Makapuku Forum

Makapuku Forum

6a8e37d8768f4fd7a17c659e3fd22081.jpg
779a42d75c897cd6948e1756ec31e05f.jpg

Mwanzilishi ni Samora Smart Dodd ambaye aliamini inatakiwa kuwepo na siku hiyo kutambua mchango wa akina baba huko Washington DC na kuwakumbusha majukumu yao kimalezi
Kufikia 1920's ikasambaa nchi nzima
Mnamo mwaka 1972 Rais wa Marekani Richard Nixon akaridhia iwe ni siku ya kitaifa.....baada ya hapo ulimwengu mzima ukaiga
......
Kumbe waanzilishi ni Wamarekani!
 
KUTOKA 14

14.Bwana atawapigania nanyi mtanyamaza kimya

Mungu Baba Mwenyezi asante kwa kutuamsha salama asante kutupa uhai asante kwa yote unayotutendea wewe ni Ebenezer hakuna kama wewe..naomba utupe kibali tupone ,tusafiri,bariki kazi za mikono yetu ...wabariki wote mahali hapa waweze kuona ukuu wako..asante sababu unatupigania..tunanyamaza kimya maana matendo yako ni makuu

Tunaomba na kushukuru katika jina la Yesu Amen

MUWE NA SIKU NJEMA YENYE BARAKA
 
Mtoto ajinyonga ugumu wa maisha

MTOTO Paulo Ezekiel amejinyonga kutokana na kile kinachodaiwa ugumu wa maisha.
c186fa60f5d7c42f16d5777a8f20c1fd.jpg
KAMANDA WA POLISI MKOA WA SHINYANGA JUMANNE MURILO

Paulo (17), aliyekuwa anaishi na wazazi wake Mtaa wa Mazinge, Kata ya Ndembezi mjini Shinyanga, alifariki dunia juzi usiku kutokana na kudaiwa kujinyonga kwa kamba juu ya mti jirani na nyumbani kwao.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 10 alfajiri baada ya marehemu kutoka nje ya geti la nyumba yao na kuelekea kwenye mti huo kisha kujipiga kitanzi kunakodaiwa kusababisha kifo chake.
Akizungumzia tukio hilo jana, baba mzazi wa marehemu, Ezekiel Paulo, alisema awali kijana wake alikuwa na ugomvi na marafiki zake ambao ni madereva bodaboda, lakini ugomvi huo ulisuluhishwa na akaendelea na majukumu yake.
Alisema chanzo cha kifo chake hajakifahamu vizuri, lakini mara kwa mara alikuwa akilalamika kuwa maisha ni magumu.
"Ilipofika majira ya saa 10 usiku nilisikia mlango wa chumba cha kijana wangu ukifunguliwa, nikajua ametoka kwenda kujisaidia, lakini muda mrefu ulipopita bila kusikia amerudi, ndipo nikatoka nje na kukuta geti la uani likiwa wazi, nikaanza kumtafuta bila mafanikio," alisema.
Aliongeza: "Niliporudi ndani nikamwamsha mama yake mzazi na wadogo zake wawili wa kike, tukaanza kumsaka ndipo tukamuona akiwa juu ya mti jirani na nyumba yetu, akiwa ameshafariki kwa kujinyonga na kamba."
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Jumanne Murilo, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na jeshi hilo kuhusiana na tukio hilo.
Alisema mwili wa merehemu umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga na unatarajiwa kuzikwa leo kwenye makaburi ya Mtaa wa Dodoma mjini hapa.
So sad RIP ,POLENI NDUGU JAMAA MARAFIKI

Vijana tujitahidi sana kuwa wazi kwa wazazi wetu,kuwa karibu na huduma za kiroho maisha ni magumu lakini je tunajua tunakoenda tukifa?are we ready?Mungu atusaidie
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom