Makanisa ya kiroho mnatupeleka wapi?

Makanisa ya kiroho mnatupeleka wapi?

Umetoka nyumbani unaamua kuingia kanisani japo kupunguza stress za ugumu wa maisha na matatizo mbalimbali lakini humo kanisani unakutana na michango isiyoisha tena kwa lazima.
Nijuavyo mimi sadaka ni kile ambacho mtu amejaaliwa kukipata
Sasa eti kuna makanisa mpaka wameweka viwango sadaka isiwe chini ya kiasi flani, bado shukrani, bado fungu la 10, bado sadaka ya utumishi, bado sadaka ya madhabahu, bado sadaka ya malimbuko sijui nini. !
Mbaya zaidi kila mahubiri ni kusisitiza utoaji sadaka na michango tu.
Sio siri makanisa yetu mnakatisha tamaa kabisa ukute mtu ni mama wa nyumbani atapataje pesa yote hiyo kama sio mwanzo wa kugombana na mmewe.
Mungu atusaidie.
pole mama,sali nyumbani Mwenyezi MUNGU yupo popote sio kanisani tu,hao Wakatoliki,Walutheri,Waangrikani etc etc ambayo ndio makanisa mama our no 1 anaombewa tena kwa SALA kuu (real!!!) .....utusamehe makosa yetu KAMA SISI tunavyowasamehe WALIOTUKOSEA ,huku ni kumdhihaki Mungu,wakitoka hapo wanatoa amri za ajabu,piga yule,ua yule,weka ndani yule etc etc ,next sunday kanisani tena,....please give me a break
 
KWANI TUNATIBIWA BURE? KWANI SHULE ZAO TUNASOMA BURE? KWA TAARIFA YAKO VITEGA UCHUMI VYAO TUNAJENGA SISI THEN TUNALIPISHWA SISI TENA KWA BEI KUBWA ZAIDI BILA KUJALI MICHANGO YETU. TUMIA KICHWA CHAKO VZURI KUFIKIRI
Askofu anatembelea v8 na ana mjengo mkali huko mtaani,wewe muumini uko na baiskeli yako mtaani na bado unatamba,hahah
 
Mungu Ni Mwema Wakati Wote

Kusifu Na Kuabudu
Maombi Na Maombezi
 
Mi church naenda natoa sakaka moja tu na baada ya salari natoa na fungu la kumi, basi, hizo nyingine sujui sadaka ya utumishi, sijui umisheni, yatima na wajane, sadaka ya madhabahu mara sadaka ya upendo ni mbwembwe tu, utakuta mtu kachenchi buku buku kapanga buku jero kila sadaka anaweka buku, mimi natoa kiwango kizuri kwenye kapu moja tu sadaka kuu.
 
Kanisa unakuta lina sadaka za umeme,maji,jengo,uzinduzi wa kwaya,kununua eneo la jirani na hapo kanisani ili kupanua parking,harambee etc aisee kwa hali hili ya sasa hivi kiukweli,nehiiiiiiiiiiiiiii
 
Makanisa mengineyo ni 'fake'
upload_2018-7-23_11-2-35.png
 
Usipotoa sadaka mchungaji wako atavimba vipi mjini?!
 
Sadaka nitatoa mwenyewe kwa jambo ninaloona mwenyewe linafaa.
Au peleka sadaka kwa watu wenye mahitaji maalumu; Wazee, Watoto; Wagonjwa, Wenye baa la njaa etl ; Ukifanya hivi hata bila ya kwenda kanisani au msikitini utapa baraka.
 
kanisa zuri ni lile ambalo liko KITAASISI kama LUTHERAN, MORAVIAN, KATHOLIC, SABATO, MAKANISA YA KIROHO (EAGT,n.k) tatizo ni zile huduma za ''kanisa la fulani'' huku ndo kuna ile inaitwa '' watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa''. huku kwa kweli mnapigwa. yaani sio siri hasa kina mama na kina dada, huku mnpigwa. WAJINGA NDO waliwao.
mimi nna shemeji yangu alikuwa anafanya biashara ya mchele Mwanjelwa, akaacha kahamia kwa mchungagaji, yaani mpaka kapoteza muelekeo wa maisha, ila tunashukuru MUNGU juzi , amerudi kwenye shughuli yake na anaendelea na kusali
 
Kitu huwa kinanishangaza kuhusu hizi sadaka
Yaani unaenda kabisani unatoa michango ya lazima lakini ukiwa umekaa mahali na watu anakuja maskini ambaye unamuona hali yake ni ngumu, humpi hata 200
Au umekaa unakula hotel unashindwa kumpa maskini aliekaa nje sahani ya wali

Ni uungwana au unafiki wa kijionesha

Halafu isitoshe sijawahi kuona mkiambiwa jamani leo tunaenda kuwapa msaada katika michango yenu vipofu au Yatima

Mungu anawaona wachangishaji wanaojilimbikizia hela zenu na nyie mnaowatajirisha wakati jirani yako analala njaa
Shame
 
Nenda kasali mahali ambapo moyo wako unakuwa na amani...Kulalamika huko inaonesha ulipo si mahala sahihi au tatizo ni wewe mwenyewe!
Si sawa wala sahihi kusema "makanisa ya kiroho" kwa ujumla wake, be specific na mpe Mungu Utukufu!
Be blessed!

Yaani ampe Mungu utukufu kwa kusema kanisa hili wanataka sana sadaka hivyo ni baya na hili halitaki sadaka hivyo ni zuri?Huo ndio utukufu unaoka apewe Mungu?Ujinga sana huo,huo utukufu jipe mwenyewe!
 
kanisa zuri ni lile ambalo liko KITAASISI kama LUTHERAN, MORAVIAN, KATHOLIC, SABATO, MAKANISA YA KIROHO (EAGT,n.k) tatizo ni zile huduma za ''kanisa la fulani'' huku ndo kuna ile inaitwa '' watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa''. huku kwa kweli mnapigwa. yaani sio siri hasa kina mama na kina dada, huku mnpigwa. WAJINGA NDO waliwao.
mimi nna shemeji yangu alikuwa anafanya biashara ya mchele Mwanjelwa, akaacha kahamia kwa mchungagaji, yaani mpaka kapoteza muelekeo wa maisha, ila tunashukuru MUNGU juzi , amerudi kwenye shughuli yake na anaendelea na kusali

Karibia yote uliyoyataja hapo ni makanisa yaliyokufa,inawezekana hata wewe umeshakufa kiroho ndio maana unapenda vitu vilivyokufa.Mimi niko hai,mimi ni simba napenda vitu vilivyo hai,vitu moto.Hizo dini hapo namwachia babu yangu.
 
niliacha kwenda makanisa ya kifedha mwaka 2010 baada ya kuchangia kama million moja hivi ndani ya mwezi mmoja na kubwa zaidi mwezi unaofuata tukaambiwa tuchangie fedha kununua gari la mchungaji na ujenzi wa nyumba yake nikaona isiwe shida, nikajivua ulokole mpaka leo, kanisa lipo morogoro kwa mchungaji john lukindo, ibada tulikuwa tunafanyia pale bene kwenye ukumbi wa kukodi, kanisa hakuna et tuanze kununua gari ya mchungaji badala ya uwanja wa kanisa, nikahisi humu hakuna MUNGU
 
Kitu huwa kinanishangaza kuhusu hizi sadaka
Yaani unaenda kabisani unatoa michango ya lazima lakini ukiwa umekaa mahali na watu anakuja maskini ambaye unamuona hali yake ni ngumu, humpi hata 200
Au umekaa unakula hotel unashindwa kumpa maskini aliekaa nje sahani ya wali

Ni uungwana au unafiki wa kijionesha

Halafu isitoshe sijawahi kuona mkiambiwa jamani leo tunaenda kuwapa msaada katika michango yenu vipofu au Yatima

Mungu anawaona wachangishaji wanaojilimbikizia hela zenu na nyie mnaowatajirisha wakati jirani yako analala njaa
Shame

Mathayo 26:11Yesu aliwaambia kina Yuda,"Maana ziku zote mnao maskini pamoja nanyi,lakini mimi hamnami siku zote"

Ndio nitasaidia maskini lakini siyo kipaumbele changu katika kumtolea Mungu,nitatoa kwenye kazi ya Mungu kwa nguvu zangu zote kwanza kisha wengine watafuatia huko,maskini siyo nafasi ya kwanza.
 
Karibia yote uliyoyataja hapo ni makanisa yaliokufa,inawezekana hata wewe umeshakufa kiroho ndio maana unapenda vitu vilivyokufa.Mimi niko hai,mimi ni simba napenda vitu vilivyo hai,vitu moto.Hizo dini hapo namwachia babu yangu.
ulivyooandika , kwanza naona wazi hupendi UKWELI, na UNA TATIZO, nina hakika mimi naheshimu kanisa kama TAASISI, naamini MAKANISA YA KIROHO (na nayaheshimu) SABATO , CATHOLIC, Moravian N.K , Sasa wewe kusema yamekufa, tayari naona UNA TATIZO la kujihesabia HAKI, NA KUJIONA UMEFIKA MBINGUNI NA HAO WA MAKANISA NILIYOYATAJA WAMEKUFA. Hongera
 
Sifa Kuu Ya Mshirika/muumini Ni Utoaji Sadaka.
Sifa kuu ya muumini siyo kutoa sadaka bali ni kuzishika Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO. YESU KRISTO alisema hivi; "enendeni mkajifunze maana ya maneno haya, sitaki sadaka nataka rehema".
 
Back
Top Bottom