Katika dondoo za bbc ...

Shughuli za kibinadamu ikiwemo ukataji wa miti kiholela nchini Tanzania, wachangia uharibifu mkubwa wa mazingira.

Uchafu wakithiri nchini DRC, watu kumi na wanne wafa kwa ugonjwa wa kipindupindu

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aibuka na ushindi wa viti vingi katika bunge la nchi hiyo

Vyombo vya Usalama nchini Mali vinasema vimeokoa zaidi ya wageni thelathini kutoka katika kituo kimoja cha Utalii, kilichokuwa kikishambuliwa na watu waliokuwa na silaha.

Maofisa nchini Nigeria wamearifu kwamba nusu ya chakula cha msaada kilichokuwa kimepelekwa kwa watu waliosambaratishwa kutoka katika makaazi yao na kundi la wana mgambo wa kiislam hakijawafikia walengwa

Nchini Uganda kuna asasi inayotoa ushauri wa masuala ya kisheria bure kwa wananchi na ili kufanikisha zoezi hilo imekuwa ikitekeleza shughuli zake kupitia mitandao ya kijamii.

Ulaji wa samaki unaonekana kupungua maeneo ya pwani ya Kenya kutokana na gharama ya juu ya kitoweo hicho