Makapuku Forum

The Little Magic angel

Sehemu ya tatu

Ndani ya Miami Beach
Ilipoishia
....
.....
.....
Kwa kuwa Chief Commander alijua kuwa anapambana na kiumbe asichokijua, kiumbe ambacho kinaaminika kuwa kimedondoka kutoka juu, aliwaza labda kiumbe hicho kinaweza kuwa alien; na kinaweza kuwa kiumbe cha ajabu na hatari. Alitumia ujuzi wa kijeshi kwa kujaribu kuwaambia wanajeshi wake wazime tochi pia wakae kimya. Alitaka kujua kama hicho kiumbe kinaona na kinasikia. Na kinatumia njia na silaha gani katika kujilinda? Hayo ndiyo yalikuwa mawazo ya haraka haraka ya Chief Commander McClaw.

Ukimya wa dakika tano bila kufanya chochote kile.sauti za watu waliokuwa wakiomba msaada zilisikika.

McClaw alilijua hilo alitambua fika kuwa watu wanaolia niwazi kuwa walijeruhiwa na kiumbe huyu ambaye mpaka sasa hawajajua ni nani?.

Haikuwa rahisi kuweza kujua nikiumbe gani sababu ya kiza kinene usiku ule.
McClaw alihisi labda kiumbe walichokuja kukabiliana nacho.

Kwa uweledi mkubwa alionao aliamua kufyatua risasi moja angani. lengo kujua kama kiumbe kipo maeneo hayo au kimeondoka?

Baada yakuona hakuna reaction yoyote ile iliyotokea aliaamulu kikosi chake kifanye upekuzi kwa kila kona ya Miami Beach.

Walifanikiwa kukuta miili ya watu 16 waliokwisha fariki na majeruhi 8.

McClaw alipiga simu hospital iliyo karibu na Beach hiyo.ilikuwa ni Mercy Hospital kuita gari ya wagonjwa kuweza kutoa msaada wa haraka kwa wahanga.

Majeruhi walikuwa na hali mbaya sana. Majeraha yao yalionekana ni kama yameunguzwa na moto mkali sana na sio risasi.

Hali hiyo ilimpa mawazo Chief Comander watu "wameunguzwa kiasi hiki na nikiumbe gani ambacho kinatumia moto kama siraha yake yakujikinga?"McClaw alikuwa akijiuliza

Alibaini wenda akawa ni Dragon au Dinosaur "lakini mbona wanyama kama hawa walitoweka dunia miaka mingi iliyopita"aliendelea kujiuliza bila majibu yoyote.

Alimwita kando Detective Kelvin Ago waongee kuhusu vita hii wasiyo ielewa.

"nimepigana na vita nyingi tokea nizaliwe lakini hii sijawahi kuiona"McClaw alifungua maongezi.

"Mkuu chakufanya hapa ni kuwa makini kwa kila hatua tunayopiga"Detective alijibu.

"hakika usiku umeingia sana pia nimechoka sana tukutane kesho asubuhi tupange mbinu mpya ya kupambana na hivi viumbe"alimpa maagizo kisha akapanda gari yake akaondoka.

Ndani ya San Francisco
Wakati Chief Commander anarudi nyumbani baada ya kazi ngumu ya usiku njiani gari yake ilipata tatizo(Jam)"shiiit"alilalama huku akishuka na vifaa kwa hasira hili alitengeneze.

Wakati anaendelea kulitengeneza uso kwa uso na kiumbe kinafanana kabisa na binadamu lakini ni kirefu(giant) sana na kinaonekana kuwa na hasira sana kanakwamba kimekula pili pili.

Je nini kiliendelea hapo usikose sehemu ya nne hapa hapa makapukuz
 
Maelezo yako mazuri
Pia katika mashambulizi niliyoyaelezea ya huko Irak
Mojawapo liliwalenga hasa Washia ila sikuandika sababu ya kufupisha

Ila USA kumuondoa Saddam ndo kuliliamsha dude
.....
Yap! Vice President Dick Cheney akawa anajigamba eti "We will be received as liberators". Liberators my foot. Kuivamia Iraq na kumwondoa Saddam ni mojawapo ya blunders kubwa za kihistoria kwa hawa jamaa. Na kwa vile huwa hawajifunzi, makosa yale yale tena wameyarudia Libya. Leo hii Walibya wanakufa kwenye boti kila leo wakijaribu kukimbilia Ulaya.

Pengine ndiyo maana Trump anasita sita kuliamsha dude dhidi ya yule dogo mnyoa kiduku.
 
And dream never die..

Mwisho umeishika Ak-47 ..
 
Pamoja mdau
Mi nimezaliwa Kidatu kambini(ilivunjwa miaka ya1990 kugeuzwa kuwa Chuo Cha Kipolisi)
Hivyo nikiwa dogo nakumbuka kufaidi beaf,biskuti kubwakubwa za jeshi,maharage ya kopo,kutibiwa hospitali za kijeshi n.k
Mambo ya JWTZ nayafahamu sana na wapo ndugu zangu waliorithi kazi ya msingi
Ila siku hizi hakunacha biskuti wala beaf

........
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…