yaliyozika ndoto zake na kujikuta anazeekea jela akisubiri kifo tu. Aliamua sasa aweke kila kitu wazi kwa kijana yule ambaye aliamini ni askari kiongozi mwenye moyo wa kipekee sana.
Huku akipangusa mafua Hussein aliendelea kusimulia ilivyokuwa mara baada ya kupigwa na kupoteza fahamu.

*******
||SIRI GIZANI||
_______________

Hali ya ubaridi na unyevunyevu ndiyo ilinizindusha kwenye sinzio la mauti. Nilijinyanyua kutaka kusimama lakini uzito wa kichwa ulizidi mwili. Nilijikuta nakaa kitako nguvu zimeperuka. 'Pwitu..pwitu..pwiii!' Kisogo kilinipwita na ubaridi ulizidi kunitirika. Niliupeleka mkono kujishika eneo la nyuma ya kichwa. Looh! Niligundua kuwa navuja damu kichwani. Bila shaka kama si yale mabuti basi ni lile rungu lililopigiza kisogo changu ndilo lilinipasua. Nilitazama huku na huko kuangalia kama kuna watu wanaoweza nipa msaada. Lakini pori lilizizima 'Ziii'. Ndipo lilinijia wazo nikusanye nguvu nipige mayowe huenda ukatokea muujiza yeyote akanisikia. Lakini pia sauti yangu ilikosa nguvu. Sikujua yalipita masaa mangapi toka nipoteze fahamu. Lakini mng'ao wa mbaramwezi ulitosha kunijuza kuwa muda ulisonga sana. Ndipo nilipojikaza na kusimama tena huku nikijikagua.
"Mungu wangu!" Nilihamaki kuona damu zimetapakaa kwenye nguo niliyovaa. Chini mpaka juu. Lakini nilipojipapasa mwili sikuhisi kuwa na jeraha lolote zaidi ya kisogoni ambapo mishipa ya kichwa ilinipwita kama saa ya mshale. Laa haula! nilipoyatupa macho chini pale niliponyanyuka nilishangaa kuliona panga lililooga damu. Kutokana na nuru ya mbaramwezi niliweza ona michirizi mengine ya damu kuelekea porini. Nilishindwa kuyaamini macho yangu kwa haraka. Ndipo nilijikuta nikilishika lile panga kwa taharuki na kuligeuza geuza kuhakiki kama ni kweli au naona mawenge. Hapo ndipo akili iliniaminisha kuwa kile nikionacho ni kweli wala si mawenge. Lile ni panga na zile ni damu pia sikuwa na majeraha mwilini. Na hapo ndipo nilipostuka na kulitupa chini haraka lile panga na kujikuta nguvu zikinirudia. Nyatu nyatu kwa umakini niliifatilia ile michilizi ya damu. Macho pima yamenituka huku moyo tikatika ukinitikisa kifua.
Lakini kabla sijafika kwenye ukomo wa michirizi ya zile damu kuona kulikoni. Ndipo kwa mbali nilisikia kelele za watu. Niligeuka niliweza kuona vimulimuli vya tochi kutokea upande ule wa kwendea kijiji alichoishi ba'mkubwa. Tumaini jipya lilizaliwa moyoni mwangu kwa kutaraji msaada umenifikia sasa. Lakini kadili walivyonikaribi wale watu niliweza kusikia maneno yao waliyokuwa wanasema kwa sauti za mihemuko ya hasira. Nikiwa katika hali ya sintofahamu mara waliponiona walininyooshea vidole na maneno yao yalinitisha zaidi na kuniogopesha.
"Mwanaharamu mwenyewe si ndio yuuleeee.."
"Enheeeee yule yule si unaona alivyolowa damu?"
"Aliyeua auaweeee hebu tupisheni sie mbona hamtembei tutamkosaaa.." Walipaza sauti na wengine walianza kunirushia mawe huku wakinadi mayowe.
"PIGAAA...! UWAAAAA"
Hapo nilipagawa zaidi na kujaribu kuipaza sauti huku nikikwepa mawe na kusema.
"Jamani sio mimiii! Mimi ndiye niliyevamiwaaa."
"MUONGO HUYOOO MUUAJI UWAA!" Sauti yangu haikusadikiwa na yeyote zaidi nilipunyuliwa na mkuki ulioenda kuchoma kwenye mti uliokuwa nyuma yangu. Niliwashuhudia wengine wakiwa pia wamebeba silaha za jadi. Hapo sikuwa na chaguo zaidi ya kuukimbiza mwili wangu ili kunusuru maisha yangu yanayotaka kupokwa na kundi lile la wanakijiji walioshiba jazba.
Nilijikuta naruka na kuanza kutimua mbio huku upepo mkali ukinipitia 'Vuup' karibu na kichwa baada ya kurushwa kwa rungu moja kubwa ambalo niliamini lingenipata huenda ningezima pale pale kama sio kufa kabisa.
Nilikimbia kwa kasi na kiwewe kunusuru maisha yangu kwa kuifata ile njia iliyoelekea barabara kuu. Waliniandamisha kama mwizi au mnyama mwitu aliyevamia makazi ya watu.
Lakini kabla sijafika mbali mbele yangu nilimulikwa usoni na mwanga mkali wa tochi. Niliamini kama wamenipitia denge sasa nimekwisha. Nilishindwa kuona vizuri na kujikuta navamia pori. Lakini ile kutahamaki nilisikia 'PAA! PAA!' risasi zilichana anga sambamba na sauti kali ikiniamuru.
"SIMAMA HARAKA." Ilisikika sauti hii ya mamlaka kupitia spika ya mkononi. Nilitii sikuwa na budi. Nilikinai na kukubaliana na yote kama kufa acha nife tu.
"Sisi ni POLISI tunawasihi raia mtulie msichukue sheria mkononi. Mshatoa taarifa kwetu tunaomba mtusaidie kuona eneo lenyewe la tukio hasa ni lipi na jee mtuhumiwa husika ndie huyu mliyekuwa mnamfukuzaa?" Sauti ilitangaza zaidi na hapo hofu ilizidi kunikumbata punde wananchi walipojibu.
"Ndioooooo Afande tuachieni tuliue kabisaaa linyamaa hiloo." Walichagiza huku wakiwa wanashindwa kunifanya chochote baada ya askari wale wenye bunduki kunifikia.
"tulia hivyo hivyo piga magoti nyang'au wee." Kitako cha bunduki kilinisabahi kwenye mabega baada ya kubamizwa na askari mmoja huku akinitia pingu mikononi. Viungo vilitepeteka na kila kitu niliona kama ndoto.
Nilikamatwa suruali na kunyanyuliwa kibabe na askari yule mwenye umbo la miraba minne huku wengine wakinizunguka wakiwa na bunduki. Nilitembelea vidole mpelampela wananchi waliongoza njia mpaka eneo la tukio. Moja kwa moja hadi kwenye kichaka ambapo kulikuwa na michilizi ya damu niliyokuwa naifatilia awali. Askari walipofika na kumulika kwa tochi zao ndipo niliwehuka kwa kile nilichokiona. Maiti mbili ya mama na mtoto mdogo zikiwa zimekatwa katwa vibaya.
"ZAIIIIII MKE WANGU?!! MWINSHEHEEEE MWANANGUU!" Nilipiga yowe lakini nilipigwa vitako vya bunduki na maafande.
"Tulia liuaji wee!" Afande mmoja aliniamuru. Sikumbuki walikuwa askari wangapi. Lakini nilizidi kuchanganyikiwa hasa baada ya kuona nguo za kale katoto ndio zilezile alizovaa mwanangu siku hiyo. Nilipata hakika ni yeye mwanangu ambaye aliuawa kinyama sana.
Nilipiga kelele kwa kumlilia huku nikiitazama na maiti ya mke wangu ambayo iliharibiwa sana sehemu za uso. Askari walininyong'onyesha zaidi kwa kunipiga huku raia wakitamani waachiwe wanimalize.
"Afande Jacobo jitahidi kusogeza gari hadi pale kwenye mti mkubwa pia coplo Dullah utachukua hilo panga hakikisha mtu yeyote asilishike direct bila groves pia inabidi turisachi hili liuaji vizuri tuone kama kutakuwa na ushahidi zaidi.. hakikisheni kila tukio linapigwa picha." Sauti ya mamlaka toka kwa afande mmoja ilisikika. Nilihisi ulimwengu wote nimeutwika kichwani. Askari vilanga walianza kunipekua mifuko ya suruali kwa pupa. Mikononi mwao walivaa mifuko maalum. Ndipo ajabu sikuamini nilichokiona kikitoka kwenye mifuko yangu na kunistua. Macho kodo mdomo wazi.
Mithili ya mtu aliyeyaona ya Firauni baada ya kustaajabu ya Musa. Kiganja cha mtoto mdogo kilichozungushwa hirizi kiliopolewa kwenye mfuko wangu wa suruali na kunifanya nibutwaike kwa mshtuko mkubwa. Pole pole kizunguzungu kilinivaa na fahamu kunivuka kwa mara ya pili nilizima.

********itaendelea*****
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom