Mkuu Nitonye, nafikiri unamfahamu
Mkandara wa JF ambaye ni mtu anaishi nje ya Tanzania hadi sasa kama sikosei. Ni msomi mzuri tu na mtu mwenye heshima yake kubwa sana hapa JF. Mie pia nimejifunza mengi sana kwa makala zake.
Ila nakuomba uende ukurasa huu:
https://www.jamiiforums.com/habari-...ofu-lakutana-mbagala-latoa-tamko-zito-11.html
Na ukishasoma Maelezo yake, nafikiri utanielewa kwa nini nilianzisha hii thread. Ukiona Wasomi wa Kiislaam wanaandika hivi, basi huko kijijini hesabu maumivu. Labda wakiona Waislaam vijijini wanabadili dini kwa wingi ili wapate huduma (Makanisa yanaweza hilo kabisa kulifanya ingawa mie SILIPENDI na ningelipenda ni SERIKALI ilifanye, ila ndiyo Serikali yenyewe hiyo tunayo) basi Wasomi hawa na hao wadhamini wao wataanza kufunguka macho.
Ni njia moja KALI sana ila nisingelipendelea kufika huko. Kama alivyosema
Jasusi ni kuwa hata MOU ikivunjwa, baso watu watalialia. Ila ukweli unabaki kuwa sasa watajilaumu wenyewe.
Ni Kama Zanzibar ambavyo wanalilia kuvunja Muungano. Unawapa wajitawale kwa miaka 5 na baada ya hapo ndipo mnakutana tena mezani kama "vipi muungano uvunjwe sasa au mnarudi kuwa mkoa wa Tanzania?"
Ni kujaribu tu kuangalia kipi kifanyike ili kumaliza hizi kelele za kila siku kuhusu Mfumo Kristo ambazo hata Wasomi wazuri kama wale waliopo NSSF ila kwa kuwa wapo dini nyingine basi wamekuwa vipofu.